• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Wodi ya Wazazi kunufaisha Wananchi elfu 71 Tarafa ya Mbarika,kutoa huduma bora za uzazi kwa Wajawazito

Imewekwa : March 18th, 2020

Wananchi  71,960, wa Tarafa ya M barika, Wilayani Misungwi, Mkoani Mwanza kuanza kunufaika na huduma za uzazi kwa akina mama wajawazito na watoto baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Wodi ya Wazazi Kituo cha Afya Mbarika.

Hayo yamebainishwa mwishoni mwa wiki  jana wakati wa hafla ya kukabidhi Jengo la Wodi ya Wazazi katika Kituo cha Afya Mbarika, Wilayani Misungwi lililojengwa kwa ufadhili wa Shirika la Global Affair la nchini Canada kupitia Mradi wa Mama na mtoto uliokuwa unatekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi na Halamshauri ya Wilaya ya Kwimba, Mkoani Mwanza kuanzia mwaka 2016.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mradi na hali ya utoaji wa huduma za Afya, katika Kituo cha Afya Mbarika  iliyowasilishwa  na Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mbarika, Dkt, Barnabas Makanza amesema kuwa Jengo la Wazazi limetekelezwa na kujengwa chini ya  usimamizi wa Mhandisi wa Halmashauri kwa gharama ya shilingi Milioni 156 hadi kukamilika, ambapo Shirika la Global Affair la Canada lilitoa fedha shilingi Milioni 146, mchango wa Halmashauri wa shilingi Milioni 5 na jamii imechangia mawe, mchanga na nguvu kazi ya kuchimba msingi  na maji ambao ni mchango wenye thamani ya shilingi Milioni 5.

Dkt, Makanza amesema kwamba Jengo hilo la Wodi ya Wazazi lina uwezo wa kuweka  vitanda 31 vya kuhudumia Wazazi  na uwezo wa kuhudumia Wazazi wanne  kwa wakati mmoja pamoja na uwezo wa vitanda vinne vya kujifungulia (derivery beds), ambapo mradi huo pia umewezesha kujengwa kwa Jengo la Upasuaji ambalo lilikamilika kwa gharama ya shilingi Milioni 194 na tayari limeshaanza kutoa huduma kwa Wagonjwa wa upasuaji.

Akizungumza na Wananchi wa Tarafa ya Mbarika, Afisa Tawala Wilaya ya Misungwi, Zubeda Kimaro kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda, alieleza kwamba amekagua ujenzi wa Jengo hilo na kujiridhisha zaidi kwamba ujenzi umefanyika vizuri ambapo Jengo hilo limejengwa kwa kiwango na ubora, sambamba na kuwa  na vyumba vya kutosha kuweka vitanda vya kuwahudumia akinamama wajawazito kwa wakati mmoja na kusisitiza kuwekwa kwa vitanda hivyo na vifaa tiba vingine ili huduma kwa Wazazi zianze kutolewa mapema, pia ameelekeza Jengo hilo liitwe “Tanya Maternity Ward “ kwa lengo la kutambua mchango wa Meneja mradi huo.

Bi, Zubeda Kimaro, amewataka Wananchi wa Tarafa ya Mbarika kuitumia kikamilifu na kuitunza Wodi hiyo ya Wazazi ili akinamama waweze kujifungua katika hali salama na bora ili kupunguza na kuondoa vifo vya akina mama Wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano, ambapo amewashukuru wawakilishi wa Shirika la Global Affair la nchini Canada ambalo limetekeleza Mradi huu wa Mama na Mtoto  na kuwapongeza kwa juhudi na ufadhili waliutoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kipindi chote.

Mganga Mkuu Wilaya ya Misungwi, Dkt, Zabron Masatu alifafanua na kueleza kwamba, Tarafa ya Mbarika Wilayani Misungwi ni moja kati ya maeneo yaliyokuwa yameshamiri na kuongoza kwenye Vifo vya akina mama na Watoto chini ya miaka mitano kutokana na adha ya kukosekana kwa  huduma za uzazi kwa wananchi hao , hivyo kupitia uongozi wa Halmashauri waliamua kusogeza na kuongeza upatikanaji wa huduma ya Afya ya mama na mtoto kwa kujenga Jengo la upasuaji pamoja na Wodi ya Wazazi kupitia ufadhili wa Mradi wa Mama na mtoto.

Kwa upande wake Meneja Mradi wa mama na mtoto, Tanya Salewski amesema kwamba Mradi wa mama na mtoto umetekeleza miradi ya kusaidia na kuimarisha huduma za uzazi kwa akina mama na watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi tangu mwaka 2016, na wamefanikiwa kujenga Jengo la upasuaji, na sasa  wamekamilisha ujenzi wa Wodi ya Wazazi na mwanzoni kabla ya kuanza  mradi walitoa ufadhili wa gari la Wagonjwa (Ambulance) ambalo limeweza kutoa huduma katika Kituo cha Afya Mbarika,  pamoja na ukarabati wa Jengo la Wagonjwa wa nje katika Zahanati ya Nyamayinza na ukarabati wa chumba cha upasuaji mdogo katika Zahanati ya Mwawile.

Meneja Mradi wa mama na mtoto, Tanya ameeleza kwamba tayari wameweka utaratibu wa kutoa vifaa tiba ambapo wiki ijayo wataleta vifaa tiba hivyo kwa ajili ya matumizi ya  Wazazi kujifungulia, pia  amewaomba Wananchi wa Mbarika kuvitumia vizuri na kuvitunza ili vidumu kwa muda mrefu zaidi pamoja na kuwashukuru kwa ushirikiano waliouonyesha katika mradi huo na kuwataka kuendelea na moyo  huo wa upendo na ushirikiano. 

Katika hafla hiyo ya makabidhiano  Mradi wa Mama na mtoto wameweza kukabidhi na kutoa gari aina ya Toyati Nissan yenye namba za usajili T 796 DKG lenye thamani ya shilingi Milioni 140 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

 

Meneja Mradi wa Mama na mtoto Bi,Tanya Salewski akimkabidhi funguo za Gari aina ya Toyata Nissan yenye namba za usajiri T 796 DKG, Afisa TawalaWilaya ya Misungwi, Bi, Zubeda Kimaro kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misumgwi, Juma Sweda, Gari hilo limetolewa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ili kusaidia shughuli za utoaji wa huduma za afya kwa Wazazi na watoto chini ya miaka mitano.

Mratibu wa Mama na mtoto,Bi, Halima Bumbo (kushoto) akifuatiwa  na Meneja Mradi wa Mama na mtoto Tanya Salewski wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kusaidia watoto kupumua (baby woma ambavyo vimekabidhiwa na mradi huo wa mama na mtoto kwa Wilaya ya Misungwi.

Afisa Tawala Wilaya ya Misungwi, Bi, Zubeda Kimaro akizungumza na Viongozi na Wananchi wa Tarafa ya Mbarika kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda alipomwakilisha katika hafla ya Makabidhiano ya Jengo la Wodi ya Wazazi katikaKituo cha Afya Mbarika Jengo hilo lilijengwa kwa ufadhili wa Mradi wa Mama na mtoto kwa gharama ya shilingi milioni 146, (kushoto ni) Mganga Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Dkt, Zabron Masatu pamoja na Meneja Mradi wa Mama na mtoto, Tanya Salewski (kulia)

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.