• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Watu wenye ulemavu watakiwa kuchangamkia fursa za mikopo kubadili maisha Wilayani Misungwi

Imewekwa : December 5th, 2022

Watu wenye Ulemavu watakiwa kutumia fursa za Mikopo kubadili maisha yao Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi na Diwani wa Kata ya Usagara Mhe,Kashinje Machibya amewataka Watu wenye Ulemavu kutumia fursa za Mikopo ya asilimia 10 asilimia ambapo asilimia 2 ni ya Watu wenye ulemavu  wakati wa Maazimisho ya siku ya watu wenye Ulemavu.

Hayo yamesemwa tarehe 3/12/2022 kwenye maazimisho ya Watu wenye Ulemavu yaliyofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Msingi Maalumu ya Mitindo Misungwi ambapo amewataka Watu wenye ulemavu kukopa na kurejesha mikopo hiyo isiyokuwa  na riba ili kuweza kujikwamua kwa kufanya shughuli za maendeleo na  kujipatia kipato ambapo mikopo hiyo inatolewa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Bwana Machibya amesema kuwa Mwaka wa fedha 2022/2023 wametenga zaidi shilingi Bilioni moja  ambazo  asilimia 40  kwa maendeleo na fedha hizo asilimia 10 ni kwa ajili ya mikopo kwa vikundi.Amesisitiza Ofisi ya Maendeleo ya Jamii waendelee kutoa mikopo kwa uaminifu na uadilifu kwa vikundi mbalimbali kwani fedha ipo kwa ajili yao.

Kwa upande wake Mtaalamu Kiongozi  Ujumuishi kwa Wenye Ulemavu Mwl.Benjamin L Kihwele wa Shirika la Sense International Tanzania linalofanya kazi kwa Ushirika na ADD International  na Tanzania Cheshire Foundation katika kutekeleza mradi wa Elimu jumuishi uitwao Task Order –T051 kwa Ufadhili wa FCDO kupitia Serikali ya Uingereza amesema kuwa kazi kubwa ya Mashirika haya ni kubaini watoto wenye ulemavu ,kuwapima ESRAC kwa kubaini mahitaji maalumu ya ujifunzaji na kuwaandikisha shule jumuishi jirani na nyumbani kwao.

Vilevile Mwl.Kihwele ameongeza kuwa wamekuwa wakifundisha walimu jinsi ya kutumia mbinu shirikishi za ujifunzaji katika madarasa jumuishi ili kuweza kubaini watoto wenye ulemavu katika mazingira tofauti yanayowazunguka,na kutoa rai wa wadau na wazazi na walezi kutoa ushirikiano kwa kuwatoa watoto wao wenye ulemavu ili wapate huduma bora,Elimu kulingana na kiwango chao; na kuwashukuru Wageni walikwa na wadau mbalimbali waliojitokeza katika Maazimisho hayo.

Kwa upande wake Bw.Malimi Luhanya  ambaye ni Mratibu wa Shirika lisilo la Kiserikali APDM Mkoa wa Mwanza linalojihusisha na Watu wenye ulemavu  amesema kuwa kuna umuhimu wa elimu na mafunzo  kutolewa kwa watu wenye ulemavu juu ya mikopo ya asilimia 10 ambayo inatolewa na Halmashauri isiyo kuwa na riba ambapo asilimia 2 ni kwa watu wenye ulemavu ili wawe sifa na vigezo vya kukopesheka na kurejesha mikopo hiyo kwa wakati.Pia Shirika hilo wanatoa ushauri na elimu kwa wazazi wenye watoto wenye mahitaji maalumu kwa kuwajengea uwezo na kuwaandikisha watoto hao kulingana kiwango chao.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri wa Wilaya ya Misungwi Bi.Juliana Mwongerezi amesema mikopo ya asilimia 10 inatolewa katika Halmashauri zote nchini bila riba na asilimia 2 ni kwa watu wenye ulemavu ambapo amewaomba kuchangamkia fursa ya mikopo  kwa lengo la kuzalisha faida endelevu ili kuweza kurejesha mikopo hiyo kwa wakati na kuwa mpango mkakati wa kujikwamua sehemu moja kwenda nyingine,na ni ruksa kwa kikundi au mtu mmoja mmoja kukopa kwa watu wenye ulemavu. Bi.Mwongerezi amesisitiza kuwa moja ya vigezo vya Mikopo ni pamoja na uaminifu kwa mwanakikundi katika kukopa.

“Suluhisho la mabadiliko kwa maendeleo jumuishi kwa mchango wa ubunifu katika kuchagiza dunia na yenye Usawa” kauli mbiu.


Mtaalamu Kiongozi Jumuishi kwa wenye ulemavu Mwl.Benjamini Kihwele akiongoza mjadala katika siku ya Maazimisho ya siku ya watu wenye ulemavu katika ukumbi wa Shule ya Msingi Mitindo siku ya Jumamosi tarehe 3/12/2022

Mwenyekiti wa Halmashauri wa Wilaya ya Misungwi Mhe.Kashinje Machibya aliyesimama, akiwa mgeni rasmi katika Maazimisho ya siku ya Watu wenye Ulemavu katika Ukumbi wa Shule ya Msingi Mitindo Misungwi yalifanyika siku ya Jumamosi tarehe 3/12/2022

Baadhi ya viongozi (alivaa suti ya daki bluu katikati ni Mratibu wa APDM Mkoa wa Mwanza)na wadau mbalimbali waliofika katika maazimisho ya siku ya Welemavu siku ya Jumamosi 3/12/2022 katika ukumbi wa Shule Maalumu ya Mitindo 

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.