• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Watendaji wa Kata na Vijiji wasiosoma taarifa za Mapato na Matumiizi sasa kukiona ---- Asema DC Misungwi

Imewekwa : October 2nd, 2018

Watendaji wa Kata na Vijiji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi watakiwa kusoma taarifa za Mapato na Matumizi katika Mikutano ya  kisheria ya kila robo mwaka ili kuleta ufahamu na uelewa  kwa Wananchi kuhusu fedha zinazotolewa na zinavyotumika katika utekelezaji wa  miradi katika maeneo yao.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe, Juma Sweda ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Ngudama katika Kata ya Bulemeji baada ya kukamilisha Ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya sekta mbalimbali inayotekelezwa katika vijiji vya Kata hiyo kwa ufadhili wa fedha za Serikali,Wahisani pamoja na michango na nguvu za Wananchi.

Mhe,Juma Sweda amewataka Watendaji wa Kata na Vijiji wote kufanya kazi na kuwajibika kikamilifu hususani kusoma taarifa za Mapato na Matumizi ya fedha zote zinazotolewa na Serikali,Wafadhili na Wahisani mbalimbali pamoja na michango na nguvu za Wananchi kwa lengo la kuongeza uwajibikaji, uwazi na kuleta imani kwa Wananchi kushiriki katika kuchangia na kutekeleza miradi mbalimbali na kuona na kuhakikisha namna fedha hizo zinavvotumika kutekeleza vizuri miradi husika na hatimaye kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa Wananchi.

Amewataka pia Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Vikao na Mikutano hiyo ya vijiji kwa ajili ya kujadili ajenda ya taarifa ya mapato na matumizi na kuwaomba washirikiane na Kamati za Siasa za Kata na Vijiji ili kutekeleza ipasavyo Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 na Viongozi hao wa Chama wahakikishe Ilani inatekelezwa vizuri katika sekta zote, “ na huo ndio utaratibu na kanuni za Chama cha Mapinduzi katika kuwaletea maendeleo Wananchi wake” Alisisitiza Mkuu wa Wilaya, Juma Sweda. 

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi,Mhe, juma Sweda akihutubia Wananchi wa Kijiji cha Ngudama Kata ya Bulemeji wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika maeneo ya Viwanja vya Ngudama.

Mhe,Sweda amewataka Wananchi kutumia fursa ya Kilimo na  kuandaa mashamba kikamilifu kwa kuweka mbolea aina ya Samadi na kulima kwa wakati mara msimu wa mvua utakapoanza kwa kuzingatia kanuni bora za Kilimo na ushauri wa Wataalam wa Ugani /Kilimo kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao ya Chakula na Biashara na hatimaye kuongeza kipato na uchumi wa Kaya na jamii kwa ujumla.

Baadhi ya Wananchi na wakazi wa Kijiji cha Ngudama,Kata ya Bulemeji wakisikiliza kwa makini maelekezo na maagizo ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi kwenye Mkutano wa hadhara

Amewaasa Wananchi hao kutouza ardhi na mashamba yao kiholela na badala yake wavute subira na kuyatunza kwa manufaa na faida kubwa ya baadae kutokana na kupanda kwa thamani ya ardhi na kuwaomba wapime maeneo hayo kupitia sera ya upimaji shirikishi inayoendelea kutekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Makampuni binafsi ya upimaji wa Ardhi kwa lengo la kutekeleza na kufikia adhima ya jenzi wa uchumi wa Viwanda.

Mhe,Juma Sweda amewahamasisha na kuwataka Wananchi wa rika mbalimbali kuanzisha na kujiunga katika vikundi mbalimbali vya uzalishaji mali na kutumia fursa ya Mikopo inayotolewa na Serikali kupitia makundi ya akinamama, Vijana na watu wenye ulemavu na kuweza kunufaika na kufaidika na mikopo ya fedha hizo kuanzisha miradi mbalimbali ya kuinua kipato na kukuza uchumi katika jamii.

Awali  katika ziara yake Mkuu wa Wilaya huyo na Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo walitembelea na kukagua shughuli na kuona utekelezaji wa miradi ya sekta mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Kisima cha Maji katika Kijiji cha Mwalwigi, Ujenzi wa miundombinu katika Shule ya Sekondari ya Kata ya Mamaye na kuona Vikundi vya Watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Kata ya Ukiriguru, ujenzi wa mabweni na Ukamilishaji wa miundombinu ya Maabara katika Shule ya Sekondari ya Paulo Bomani, Ujenzi wa Jengo la Zahanati ya Kijiji cha Nyamatala, Kata ya Ukiriguru.

Jengo la Maabara tatu za Sayansi lililojengwa katika Shule ya Sekondari Paulo Bomani Kata ya Ukiriguru na sasa linaendelea kukamilishwa..

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe, Juma Sweda akishiriki kupaka rangi kwenye ukuta wa  ndani ya Jengo la Maabara yanayoendelea kukamilishwa kwa gharama ya shillingi Millioni 50 zilizotolewa na Serikali hivi karibuni katika Shule ya Sekondari Paulo Bomani Kata ya Ukiriguru.

Vile vile, wameweza kukagua na kuona ujenzi wa Choo katika Shule ya Msingi Mwalogwabagole na ujenzi wa Nyumba ya Mtumishi katika Zahanati ya Buhunda pamoja na kukagua shughuli za mradi wa Uzalishaji mali wa Kikundi cha akinamama cha Ngudama ambapo Mkuu wa Wilaya alipongeza juhudi za  Kikundi hicho cha akinamama ambao wanatengeneza bidhaa za asili vya matumizi ya Nyumbani na kuwasihi waendelee na kazi hiyo na wengine waige na kujiunga kwenye vikundi vya ujasiliamali.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.