• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Wanafunzi 7,879 Wilayani Misungwi kufanya Mitihani ya Darasa la Saba kesho na kesho kutwa.

Imewekwa : October 6th, 2020

Watahiniwa 7,879 wanatarajiwa kufanya Mitihani ya kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2020 katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Bw, Frank Magabiro ameeleza haya  ofisini kwake mapema wiki hii,  kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba, alisema kwamba Halmashauri hiyo imeshakamilisha maandalizi ya zoezi la kitaifa la uendeshaji wa Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi kwa Wanafunzi wa darasa la saba mwaka 2020.

Afisa Elimu Magabiro amesema kwamba kuna jumla ya Watahiniwa 7,879 waliosajiliwa na wapo tayari kwa ajili ya kufanya Mtihani huo wa kumaliza Elimu ya msingi itakayofanyika kwa siku mbili mfululizo  ambapo miongoni mwao Wavulani ni 3,740 na Wasichana ni 4,157 na tayari maandalizi ya msingi yapo vizuri hususani suala la usafiri na usambazaji wa Mitihani kuelekea katika vituo 146 yamekamilika .

Bw, Magabiro alifafanua kuwa kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la Mitihani la Tanzania inaeleza kwamba Mitihani hiyo ya kumaliza Elimu ya Msingi itaanza siku ya Jumatano tarehe 7 mwezi oktoba mwaka 2020 kuanzia saa 2.00 asubuhi kwa watahiniwa wote  kufanya masomo ya Kiswahili , Hisabati na Sayansi  na  mitihani hiyo itakamilika siku ya Alhamisi ambapo watafanya masomo ya English Language na Maarifa ya jamii.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya Wanafunzi katika masomo, Bw, Magabiro alisema kwamba Wanafunzi wote wameendaliwa vizuri kimasomo ambapo mada zote zilifundishwa vizuri  na kukamilishwa, na wamefanya majaribio ya kutosha pamoja na Mitihani mbalimbali ya ngazi ya Kata, Wilaya ukiwemo  na Mtihani wa MOCK Mkoa, pia wamejengwa vizuri kisaikolojia na Walimu pamoja na Wazazi ‘’alibainisha kwamba  kimsingi Watahiniwa wote wapo vizuri kwa ajili ya kufanya Mitihani hiyo’’. Alisisitiza Bw, Magabiro.

Afisa Elimu huyo ameongeza kuwa kwa upande wa Watahiniwa wa Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi mwaka huu 2020 kumekuwepo na ongezeko la Watahiniwa 87 ukilinganisha na Watahiniwa 7,792 waliohitimu Elimu ya Msingi mwaka 2019 katika Halmashauri ya Misungwi.

Bw, Frank Magabiro ameeleza kwamba baadhi ya  sababu iliyowezesha kuongezeka kwa Watahiniwa hao ni pamoja na udhibiti wa utoro kwa Wanafunzi, mwitikio wa Wazazi na jamii katika suala la Elimu sambamba na utekelezaji wa Sera ya Serikali ya utoaji wa Elimu bila malipo ambayo inatekelezwa katika Shule zote za msingi 147, zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi zikwemo Shule za Serikali 139 na shule binafsi 8.

Baadhi ya Wasimamizi na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Wilayani Misungwi wakiwa katika Semina maalum ya maandalizi ya Mitihani ya darasa la saba mwak 2020 katika Ukumbi wa Shule maalum ya Mitindo hivi karibuni.

Amewataka Watahiniwa hao kufanya mitihani yao katika hali ya amani na  kuwa watulivu na kutambua kwamba Mtihani huo wa Taifa ni sawa na Mitihani mingine na kuwatakia afya njema wakati wote na kuwaomba wamtangulize Mungu awasaidie, sambamba na kuwaomba wasimamizi wa Mitihani kusimamia vizuri mitihani hiyo kulingana na maelekezo na taratibu zilizotolewa na Baraza la Mitihani la Tanzania.


Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Misungwi, Frank Magabiro akiwa ofisini kwake kwa ajili ya maandalizi maalum ya zoezi la Mitihani ya darasa la saba mwaka 2020.


Viongozi na Maafisa Elimu wa ngazi ya Mkoa na Wilaya wakiendelea na utoaji wa maelekezo mbalimbali katika semina maalum ya maandalizi ya Mitihani ya darasa la saba mwaka 2020 kwa Wasimamizi na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Wilayani Misungwi. 

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.