• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Shirika la Amani Girls Home lajipanga kuboresha masuala ya Lishe Wilayani Misungwi mwaka 2020

Imewekwa : January 12th, 2020

Shirika la  Amani Girls Home la Mwanza latarajia kuanza utekelezaji wa mradi wa AMKA katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa lengo la kuboresha lishe kwa Watoto na akina mama wajawazito mwaka huu 2020.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa Shirika la Amani Girls Home, Revocutus Sono wakati wa kikao cha kutambulisha mradi huo kilichofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Graceland kilichowahusisha Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi pamoja na Wataalam wa Shirika hilo.

Bw, Sono ameeleza kuwa mradi huo utatekelezwa  mwanzoni kwa majaribio katika  Kata nane (8) za Halmashauri hiyo kwa gharama ya shilingi millioni 65 kwa lengo la kuboresha lishe kwa Watoto chini ya umri wa miaka mitano pamoja na akina mama walio kwenye umri wa uzazi, na lengo la mradi huu ni kutekelezwa katika Vijiji vyote 114 vya Halmashauri ya Wilaya ya  Misungwi.

Amefafanua zaidi kwamba mradi huo utatekelezwa kwa ushirikiano na Wadau wengine wakiwemo Shirika la PANITA ambalo ni Jukwaa la Lishe Tanzania kwa pamoja katika kuhamasisha Wananchi vijijini kuhusu umuhimu wa masuala ya Lishe bora kwa Watoto wenye umri mdogo sambamba na akina mama wenye umri wa uzazi ili kuweza kuboresha Afya zao.

Mwenyekiti wa kikao hicho Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi, Bw, Peter  Sabatto  akifunga kikao hicho amewataka Wadau wa maendeleo kushirikiana kwa pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi katika kutekeleza masuala ya Lishe kwa Wananchi na kuwahakikishia  amani na usalama wakati wote wa utekelezaji wa mradi huo, na kwamba Serikali inatambua juhudi za Wadau na Wafadhili mbalimbali wanaoendelea kusaidia maendeleo katika sekta zote kwa lengo la kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 – 2020.

 Peter Sabato Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi akisisitiza jambo kuhusu umuhimu wa Lishe kwa Wananchi wa Wilaya ya Misungwi, kwenye kikao cha Wadau katika Ukumbi wa Hoteli ya Graceland

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Bw, Kisena Mabuba amewataka Wataalam na Maafisa Ugani wa Idara ya Kilimo na Mifugo kupitia mpango wa Kitaifa wa Lishe na kuweza kutoa elimu kwa Maafisa waliopo katika ngazi za chini ili kuwawezesha kuhamasisha  na kuhimiza Wananchi katika masuala ya lishe pamoja na kusisitiza kilimo cha mazao muhimu ya chakula na ufugaji wa mifugo ikiwemo kuku wa mayai.

Bw, Kisena Mabuba amesema kwamba ni muhimu sana Wananchi wapewe elimu na kujengewa uelewa wa masuala ya lishe na kuweza kuendeleza kwa baadae hii ni kutokana na Sera na mwelekeo wa Serikali ya awamu ya tano ya kujenga uchumi wa kujitegemea na kupunguza ufadhili unaotolewa kwa masharti mbalimbali yasiyokuwa na tija na taifa.

Baadhi ya Washiriki wa kikao cha Viongozi kwa ajili ya kutambulisha mradi wa AMKA wakisikiliza mada kwa lengo la utekelezaji mradi wa Lishe katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.