• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Sport, Culture and Arts Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Wananchi wahimizwa kutunza Miundombinu Miradi ya Maendeleo kwa Manufaa ya vizazi vijavyo Wilayani Misungwi

Imewekwa : December 8th, 2023

Viongozi,Wananchi watakiwa kuitunza  vizuri Miundombinu ya Miradi ya Elimu Jumuishi kwa manufaa ya wanafunzi Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Wito huo umetolewa jana 7, Desemba, 2023 na Afisa Msimamizi wa Elimu maalumu OR-TAMISEMI Bi.Anna Mark katika hafla fupi ya kukabidhi ukarabati wa vyumba 7 vya madarasa na Ujenzi wa matundu ya vyoo mara baada ya kukamilika iliyofanyika katika Shule ya Msingi Mabuki chini ya Mradi wa Elimu Jumuishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ambapo amewataka Wananchi na wadau mbalimbali kuilinda na kuitunza miundombinu hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Aidha Bi.Mark amesema kuwa vifaa vinatolewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu ni kwa ajili ya watoto wote wenye mahitaji maalumu  waliobainishwa na wataalamu kutoka ngazi ya Halmashauri vifaa hivyo ni vya kujifunzia na vifaa saidizi kama viti vya magurudumu pamoja na vifaa vya kukuza maandishi kwa wale wenye uoni hafifu.

 Mkurugenzi wa Sense International Tanzania Bi.Naomi B Lugoe amesema kuwa baadhi ya malengo ya mradi huo ni pamoja na kufanya utambuzi na uchunguzi wa hali ya ulemavu ili kubaini mahitaji ya ujifunzaji kwa watoto husika,kuhamasisha uandikishaji wa watoto wenye ulemavu watakaobainika na kupimwa kwenye vituo vya upimaji wa kubaini mahitaji maalumu ya ujifunzaji,kuimarisha ujuzi kazi kwa walimu ili wawe na mbinu za kuwasaidia wanafunzi wenye ulemavu kuweza kujifunza katika madarasa jumuishi na kuboresha miundombinu ya shule za mradi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bi Ester Msoka ambaye Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Misungwi amesema kuwa Serikali inaendelea kushirikiana na Wadau mbalimbali wa Elimu kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kuboresha huduma ambazo zinatolewa kwa watoto wenye mahitaji maalumu na kutoa wito kwa wadau wengine waendelee kutoa huduma maeneo mengine.

Sambamba na hilo ameongeza kuwa si watoto tu bali hata watu wazima wenye ulemavu wanapewa vipaumbele katika Nyanja tofauti ikiwemo kiuchumi na kijamii pamoja na miundombinu na kuwaomba wadau waendelee kutoa ushirikiano katika Sekta mbalimbali za maendeleo.

Wakati huo huo Diwani wa Kata ya Mabuki Mhe.Petro Lutonja  ameshukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta mradi wa Elimu Jumuishi wenye thamani Shilingi Milioni 15 katika Kata ya Mabuki ambapo fedha hizo zimeweza kukarabati vyumba 7 vya madarasa pamoja na ujenzi wa matundu ya vyoo.

Mhe. Lutonja ametoa wito kwa Wannachi kuwa pindi Mradi wa Maji utakapofika  kutoka Ihelele kwenda Misasi hadi Mabuki,Wananchi watoe ushirikiano  wa kutosha na hakutakuwa na fidia kwenye njia zitakapopita bomba ili kurahisisha kupata huduma ya maji kwa Wananchi wa Mabuki.

Naye Mwanafuzi wa Shule ya Msingi Mabuki Bi. Rehema John ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuleta mradi wa maendeleo Ujenzi wa matundu ya vyoo na ukarabati wa madarasa katika Shule ya Msingi Mabuki na kuahidi kutunza vizuri miundombinu iliyojengwa kupitia mradi wa elimu jumuishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Mkurugenzi wa SENSE International Tanzania Bi.Naomi Lugoe akiongea na Wadau mbalimbali wa Elimu jana wakati wa kukabidhi ukarabati wa vyumba 7 vya madarasa pamoja na ujenzi wa matundu ya vyoo katika Shule ya Msingi Mabuki.

Baadhi ya Wadau wa Elimu wakisikiliza na kupokea maoni ya Wataalamu kutoka TAMISEMI jana wakati hafla fupi ya kukabidhi ukarabati wa majengo ya madarasa na vyoo katika Shule ya Msingi Mabuki.

Mwonekano wa Vyoo vipya ambavyo vimejengwa kupitia Mradi wa Elimu jumuishi na Shirika la Sense Internatinal katika Shule ya Msingi Mabuki.

Matangazo

  • MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA SITA ACSEE MWAKA 2025 July 07, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • Makala : ​Miradi ya Boost yaipaisha sekta ya Elimu Misungwi 2026

    January 09, 2026
  • DAS Misungwi awataka Waheshimiwa Madiwani kutimiza thamani waliopewa na Wananchi

    December 03, 2025
  • DC Misungwi Mhe. Johari Samizi ahamasisha Ujenzi wa Zahanati Mpya Kufuatia Kuhalibiwa na Mvua Zahanati Iliyokuwepo.

    November 15, 2025
  • DC Misungwi awahamasisha Wananchi kujitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa amani na utulivu

    October 27, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.