• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Wawekezaji Watanzania wajenga Chuo cha Afya MacWish kwa Bilioni 1.5 Wilayani Misungwi

Imewekwa : July 15th, 2022

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2022 Sahili Geraruma awashauri Watanzania Wazawa kutumia fursa za maeneo na rasilimali zilizopo nchini kuwekeza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Wito huo umetolewa mapema jana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wakati akikagua  na kuweka Jiwe la  msingi katika mradi wa ujenzi wa Chuo cha Afya cha MacWish kilichopo katika Kijiji cha Nyang’homango Kata ya Usagara katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ambacho hadi kukamilika kitagharimu fedha shilingi Bilioni 1.5.

Bw. Geraruma aliwataka Watanzania kutumia fursa zilizopo katika uwekezaji na kuendeleza sera ya Serikali ya awamu ya sita ya kutumia Wazawa kuwekeza katika maeneo ya sekta mbalimbali kwa lengo la kutatua na kupunguza changamoto ya ajira kwa Vijana kwa kuzalisha ajira za kutosha hapa nchini.

Naye Mkurugenzi wa Chuo hicho Bw,Patrice Makasi ametoa rai na  kuwaomba Wananchi kutoa ushirikiano katika kuwekeza, kuleta maendeleo na kukuza uchumi  katika sekta ya uwekazaji na kuwahakikisha kwamba watazalisha Wataalamu  wenye viwango bora ndani ya nchi na nje ya nchi katika kada ya Afya ili kuleta ushindani katika soko la ajira.

Aliongeza kwamba katika mikakati ya Chuo hicho katika  mipango ya utoaji wa elimu bora kina uwezo wa kudahili  Wanafunzi 1,500 kwa mwaka huu wa masomo  2022/2023 wanatarajia kudahili Wanafunzi 250 katika kozi ya Ufamasia na Utabibu na kusisitiza Watanzania kutumia fursa za masomo katika Chuo hicho.

Kwa upande wake Afisa wa Masoko wa Chuo hicho Bw,Boniphace Mwaliki amesema kuwa lengo kubwa ni kuandaa  Wataalamu wa Afya wenye ubora wa kimataifa wenye kuleta tija katika soko la ajira na kusisitiza  kuwa  ulipaji wa ada ni nafuu unaweza kulipa kwa awamu nne ,na wamezingatia ubora katika utoaji wa Elimu hapa nchini.

Wakati huo huo, Mbunge wa Jimbo la Misungwi Mhe, Alexander Mnyeti amebainisha kwamba Serikali ya awamu ya sita katika mwaka wa fedha 2021/2022 imetoa takribani shilingi Bilioni 3 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya sekta ya Afya  fedha ambazo zimetumika kujenga miundombinu ya majengo ya Hospitali,ya Wilaya, Kituo cha Afya cha Usagara na baadhi ya Zahanati.

Ametoa shukrani za dhati kwa Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha ambazo zimeweza kutekeleza mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Usagara ambacho kimewekewa jiwe la msingi kilichogharimu shilingi 257,950,000/=  ambapo majengo yaliyojengwa ni pamoja na jengo la Wagonjwa wa nje (OPD) , jengo la Maabara, na Kichomea taka.

Naye mkazi wa Usagara Bw,Faustine Joseph ameishukuru Serikali kwa kujenga Kituo cha Afya Usagara na kwamba  kitarahisisha kupatikana kwa huduma ya Afya kuwa karibu na wananchi na kuondoa adha ya umbali kwenda kutafuta huduma maeneo ya mbali na  kusafiri kwa umbali mrefu kwenda Misungwi , Bukumbi hospitali  na Butimba Mwanza mjini kutafuta huduma ya matibabu hivyo  kwa kupata Kituo hiki cha Afya kitasaidia kuondoa adha hiyo kwa wakazi wa Usagara.

Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2022 katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi zimeweza kupitia Miradi saba yenye thamani ya Bilioni 3.2 yote ikiwa katika hali nzuri ya utekelezaji na imejengwa kwa kiwango na ubora.

  

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Bw,Sahili Geraruma (kushoto) akikagua Mradi wa Ujenzi wa Chuo Cha Afya MacWish kilichopo kijiji cha Nyanghomango Kata ya Usagara wakati wa uwekaji wa jiwe la Msingi,kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Misungwi  Mhe,Veronika Kessy.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Bw,Sahili Geraruma(wa pili kutoka kulia) akiwa na Wakurugenzi wa  Chuo cha  MacWish Bw. Ernest Wish( wa kwanza kulia) na Patrice Makasi( wa tatu kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Uwekaji wa Jiwe la Msingi.an Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Veronika Kessy.

Bw. Edward Wish  ((kushoto) ambaye ni Baba mzazi wa Wakurugenzi wa Chuo cha Afya cha MacWish akiwa ameshika Mwenge wa Uhuru  2022 akiwa katika picha ya pamoja wakati wa uwekaji wa jiwe la Msingi Chuo cha MacWish pamoja na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2022  Bw,Sahili Geraruma wa pili kulia, na  katikati ni Mkuu wa Wilaya Mhe, Veronica Kessy,wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Misungwi Mhe, Kashinje Machibya.   

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.