• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Sport, Culture and Arts Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Makala : ​Miradi ya Boost yaipaisha sekta ya Elimu Misungwi 2026

Imewekwa : January 9th, 2026

Miradi ya Boost inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya Sita imeendelea kuidhihirisha dhamira yake ya dhati katika kuboresha sekta ya elimu nchini kwa kutoa fedha za BOOST kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya elimu wilayani Misungwi, Mkoani Mwanza. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Dkt. Chrispine Shami,

Hatua hii inalenga kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia pamoja na kuongeza fursa za elimu bora kwa watoto wa wilaya hiyo, kupitia mpango huo, jumla ya shilingi bilioni 1,282,079,136/= mwaka 2024/2025 zimetolewa kwa ajili ya kugharamia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya shule za awali na msingi, fedha hizo ni mchango mkubwa katika kuimarisha huduma za elimu na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa Misungwi kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa tarehe 9 Januari 2026 wakati wa ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa wilayani humo kwa lengo la kujiridhisha na hatua za utekelezaji wa miradi, ubora wa kazi pamoja na matumizi sahihi ya fedha za umma kwa maslahi ya wananchi.

Akizungumza katika ukaguzi wa miradi hiyo  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Dkt. Chrispine Shami, alisema kuwa hakuna sababu ya kukwamisha utekelezaji wa miradi kwa visingizio visivyo na msingi, amesisitiza kuwa miradi hiyo ni ya wananchi, hivyo lazima ikamilike kwa wakati ili iweze kuleta tija iliyokusudiwa mapema.

Dkt. Shami aliwataka watendaji wa Halmashauri, wakandarasi pamoja na vibarua kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa mikataba waliyoingia na alieleza kuwa uwajibikaji na uadilifu katika utekelezaji wa miradi ni muhimu ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora baada ya miradi hiyo kukamilika.

Naye Kaimu Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Bi. Mwanajumbe Zuberi, alieleza kuwa miradi iliyokaguliwa inatekelezwa kwa fedha za BOOST katika kata mbalimbali ikiwemo Kata ya Koromije, ambapo  kuna ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi Kigara pamoja na ukarabati wa Shule ya Msingi Ibongoya ‘A’ kwa gharama ya shilingi 462,179,136.00.

Ameongeza kwamba katika Shule ya Sekondari Gambajiga, kuna ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi utakaogharimu shilingi 330,700,000.00, aliitaja Miradi mingine ni pamoja na ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa na vyoo vyenye matundu sita katika Shule ya Msingi Busagara, Kata ya Usagara, kwa gharama ya shilingi 138,600,000.00.

Katika Kata ya Idetemya, Serikali imefanya ukarabati wa miundombinu ya Shule ya Msingi Bukumbi kwa shilingi 121,000,000.00 na Shule ya Msingi Kigongo kwa shilingi 141,000,000.00 Vilevile, ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na choo chenye matundu sita katika Shule ya Msingi Seth-Benjamin umetengewa shilingi 88,600,000.00, fedha zote zikitokana na mpango wa BOOST.

Kwa upande wao, timu ya Menejimenti ya Halmashauri wamewataka Wataalam na wasimamizi wa miradi kusimamia utekelezaji kwa weledi na uwajibikaji mkubwa, huku wakiwahimiza wananchi kushiriki katika ulinzi na utunzaji wa miradi hiyo, ushirikiano kati ya Serikali na wananchi umeelezwa kuwa ni nguzo muhimu ya kuhakikisha miradi inakamilika kwa ubora unaotakiwa na kuleta maendeleo endelevu katika sekta ya elimu wilayani Misungwi.

Baadhi ya Wananchi wa Wilaya ya Misungwi akiwemo Bw. John Nyanda Mkazi wa Kijiji cha Gambajiga ameeleza  kuridhishwa kwao na utekelezaji wa miradi ya elimu inayofadhiliwa kupitia fedha za BOOST, amesema kuwa miradi hiyo imekuwa mkombozi mkubwa kwa watoto wao na jamii kwa ujumla. Baadhi ya wananchi wamesema ujenzi wa shule mpya na ukarabati wa miundombinu ya shule za awali na msingi utapunguza umbali wanaotembea watoto kwenda shule, kuongeza usalama wao na kuboresha mazingira ya kujifunzia, jambo litakalosaidia kuinua kiwango cha elimu katika wilaya hiyo.

Wakati huo huo Wananchi wameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuwekeza kwenye sekta ya elimu na kusikiliza mahitaji ya wananchi wa maeneo ya vijijini, hata hivyo, wametoa maoni yao wakitaka miradi hiyo isimamiwe kwa karibu ili ikamilike kwa ubora na kwa wakati uliopangwa, huku wakiahidi kushiriki kikamilifu katika ulinzi na utunzaji wa miundombinu hiyo ili idumu na kuendelea kuwanufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.

Matangazo

  • MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA SITA ACSEE MWAKA 2025 July 07, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • Makala : ​Miradi ya Boost yaipaisha sekta ya Elimu Misungwi 2026

    January 09, 2026
  • DAS Misungwi awataka Waheshimiwa Madiwani kutimiza thamani waliopewa na Wananchi

    December 03, 2025
  • DC Misungwi Mhe. Johari Samizi ahamasisha Ujenzi wa Zahanati Mpya Kufuatia Kuhalibiwa na Mvua Zahanati Iliyokuwepo.

    November 15, 2025
  • DC Misungwi awahamasisha Wananchi kujitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa amani na utulivu

    October 27, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.