• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Watoto wenye umri wa Miaka 5 -14 Kupata Dawa ya Minyoo na Kichocho Wilayani Misungwi

Imewekwa : November 23rd, 2023

Wazazi na Wananchi wahamasishwa na kushauriwa kuwaandaa na kuwaruhusu Watoto wa umri wa miaka 5 hadi 14 kupata Dawa ya matibabu ya Ugonjwa wa Minyoo na Kichocho Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Paulo Chacha kupitia kwa Mwakilishi wake Afisa Tawala Wilaya ya Misungwi Bw. Jonas Kamugisha ambaye amewataka Viongozi na Watendaji kutoa elimu na kuhamasisha jamii na Wazazi kuwaruhusu Watoto kujitokeza kupata Dawa ya kuua wadudu wa Kichoo na Minyoo

Mhe, Kamugisha ambaye ni Afisa Tawala Wilaya  ameyasema hayo katika kikao cha Kamati ya Afya ya msingi ya Wilaya kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa ajili ya kuweka mikakati na maandalizi ya utoaji wa Dawa ya matibabu ya Ugonjwa wa Kichocho na Minyoo amabyo hutolewa kwa watoto wote wa umri kuanzia miaka 5 hadi 14.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw. Christopher Legonda amesema na kuwataka Viongozi na Watendaji kuendelea kuhamasisha na kutoa elimu kwa Wananchi ili kuongeza ulewa wa namna ya kuchukua tahadhari na kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya kuambukiza na magonjwa ya mlipuko ikiwemo ugonjwa wa Kipindupindu ambao umeshaanza kutokea katika maeneo mengine ya Mikoa jirani ya Mara na Simiyu sambamba na kuwashauri Wazazi wote kutoa hamasa kwa watoto kujitokeza kupata dawa ya Minyoo na Kichocho katika vituo vilivopangwa kwenye shule za msingi na Sekondari siku ya Ijumaa na Jumamosi wiki hii..

Naye, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Dkt. Clement Morabu ametoa rai kwa Viongozi na Watendaji kuendelea kutoa elimu na hamasa kwa Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari na kujikinga na maambukizi ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya kuambukiza na magojwa ya mlipuko na kushauri Wananchi kutunza mazingira,kufuata na kuzingatia kanuni bora za Afya na kuzingatia maelekezo na ushauri unaotolewa na Wataalam wa Afya.

Dkt. Morabu amesema kwamba kuna umuhimu mkubwa jamii ikafahamu kuhusu namna magonjwa haya ya Kichocho na Minyoo yanavyoambukizwa na kusababisha athari katika mwili wa binadamu ikiwemo kuharibu ini,  na kusababisha Kansa ya utumbo, alieleza baadhi ya aina ya Kichocho na athari zake na kwamba Serikali imeweka mpango  na Kampeni yaa kutoa dawa ya matibabu ya Ugonjwa Kichocho na Minyoo kwa watoto wote kuanzia umri wa miaka 5 hadi 14 na zoezi hili linafanyika mwezi Novemba kwa kila mwaka kabala ya Wanafunzi hawajafunga shule.

Dkt. Morabu amewasihi Viongozi na Watendaji hao kuendelea kutoa elimu kwa Wazazi na Wananchi kuwaruhusu watoto kujitokeza kupata dawa hizo na kuwaomba  Wazazi na Walimu wa Shule za msingi na Sekondari kuwandaa watoto kikamilifu kwa kuwapatia chakula cha kutosha kuweza kuhimili uwezo wa dawa mwilini ambapo utaratibu wa utoaji wa Dawa hizo hutolewa kwa kuzingatia uzito wa mtoto mwenyewe.

Wakati huo huo, Afisa Afya wa Wilaya  ya Misungwi Bw. Dismas Dotto ametoa elimu katika mada ya Mlipuko wa Ugonjwa wa Kipundupindu na kuwakumbusha Wajumbe kuhusu majukumu yao ikiwemo kuhamasisha na kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu kujikinga na maambukizi pamoja na kuwa tayari na kukabiliana na mlipuko wa magonjwa mbalimbali ikiwemo Ugonjwa wa Kipindupindu uliojitokeza hivi karibuni mwaka huu katika Mikoa 6 na baadhi ya Wananchi waliambukizwa ambapo kwa sasa hakuna Mgonjwa mpya ambaye ametolewa taarifa.

Bw. Dotto amebainisha baadhi ya mikakati ambayo Wilaya imeendelea kuchukua ni pamoja na kuhamasisha Wananchi kujenga vyoo,Wananchi kuendelea kunawa mikono mara kwa mara, kuendelea kuchemsha maji na kuweka mazingira ya majumbani katika usafi,  ili kuweza kuepuka na kukabiliana na Magonjwa ya mlipuko ikiwemo Ugonjwa huu wa Kipindupindu.

Badhii ya Wajumbe walioshiriki katika kikao hicho ni pamoja na Viongozi wa Madhehebu ya Dini, Wataalam na Watendaji wa Idara ya Afya, Elimu, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa jamii , Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini Maafisa Afya na Maafisa Tarafa wote wa Wilaya ya Misungwi kwa lengo la kuwapa uelewa na kuweza kupeleka elimu katika jamii na kuongeza hamasa kwa Wananchi juu ya masula ya kujikinga na magonjwa mbalimbali ya kuambukiza na magonjwa ya mlipuko.

Baadhi ya Wajumbe walioshiriki katika kikao hicho na Viongozi wa madhehebu ya Dini katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Novemba,22,2023


Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Dr.Clement Morabu akitoa maelezo juu ya zoezi la kupatiwa dawa za Minyoo na Kichocho kwa Watoto wenye umri wa miaka 5 hadi 14 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Novemba,22,2023.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.