• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Sekondari ya J Magufuli na Mamaye, Wilayani Misungwi zawezeshwa Vifaa vya Shule na Kampuni ya NEBRIX LTD.

Imewekwa : August 22nd, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza yapokea msaada wa Vifaa vya kufundishia na kujifunzia kutoka kwa Kampuni ya Nebrix Ltd yenye Makao Makuu Jijini Mwanza kwa ajili ya matumizi ya Wanafunzi wa Shule za Sekondari za Serikali Wilayani humu.

 Akizungumza katika makabidhiano ya msaada wa vifaa hivyo ofisini kwa  Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Afisa Masoko wa Kampuni ya Nebrix Ltd, Mwanza, Ayubu Robert  Ng”hwelo  amesema kwamba msaada huo ni pamoja na Vitabu  50 mchanganyiko vya masomo mbalimbali, Global 1, Dustbin 5 za kuhifadhia taka laini, Heart Model 1, Charts 20, First Aid Kit 1, na Skeleton Model 1. 

Afisa Masoko, Ayubu Robert, wa Kampuni ya Nebrix Ltd ya Mwanza ameeleza kwamba Vifaa hivyo vina thamani ya shilingi 4,300,000/= ambapo vyote vitatumika kufundishia na kujifunzia kwa Walimu na Wanafunzi wa Shule za Sekondari katika Halmashauri ya Misungwi zenye upungufu na uhaba wa Vifaa hivyo  na vitasaidia kuboresha utendaji kazi na kuinua kiwango cha taaluma kwa Wanafunzi Wilayani humo.

Bw, Philipo Andrea(kulia) Afisa Masoko wa Kampuni ya Nebrix Ltd akimkabidhi  na kutoa maelezo ya Vifaa vya kujifunzia na kufundishia Wanafunzi wa Sekondari, Bi, Dianah Kuboja  Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Misungwi.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya  Misungwi, Kisena Mabuba  amesema kuwa katika Halmashauri ya Misungwi kuna Shule za Sekondari 30 ambapo Shule za Serikali ni 25 na Shule za Sekondari za binafsi ni 5, hivyo mahitaji ya Vifaa vya kujifunzia na kufundishia ni muhimu na vinahitajika sana, hivyo amewashukuru na kuwapongeza Kampuni ya Nebrix Ltd ya Mwanza, kwa maamuzi ya kutoa msaada huo katika Halmashauri ya Misungwi,.

Bw, Kisena Mabuba aliongeza kuwa Kampuni hiyo imefanya  vizuri kwa kukumbuka kuwasaidia Wateja wake  kwa kutoa Vifaa wezeshi kutokana na faida ya mapato yanayotokana na shughuli yao ya  usambazaji wa Vifaa vya Maabara na Kemikali katika Shule za Sekondari, na kwamba Vifaa hivi vitawasaidia sana Wanafunzi kujifunzia na hivyo kuinua kiwango cha taaluma katika Shule za Sekondari hususan katika Shule zenye upungufu wa Vifaa husika.  

Kwa upande wake, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Bi. Dianah Kuboja  amesema  kwamba Vifaa hivyo vyote vitapelekwa katika Shule za Sekondari mpya  ambazo ni  J Magufuli  Sekondari pamoja na Mamaye Sekondari, Shule hizo zina uhaba na upungufu mkubwa wa Vifaa vya kujifunzia na kufundishia  kwa Wanafunzi na Walimu , hivyo vitawasaidia sana na hatimaye kuboresha taaluma katika Shule hizo.

Bi, Kuboja alieleza kwamba  Vifaa hivyo  vitaongeza pia kiwango cha ufaulu kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Wilayani Misungwi  ambapo kwa upande wa ufaulu wa Mitihani ya Kidato cha Nne kwa mwaka 2018 , Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi  ilikuwa katika nafasi ya 4 Kimkoa kati ya Halmashauri 8 za Mkoa wa Mwanza .

Kampuni ya Nebrix  Ltd yenye Makao Makuu Jijini  Mwanza imeanzishwa rasmi mwaka 2007 na  inajuhusisha katika shughuli za usambazaji wa Vifaa vya Maabara, Kemikali pamoja na Vifaa vya kujifunzia na kufundishia na ina matawi mbalimbali katika Mikoa 10 kwenye  maeneo  ya Shinyanga, Dodoma, Iringa, Mbeya, Njombe, Songea, Kasulu, Ifakara, Mpanda, Sumbawanga , Dar Es Salaam na Mwanza.

Bi, Dianah Kuboja Afisa Elimu Sekondar Wilaya ya Misungwi akifurahia Msaada wa Vifaa baada ya kukabidhiwa na Kampuni ya Nebrix kupitia kwa Bw, Ayub Robert ambaye ni  Afisa Masoko

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.