• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Serikali Wilayani Misungwi yapiga marufuku Walimu kuwatumikisha Wanafunzi mashambani na majumbani.

Imewekwa : February 24th, 2020

Serikali Wilayani Misungwi, Mkoani Mwanza imepiga marufuku vitendo vya Walimu kuwatumikisha Wanafunzi kwenye shughuli za mashamba yao binafsi na majumbani hivyo kusababisha kuzorota kwa elimu.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda wakati wa ziara ya kukagua Miradi na shughuli za maendeleo iliyofanyika katika Kata ya Gulumungu Tarafa ya Inonelwa Wilayani humo kwa lengo la kutembelea na kuona utekelezaji wa miradi katika Zahanati ya Nyamayinza, Shule  ya Sekondari  J. Magufuli na  Shule ya Msingi Mwakiteleja, Miundombinu ya barabara na Maji pamoja na miradi ya sekta zingine.

Akizungumza na Viongozi, Wananchi na Walimu katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya maeneo ya Shule ya Sekondari J. Magufuli  Kijiji cha Nyamayinza  Kata ya Gulumungu, baada ya kusikiliza kero na malalamiko ya Wananchi hao Mkuu wa Wilaya huyo,  amesema kuwa kumekuwepo na baadhi ya Walimu ambao wanaendelea kuwatumikisha pamoja na kuchapa viboko Wanafunzi bila utaratibu maalum na kusababisha migongano baina ya Walimu  hao na Wazazi pamoja na kuzorotesha utoaji wa elimu bora hatimaye kusababisha kushuka kwa kiwango cha taaluma na ufaulu.

“ Ninyi Walimu nataka niwaambieni mzingatie maadili ya taaluma yenu, kazi kubwa kwenu nikufundisha, hivyo ni marufuku kuanzia leo kwa Wanafunzi hawa kulima katika mashamba yenu binafsi pamoja  na kuwapa kazi majumbani mwenu, pia nawataka mtekeleze na kusimamia haya  ambapo mashamba ya shule yabaki kutumiwa na shule yenyewe kwa ajili ya kulima mazao ya Chakula na siyo Walimu kujinufaisha  nayo tena,”alisititiza na kuagiza Mkuu wa Wilaya Juma Sweda.

Juma Sweda, amewataka Viongozi wa Vijiji na Kata zote Wilayani humo kusimamia kikamilifu maendeleo ya  utoaji wa elimu na taaluma na kuhakikisha uadilifu na nidhamu kwa Walimu na Wanafunzi unadumishwa pamoja na kuendelea na utoaji wa chakula  na masomo ya ziada kwa Wanafunzi ili kuboresha na kuongeza kiwango cha taaluma na ufaulu wa Wanafunzi na kutimiza mpango mkakati wa Wilaya wa kuondoa “Division Four na Ziro” kwa mwaka 2020.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda (kulia) akisalimiana  na kumuuliza maswali kuhusu masomo Mwanafunzi wa Kidato cha Pili katika Shule ya Sekondari J.Magufuli wakati wa ukaguzi wa  madarasa na kuona maendeleo ya Wanafunzi wa shule hiyo uliofanyika katika ziara aliyoifanya hivi karibuni.


Mmoja wa Wakazi wa Kijiji cha Nyamayinza akitoa kero na malalamiko yake kwa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, kuhusu adhabu wanayopatiwa Wazazi wanaozesha na kuwapa mimba watoto wa shule.

Mkuu wa Wilaya huyo pia  amewaagiza Viongozi hao pia kuwasaka  watoto watatu (3) ambao hawajaripoti kidato cha kwanza mpaka sasa katika Sekondari ya J. Magufuli , kuhakikisha wanapatikana  na wanaanza masomo haraka, vile vile amekemea tabia ya baadhi ya Wazazi wanaowaozesha na kuwapa mimba watoto wa shule na kukatisha ndoto zao na kuwaonya waache tabia hiyo chafu vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao hatimaye kufungwa maisha.

Ameongeza kwamba ni vyema Viongozi wa nagzi za Vijiji na Vitongoji kutambua nafasi na wajibu wao katika kutekeleza majukumu ya Serikali  na kuleta maendeleo kwa Wananchi pamoja na kuhakikisha wanatunza na kulinda amani na usalama katika maeneo yao hususan katika kipindi hiki cha maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, hivyo wanapaswa kuimarisha ulinzi wa Jeshi la  jadi la Sungusungu.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Kata ya Gulumungu, Valentine Lukandiza  amesema kwamba amepokea maagizo na maelekezo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, na watahakikisha wanatekeleza na kusimamia masuala ya  kuboresha taaluma  katika shule za Msingi na Sekondari  kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria zilizopo ili kuweza kutatua kero na kuwaletea maendeleo Wananchi.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.