• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Serikali kujenga Bweni Sekondari ya Misungwi, kupunguza tatizo la mimba na kutembea umbali mrefu

Imewekwa : March 13th, 2020

Serikali  kujenga bweni la shilingi Milioni 75 kwa ajili ya  kulala  Wanafunzi wa kike  katika Shule ya Sekondari Misungwi, Wilayani Misungwi, Mkoani Mwanza ikiwa ni jitihada za kupunguza  na kuondoa tatizo la kutembea umbali mrefu.

Akizungumza na Viongozi na Wanafunzi katika Shule ya Sekondari Misungwi, wakati wa ziara ya kikazi Wilayani Misungwi,  Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI, anaeyeshughulikia Elimu, Gerald Mweli ametoa ahadi ya Serikali kupitia Wizara ya ofisi ya Rais - TAMISEMI kwamba watajenga bweni moja la Wanafunzi kwa gharama ya shilingi Milioni 75 na kueleza kuwa amekagua  ujenzi  unaoendelea na kuridhishwa na kazi zinazofanyika na tayari Wizara imeshapokea maombi ya fedha za ujenzi wa mabweni.

“ Sisi kama ofisi ya Rais –TAMISEMI kupitia kwa Mhe, Waziri Jaffo alipokea maombi yenu ya ujenzi wa bweni kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, na sisi baada ya kuona juhudi hizi tumeona tutafute fedha,  na tutajenga bweni moja ambapo hali na uwezo ukiruhusu tutaongeza bweni lingine,”alifafanua kwa msisitizo zaidi Naibu Katibu Mkuu,  Mweli.

Naibu Katibu Mkuu  huyo, amewapongeza Viongozi na Watendaji wote wa  Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kusimamia  vizuri maendeleo ya sekta ya elimu pamoja na jitihada za kupunguza mdondoko wa Wanafunzi katika elimu, sambamba na suala la kuwachukulia hatua za kinidhamu baadhi ya Walimu wasiozingatia na kufuata maadili ya ualimu na kuongeza kiwango cha ufaulu katika matokeo ya darasa la saba,  kidato cha Nne na sita mwaka  jana 2019.

Bw, Mweli amempongeza Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Misungwi, Ananias Mbandwa kwa kazi nzuri aliyoifanya na kuweza kuokoa fedha zaidi ya Milioni 30 zilizotolewa na Serikali za ununuzi wa Chakula na kununua kwa bei ya sokoni, ambazo ameamua kuanzisha ujenzi wa bweni la Wasichana ambalo linaendelea kujengwa, amesema kwamba,  hii ndo aina ya viongozi tunaowataka, viongozi wanaoishi ndani ya changamoto na wanashiriki katika kutatua changamoto na wanasherekea mafanikio kwa pamoja.

Wakati huo huo, baadhi ya Wanafunzi wa  Shule ya Sekondari Misungwi,  akiwemo kaka Mkuu wa Shule hiyo, Timoth John  anayesoma kidato cha Nne pamoja na Dada Mkuu Yustina Antipas ambaye ni  Mwanafunzi wa kidato cha Tano kwa nyakati tofauti wametoa salamu za pongezi na shukrani kwa Mhe, Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, John Pombe Joseph Magufuli kwa juhudi kubwa aliyowafanyia Watanzania kwa kutoa elimu bila malipo, ambapo utaratibu huo umeongeza idadi ya Wanafunzi na kupunguza Watoto wa mitaani na wanaoishi katika mazingira magumu hatimaye kiwango cha ufaulu kimeongezeka.

Wanafunzi hao wamebainisha mikakati yao pamoja na Walimu kwa mwaka huu 2020 ambayo ni kuhakikisha wanaondoa ufaulu wa daraja sifuri katika matokeo ya kidato cha Nne, sambamba na kufuta ufaulu wa daraja la nne, na daraja la tatu katika matokeo ya kidato cha sita, na wameweza kuahidi kuweka historia na mapinduzi makubwa katika ufaulu wa mitihani ya mwaka 2020.

Katika ziara  hiyo Naibu Katibu Mkuu -TAMISEMI Wilayani hapa, ameweza kukagua na kuona shughuli za miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa Jengo la bweni la Wanafunzi wa kike katika Shule ya Sekondari ya Misungwi, kutembelea na kuzungumza na Wanafunzi wa shule ya msingi maalum ya Mitindo pamoja na kuzindua zoezi la  kitaifa la ugawaji wa Vitabu vya kiada vya kufundishia Wanafunzi wa darasa la sita katika masomo yote, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi imepata vitabu zaidi ya elfu 26.

Jengo la bweni la Wasichana linaloendelea kujengwa katika Shule ya Sekondari Misungwi ambalo litagharimu shilingi Milioni 110 hadi kukamilika., ujenzi huu ulianza kwa fedha shilingi milioni 30 ambazo ziliokolewa na Mkuu wa Shule hiyo Mwl, Ananias Mbandwa na baadaye Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia kutoa fedha za kukamilisha ujenzi huo mwaka 2020.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba (katikati) akitoa taarifa ya maendeleo ya shughuli za Sekta ya Elimu kwa mawaka 2019/2020 kwa Naibu Katibu Mkuu - TAMISEMI, Gerald Mweli wakati wa ziara ya kikazi ofisini kwa Mkurugenzi Mtendaji Wilayani Misungwi mapema jana, (kulia) ni Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Misungwi, Diana Kuboja akifuatilia kwa makini.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.