• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Waziri Mkuu Majaliwa aridhishwa na Ujenzi wa reli ya Mwanza -Isaka Wilayani Misungwi

Imewekwa : October 17th, 2022

Waziri Mkuu wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Mhe,Kassimu Majaliwa Majaliwa aridhishwa na kasi ya  ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Mwanza hadi Isaka Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Akizungumza na Wananchi wa Wilaya ya Misungwi mara baada ya kukagua maendeleo ya Ujenzi huo mapema jana katika eneo la Fela  Waziri Mkuu  ameeleza kuridhishwa na utekelezaji wa Mradi huo uliofikia asilimia 14 ya ujenzi kwa sasa.

Amewataka wafanyakazi kufanya kazi kwa weledi na kujituma pamoja na kuhakikisha kwamba wanautumia ujuzi na maarifa ya ufundi wanaopewa na watalaalam  wa kutoka nje ya Nchi  na kuendeleza kazi za ujenzi na ukarabati mara baada ya kukamilika kwa mradi huo..

Waziri Mkuu Majaliwa  amekemea vitendo vya  baadhi ya Wananchi wenye tabia ya kudokoa na kuiba vifaa vya ujenzi wa reli ya kisasa SGR ambapo amelitaka Jeshi la Polisi  Mkoani Mwanza kuwachukulia hatua Wananchi watakaobainika kufanya uhalifu na wizi wa mali za mradi huo, na kuwaomba  Wananchi kuendelee kutoa ushirikiano  kwa Serikali pamoja na kulinda mali za mradi  ili zitumike kwa ajili ya faida ya Watanzania wote.

Naibu Waziri wa Ujenzi ,Godfrey Kasekenya amesema kwamba ujenzi wa Reli ya kisasa kwa kipande cha Mwanza hadi Isaka wenye kilomita 341ambao unajengwa kwa shilingi Trioni 3.4 unaendela vizuri na Mkandarasi kutoka Nchini China anfanya kazi kwa weledi na Serikali inaendelea kusimamia mradi huo kwa karibu na kuhakikisha malipo yanatolewa kwa wakati.

Mhandisi Kasekenya amebainisha baadhi ya faida na manufaa yatakayopatikana mara baada ya ujenzi wa reli kukamilika ni pamoja na kurahisisha Usafirishaji wa Abiria na mali na usafirishaji wa mizigo ya kibiashara ikiwemo bidhaa za Viwandani na mazao kwa ajili ya biashara na Chakula kwa Wananchi na kuwaomba Wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Wafanyakazi wa mradi ili kuweza kukamilisha ujenzi huo kwa haraka na kwa ufanisi Zaidi.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo nla Misungwi Mhe,Alexender Mnyeti ameipongeza na kushukuru Serikiali ya awamu ya sita kwa kuendelea kutoa fedha za ujenzi ya miradi ya Maji takribani Bilioni 10 pamoja na miradi ya sekta ya Elimu, Afya na miundombinu na kwamba Viongozi wa Wilaya wataendelea kuisimamia kikamilifu Miradi na kukamilika kwa ubora na viwango ili  iwanufaishe Wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Rasilimali wa Shirika la reli nchini Bi. Amina Lumuli amesema ujenzi wa mradi huo  umefikia hatua ya asililimia 14 na kueleza kwamba  kupitia mradi wa ujenzi wa Reli wameweza kutoa ajira kwa Watanzania  zaidi ya wafanyakazi 5400 katika kazi tofauti tofauti pamoja na ufundi na Shirika la reli linaendelea kusimamia kikamilifu ujenzi huo.

Wakati huo huo Mhe, Majaliwa awali alikagua Ujenzi wa Mradi wa  kimkakati wa Daraja la JPM la Kigongo hadi Busisi lenye urefu wa kilomita 3.2 na tayari limefikia  asilimia 53 za ujenzi ambapo hadi kukamilika  utagharimu kiasi cha  Bilioni 699 na ameridhika na  hatua za ujenzi na kueleza kwamba Serikali inaendelea kutoa fedha za malipo ya  mradi huo kila baada  ya hatua moja ya ujenzi kukamilika na kuhakikisha kwamba fedha za mradi zipo.

Amesema kwamba hatua hiyo iliyofikiwa katika ujenzi wa miradi hiyo ni ya kujivunia kwa sababu  mradi huo utakapokamilika utawezesha Wananchi kusafiri na kusafirisha mizigo yao kwa urahisi na kuongeza kipato na uchumi wa taifa.

Mbunge wa Jimbo la Misungwi Mhe,Alexender Mnyeti kushoto, kulia ni Waziri Mkuu Mhe, Kassimu Majaliwa akiongea na wananchi waliofika katika ziara ya Mhe,Waziri Mkuu hapo jana eneo la Fela  ambapo ameishukuru Serikali kwa kuleta  Fedha za Miradi zaidi ya shilingi Bilioni 10 za Miradi ya Maendeleo ikiwa pamoja na maji.

Baadhi ya Wananchi wa Kata ya Fela wasikiliza kwa makini Hotuba ya Waziri Mkuu wakati wa ziara yake hapo jana alipokuwa akikagua Mradi wa Reli ya kisasa ya Mwanza hadi Isaka ambapo amesema Mradi huo umegharimu Trioni 3.4 


Mwonekano wa picha ya kipande cha  Reli ya kisasa(SGR) ya Mwanza hadi Isaka ambapo itakapokamilika itarahisisha usafiri wa abiria pamoja na mizigo .

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.