• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Waziri Simbachawene apongeza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini Wilayani Misungwi

Imewekwa : August 5th, 2023

Serikali yaridhishwa na utekelezaji wa shughuli za mpango wa kunusuru kaya maskini uliogharimu shilingi Bilioni 19.4 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Hayo yamebainishwa Agosti,04,2023 na Waziri  wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe, Boniphace George Simbachawene wakati akikagagua Mradi wa Mpango wa kunusuru Kaya maskini ambapo amesema kuwa Serikali imetekeleza Mradi wa kupunguza umaskini kwa kuanzisha miradi ya ujenzi wa barabara za jamii,uchimbaji wa malambo,visima vifupi na upandaji miti.

Waziri Simbachawene amesema kwamba katika kukuza kipato na kuboresha uchumi wa kaya Serikali imetoa ajira za muda,miradi ya miundombinu na miradi ya shughuli za kuongeza kipato cha kaya,ambapo kupitia miradi hiyo wananchi wamenufaika kwa kujihusisha na shughuli mbalimbali za kuchumi kama biashara ndogondogo,kilimo,ufugaji,ushonaji na kuboresha makazi yao na kaya kujiunga na mfuko afya ulioboreshwa.

Wakati wa ziara yake Mhe, Simbachawene alitembelea na kukagua Mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekonadari ya Wasichana Mwanangwa iliopo Kata ya Mabuki inayojengwa kwa fedha za Serikali kupitia mpango wa Tasaf ambao umegharimu zaidi Milioni 160 na kuridhishwa na hatua ya ujenzi wa mradi huo na thamani ya fedha imeonekana,na kuagiza kujengwa kwa uzio,kutengeneza viwanja vya michezo,kupanda miti na maua ili kuvutia wanafunzi katika kujifunza.

Wakati huo huo Mhe, Waziri Siibachawene  awali  alizungumza na Viongozi na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi katika ukumbi wa Halmashauri  na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia kanuni taratibu na sheria ili kuleta ufanisi katika kutekeleza majukumu ya kila siku ambapo amewataka Viongozi  kuwatendea haki na mema wananchi na watumishi ili kuleta furaha na Amani miongoni mwao.

“Viongozi wanapaswa kufanya kazi kama wazazi kwa kutoa usahauri na kuelekeza vizuri namna ya kutatua changamoto walizonazo watumishi kwa lengo la kuleta maendeleo na kujenga Taifa”.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Misungwi Mhe,Alexender Mnyeti ameipongeza na kushukuru Serikiali ya awamu ya sita kwa kuendelea kutoa fedha za ujenzi ya Miradi mbalimbali ikiwemo Sekta ya Afya,Elimu pamoja na Maji ambapo amsema Serikali tayari imetoa fedha ya kutosha katika Mradi wa Maji kutoka Mbarika hadi Mabuki  ambapo mradi utakapokamilika  wananchi wa Misungwi watanufaika kupitia mradi huo kwa kupata maji safi na salama.

Mnyeti amesema Mradi wa Ujenzi wa barabara ya Mwangwa ,Misasi hadi Kahama utajengwa kwa kiwango cha lami na tayari fedha imeshatengwa kwa ajili ya mradi huo ambapo itakapokamilika itarahisisha usafirishaji wa bidhaa mbalimbali pamoja usafiri kwa wananchi wa Misungwi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Paulo Chacha amesema Serikali haitafumbia macho kamwe kwa mtu yeyote ambaye atathubutu kuwarubuni Wanafunzi kwa namna yeyote   ile au watu wenye nia mbaya ya kutaka kukwamisha ndoto za wanafunzi ili kutofanikisha ndoto zao na malengo yao ya  baadaye waliojiwekea.

“Pamoja  na kuwahakikishia watoto hawa  kama unavyowaona wanapendeza kufikia ndoto zao kama walivyokusudia bila kupepesa jicho wala kurudi nyuma kila mmoja na shughuli yake lazima itimie kwa mujibu wa taratibu zilizopo na lazima wayafikie malengo yao kama walivyojipangia”.

Mhe, Diwani wa Kata ya Mabuki Bw,Petro Malale akitoa shukrani zake za pekee  mbele ya wakazi wa Mabuki  kwa Serikali kwa kuleta fedha kwa ajili ya kukamilisha Miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mwanangwa inayojengwa kwa fedha za Serikali kupitia Mpango wa Tasaf

Wananchi wa Kijiji cha Mwanangwa kata ya Mabuki kwa ujumla wake wakiliza hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe,Boniphace George Simbachawene wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekonadari ya Wasichana mwanangwa hapo jana.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe,Boniphace George Simbachawene akihutubia wakazi wa kijiji cha Mwanagwa jana wakati wa ziara yake ya kukagua Mradi wa ujenzi waShule ya Sekondari ya Wasichana Mwanangwa,ambapo aliridhishwa na hatua ya ujenzi huo.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DAS Misungwi awapongeza Watendaji Halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani katika kuongeza ufanisi na ukusanyaji wa Mapato.

    April 29, 2025
  • Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yafanya ziara ya yatembelea na kupata mafunzo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya nyang'hwale Mkoani Geita

    April 25, 2025
  • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango yaridhishwa na miradi ya maendeleo ya Halmashauri Wilaya ya Misungwi

    April 23, 2025
  • Kamati ya Lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yawataka Watendaji wa Kata na Vijiji kutoa Elimu ya Shughuli za Lishe kwa Wananchi.

    February 27, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.