• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Waziri Mkuu apongeza Halmashauri ya Misungwi kwa Matumizi mazuri ya fedha za Kituo cha Afya Koromije aagiza Bil.1.5 ujenzi wa Hospitali

Imewekwa : March 19th, 2019

Serikali ya awamu ya tano imepanga kutoa shilingi Billioni 1.5 katika mpango wa awamu ya pili za Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza ili kuboresha utoaji wa huduma za Afya kwa Wananchi na kupunguza msongamano wa wagonjwa wengi kupelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-toure.

Mhe,Waziri Mkuu ,Kassim Majaliwa alitoa ahadi hiyo ya Serikali wakati akizungumza na Wananchi wa Koromije Wilayani Misungwi katika ziara yake kwa lengo la kufuatilia utekelezaji na  ufunguzi rasmi wa mradi wa ujenzi na ukarabati mkubwa wa Kituo cha Afya Koromije uliogharimu  fedha zaidi ya  shilingi Milioni 500 zilizotolewa na Ofisi ya Rais -TAMISEMI ambapo Majengo matano yamekamilika ikwemo jengo la Maabara, Upasuaji, Wodi ya Wazazi,Nyumba ya Mganga na jengo la kuhifadhia maiti,sambamba na kujenga majengo hayo matano Halmashauri imefanikiwa kujenga na kukamilisha jengo la ziada la X-ray kutokana na fedha zilizotolewa.

Mhe,Waziri Mkuu wa Tanzania alifurahishwa sana na kuwapongeza Kamati ya ujenzi ,Viongozi wa Wilaya, Kata na Kijiji na wananchi wote kwa kushiriki na kusimamia  kikamilifu ujenzi na ukarabati huo uliofanywa kwa kiwango na ubora, na kuwaomba wananchi kuiamini Serikali ya awamu ya tano ambayo imeweka mkakati madhubuti wa kuboresha na kuimarisha utoaji wa huduma bora za Afya nchini kote, “tayari Vituo vya Afya 340 vimejengwa na kukarabatiwa nchi nzima na Serikali inaendelea kutoa fedha zingine kwa awamu ya pili za ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya na fedha za ununuzi wa madawa na vifaa tiba kwa malengo mapana ya kuboresha huduma za upasuaji mdogo na mkubwa na . Alisema Waziri Mkuu Majaliwa”.

Baadhi ya wananchi wa Koromije wakimsikiliza Waziri Mkuu wakati wa ufunguzi wa kituo cha afya Koromije

Amewaagiza Viongozi wa Halmashauri ya Misungwi kwa kushirikiana na Vijiji kuhamasisha na kuanzisha pamoja na kusimamia ujenzi wa Zahanati katika kila Kijiji ambao ni ujenzi wa angalau  vyumba vitano tu muhimu kwa ajili ya utoaji wa huduma za Afya za awali kwa Magonjwa ya kawaida , pamoja na kuongeza majengo mengine ya Wodi ya Wanaume na Wodi ya watu wenye magonjwa mchanganyiko katika Kituo cha Afya cha Koromije ili kuwezesha wananchi wengi kupata huduma bora za Afya kwa ukaribu na haraka zaidi, na alitoa onyo kwa Madaktari na Watumishi wa Afya wenye tabia ya kuwaelekeza Wagojwa kununua madawa katika maduka binafsi na kuwataka waache mara moja vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na maadili ya taaluma yao na kanuni za utumishi wa umma.

Mwonekano wa nyuma wa jengo la upasuaji katika Kituo cha Afya Koromije

Mhe,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitoa maelezo kuhusu hoja na kero ya uhaba wa maji maeneo ya Koromije iliyotolewa na Diwani wa Kata ya Koromije Mhe.Bilarmin Hilary, alisema Serikali imepanga kutoa fedha za kutekeleza mradi wa maji katika mpango wa Vijiji 17 na kuagiza Mhandisi wa Mkoa kuviunganisha Vijiji vya Kata ya Koromije ili kuondoa adha na kero ya kukosa maji wanayoipata.

Mhe,Waziri Mkuu alionyeshwa kukerwa na suala la Wananchi kukata miti na misitu ovyo sambamba na kuharibu vyanzo vya maji na kwamba ni vitendo ambavyo vinasababisha kukosekana kwa maji ardhini, “ Wananchi acheni tabia ya kukata miti ovyo na Viongozi wa Kata na Vijiji  simamieni  suala la utunzaji wa mazingira pamoja na vyanzo vya maji”.Alikemea Waziri Mkuu.

Aliwataka Wazazi kuwaandikisha na kuwapeleka Shule watoto katika darasa la awali na darasa la kwanza pamoja na kuwahudumia kwa kuwapa mahitaji muhimu ya vifaa vya shule, madaftari, sare na viatu ili kuwawezesha kusoma kwa bidii na Serikali itaendelea kutoa fedha za elimu bila malipo kwa shule zote za Serikali nchini, na amewatka Viongozi wa ngazi ya Wilaya kuhakikisha wanajiridhisha na kupata takwimu halisi ya kila shule ya msingi kuwa na darasa la awali lililo na wanafunzi, hata hivyo aliwatoa wasiwasi Wananchi kuhusu kuchangishwa michango isiyokuwa muhimu kwa ajili ya maendeleo ya shule na kwamba suala la michango ni maamuzi ya Wazazi kwa kushirikiana na Halmashauri pamoja na Wakuu wa Wilaya.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi katika Mradi wa Maji Safi wa Nyahiti Misungwi(kushoto) Mhe,John Mongella Mkuu wa Mkoa wa Mwanza akishuhudia tukio hilo

Awali, Mhe, Waziri Mkuu aliweka Jiwe la Msingi katika ujenzi wa mradi mkubwa wa Maji safi wa Nyahiti –Misugwi unaotekelezwa na Kampuni ya M/S China Civil Engineering Construction Cooperation  CCECC)  chini ya Mhandisi Mshauri Kampuni ya Egis ya Ufaransa na mradi huo unasimamiwa na Mamlaka ya Maji safi na  usafi wa Mazingira  MWAUWASA) ambao utagharimu shilingi Bilioni 12.85 na mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Mei mwaka huu.






Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.