• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Uzinduzi kampeni ya vyumba vya madarasa Wilayani Misungwi

Imewekwa : July 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Mwanza azindua ujenzi wa Vyumba 24 vya Madarasa Shule ya msingi Mbela Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe,Mhandisi Robert Gabriel ameungana na Wananchi mapema hapo jana 25,07,2022 katika kuchimba Misingi ya ujenzi wa Madarasa 24 katika viwanja vya shule ya Msingi Mbela ikiwa ni ishara ya Uzinduzi wa Kampeni kubwa ya Kizalendo ya Ujenzi wa Miundombinu ya Madarasa kwa Shule za Misingi na Sekondari Mkoani Mwanza.

Akizungumza na Wananchi ,Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe,Mhandisi Robert Gabriel amesema kampeni kubwa ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa ni matokeo na ushirikano wa viongozi mbalimbali ndani ya Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kuwaweka watoto katika mazingira rafiki ya kujifunza na kujifunzia  na kwamba kazi hiyo itafanya kwenye kila Halmashauri zikigharimu Bilioni 230 kwa Madarasa 11904.

Mhe,Mhandisi Robert Gabriel ameongeza  kuwa serikali pamoja na nguvu za Wananchi  madarasa 52 yatajengwa na kuondoa adha ya msongamano kwa watoto kukaa chini  na  wanapokaa chini hawezi kuandika vizuri.

Katika hafla hiyo Mkuu wa Mkoa Mhandisi Robert Gabriel amekemea vikali kwa yeyote ambaye atathubutu kutumia fedha ya umma hata mfumbia macho na kuchukuliwa hatua kali za kinidhamu pamoja na kupelewa mahakamani,sambamba hilo amezitaka Halmashauri kuongeza bidii katika ukusanyaji wa mapato.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Veronika Kessy amesema kuwa changamoto ya upungufu vyumba vya wa madarasa bado ni kubwa katika Shule za Msingi Wilaya ya Misungwi hivyo kwa Ujenzi wa vyumba vya madarasa utaondoa adha ya Wanafunzi kukaa kwa wingi katika madarasa.

Bi,Veronika Kessy amefafanua katika Kauli ya Mbiu Uzalendo Kwanza Kazi Iendelee imeleta mafanikio makubwa ambayo inawataka Wananchi kujitolea katika hali na mali  kuleta maendeleo na amewashukuru Wananchi na Wadau mbalimbali kwa kujitokeza kwa wingi katika Uzinduzi wa Ujenzi wa Vyumba vya madarasa 24 katika Shule ya Msingi Mbela.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Misungwi Mhe,Alexender Mnyeti amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe,Gabriel kwa mwitikio wake wa kuja Misungwi kuungana wa Wananchi katika uzinduzi na uchimbaji wa Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa katika Shule ya Msingi Mbela;na Madarasa hayo yatakapokamilika yatasaidia kuondoa changamoto ya Wanafunzi kurundikana kwa wingi katika madarasa.

“Nashukuru sana kwa niaba ya Wananchi kwa jinsi ulivyokuwa mbunifu na mchapa kazi na kuliona jambo hili na kulifanyia kazi   kuja kuzindua hivi vyumba vya madarasa 24 katika Shule Msingi Mbela.”

Philipo Manumbu ,Mwenyekiti wa Kitongoji wa Kitongoji cha Misri amesema kuwa katika kijiji cha Mbela kuna uhaba wa Shule za Msingi katika vitongoji sita kuna shule moja tu na hivyo kupelekea mrundikano mkubwa wa wanafunzi katika Shule ya Mbela,hivyo ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kushirikiana na Wananchi kwa kuanzisha ujenzi wa vyumba madarasa na kwamba baada ya Uzinduzi huo mchakato ujenzi utakuwa endelevu.

Mkazi wa Kitongoji cha Mbela B Bi,Leticia amefafanua kuwa ana furaha kubwa kwa kampeni hiyo ya Ujenzi wa Vyumba vya madarasa huku akibainisha kuwa awali palikuwa na changamoto ya madarasa hali iliyosababisha wanafunzi kuwa na zamu kwa wiki wakienda asubuhi na inayofuata wakiingia mchana.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.