• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Serikali ya Awamu ya Sita Yakomboa Sekta ya Elimu Misungwi

Imewekwa : March 19th, 2024

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa miaka mitatu ya utawala wake kwa mwaka wa fedha 2022/2023 alielekeza fedha kwa ajili ya  utekelezaji wa Miradi ya sekta ya elimu kupitia mradi wa Boost wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1,512,500,000/= ambazo zimetumika katika mradi  huo Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika ziara za Viongozi za ukaguzi wa miradi hiyo Wananchi wa Vijiji vya Mwagiligili, Busegeja na Mbela  wamefurahishwa na kuridhishwa na utekelezaji wa Miradi ya Boost ambapo miradi hiyo ililetwa kwa lengo la kutoa elimu bora kwa Wanafunzi kupitia ujenzi wa Madarasa yaliyojengwa, ujenzi wa vyoo pamoja na madawati uliotekelezwa kwa Shule za Msingi tisa Wilayani humo na wamempongeza na kumshukuru Rais wa Tanzania Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutoa fedha nyingi katika miradi ya elimu kwa muda mfupi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw. Joseph Mafuru amesema kwamba kupitia Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi  imefanikiwa kupata fedha shilingi Bilioni 1.5 kujenga shule za msingi mpya 2 na kukarabati shule zingine 7 ambapo Viongozi na Watendaji wamehakikisha fedha hizo zimetekeleza shughuli za ujenzi kwa wakati na kwa kasi ambayo inaridhisha ili kurahisisha shughuli pamoja na kuongeza kiwango cha elimu Wilayani na taifa kwa ujumla na kupunguza adha na kero kwa watoto kutembea umbali mrefu na mrundikano madarasani.  

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi Mhe, Abdi Makange akiwa na Kamati ya Usalama ya Wilaya katika  Shule ya msingi  Mwagiligili pamoja na Shule ya msingi mpya ya Shilabela Wilayani Misungwi amesema Watumishi wamejitahidi kusimamia ujenzi kwa uaminifu mkubwa na kuhakikisha miradi hiyo ya Boost Wilayani Misungwi  inakamilika na inazidi kwenda vyema kwa kujengwa kwa kiwango cha hali ya juu na hatimaye kukidhi na kujibu changamoto za watoto kutokwenda shule kwa uhaba wa majengo ya madarasa pamoja na madawati.

Mhe, Makange amewasihi na kuwataka Wananchi na Wakazi wa Kijiji cha Mwagiligili na Kata ya Busongo pamoja na Wakazi wa Shule ya msingi Shilabela kuyatunza  na kuyalinda madarasa ,madawati pamoja na vyoo ili kuwanufaisha wao na kizazi kijacho na kuwakumbusha Wazazi kuwahimiza na kuwapeleka watoto shule ili wapate elimu na maadili mema.

Naye Afisa Vifaa na Takwimu wa Shule za Msingi wa Halmashauri ya Wilaya  ya Misungwi na Mratibu wa Mradi wa Boost Bw. Godfrey Majura akitoa takwimu za fedha za miradi ya Boost amesema fedha zilizotolewa na Serikali kuu kwa Bajeti ya fedha ya mwaka 2022/2023 kwa ajili ya kutekeleza mradi ni shilingi Bilioni 1,512,500,000/= ambazo zililetwa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya sekta ya Elimu msingi  ambapo zimeweza kunufaisha na kujenga na kukarabati miundombinu na majengo  katika shule za msingi 9 ambazo ni Shilabela, Mwabebea, Mwagiligili, Chata, Igwata, Busegeja, Iteja,Kagera, na Nyabuhele .

Bw Godfrey Majura ameongeza kwamba Serikali ilitoa fedha shilingi Milioni 540.3 kujenga shule ya msingi mpya ya Shilabela pamoja na shule ya msingi Ntende kwa sasa shule ya msingi mpya ya Mwabebea ambayo imejengwa kwa shilingi Milioni 540.3 na shule za msingi 7 zilizobaki  zimefanyiwa ukarabati wa miundombinu ya majengo pamoja na nyongeza ya kujenga majengo ya Madarasa na vyoo hivyo zoezi la ujenzi limefanyika vizuri na kwa ubora unaoridhisha kupitia kamati za ujenzi, manunuzi na mapokezi.

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Misungwi akiwamo Bw, Samson Selema  amesema kuwa hapo awali watoto walikua wakipata adha kubwa wakiwa darasani kwani iliwabidi kujazana hatimaye hali hiyo kwa sasa imetatuliwa ambapo amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Misungwi kwa wakati huo Mhe. Paulo Chacha pamoja na Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo katika sekta zote ikiwemo elimu, Afya na Maji  na kuwaomba waendelee na moyo huo ili kuwaletea maendeleo ya dhati Wananchi.

Halmashauri ya Misungwi imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo sekta ya Afya, Barabara, Maji pamoja na sekta ya Elimu ambapo kwa upande wa elimu kupitia mradi wa Boost imeweza kutekeleza shule hizo pamoja na kuendelea na utekelezaji wa miradi mingine ya elimu Sekondari.

Mwonekano wa baadhi ya vyumba vya madarasa katika Shule mpya ya msingi Shilabela iliyopo Kata ya Misungwi ambayo imegharimu zaidi ya kiasi fedha shilingi Milioni 500 fedha kutoka Serikali kuu kupitia mradi  wa BOOST. 

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.