• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

RC Mwanza apongeza usimamizi miradi Misungwi, asisitiza utunzaji wa miradi

Imewekwa : June 20th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe, Mhandisi Robert Gabriel  apongeza usimamizi na  utekelezaji wa Miradi ya maendeleo iliyotekelezwa  katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza.

Mhandisi  Robert Gabriel amesema hayo wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika Halmashauri hiyo kwa ajili ya kutembelea na kuona shughuli za utekelezaji wa miradi ya maendeleo zilizofanyika kwa mwaka 2020/2021 katika  Halmashauri hiyo yenye jumla ya Kata 27.

Mhandisi Robert Gabriel amesema kwamba usimamizi wa matumizi ya fedha za umma  unaridhisha na katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo inatekekelezwa kikamilifu  hususani katika miradi inayotolewa fedha na Serikali na nguvu za Wananchi akizungumza katika mradi wa ujenzi wa maabara 3 katika Shule ya Sekondari Sanjo ambapo Jengo la maabara lenye vyumba vitatu limekamilika kwa gharama ya shilingi .117,000,000/= kati ya fedha hizo shilingi 60,000,000/= ni kutoka Serikali kuu na shilingi 57,000.000/= ni nguvu na michango ya Wananchi wa Kata ya Usagara.

Ameweza kutembelea pia katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi ambapo tayari ujenzi wa Jengo la Wodi ya Wazazi umekamilika na Jengo linatumika kwa kulaza Wagonjwa ambao ni akina Mama wajawazito, Jengo hilo limejengwa kwa msaada wa Wafadhili wa Impact wa Nchini Canada, pamoja na kuona mradi wa utafiti wa Malaria wa PAMVERRC ambao unafanya utafiti wa njia za kuzuia malaria katika Kata 17 za Wilaya ya Misungwi.

Mhandisi Gabriel amewataka Watendaji kuongeza ushirikiano kwa kufanya kazi kama timu na kwa kufanya hivyo kutaongeza na kuleta maendeleo makubwa zaidi na miradi itataekelezwa kwa umakini na ubora zaidi, amewataka  kufanya kazi kwa moyo na kujituma kwa weledi hatimaye kufikia malengo na dira iliyokusudiwa.

Awali akizungumza na Wananchi katika maeneo tofauti ya Vijiji vya Nyanghomango na Usagara amewatahadharisha na kuwataka Wananchi na Viongozi  Wilayani humo na Mkaoni  Mwanza kwa ujumla  kuchukua tahadhari kubwa na kukabiliana na mlipuko wa wimbi la tatu la Ugonjwa wa Covid 19 usababishwao na Virusi vya Corona ambao umeanza kuzikumbuka  nchi za Afrika na kuwaomba kuendelea kuzingatia masharti na maelekezo ya Watalaam wa Afya ikiwa ni pamoja na kunawa Mikono, Kuvaa Barakoa, kuepuka Mikusanyiko isiyokuwa ya lazima, kukaa umbali wa zaidi ya mita moja na nusu baina ya mtu na kufanya mazoezi

Mhandisi  Robert Gabriel ameongeza kwamba endapo Wananchi wataona dalili zitokanazo na Ugonjwa huu wa Corona ikiwemo  kuumwa kichwa, kikohozi, Mafua makali, Mwili kuchoka, kutonusa harufu, na kubanwa mbavu wawahi mapema katika Vituo vya kutolea huduma za Afya kwa matibabu na kuendelea kuwakinga wengine.

Katika ziara hiyo ya kutembelea shughuli za miradi Mhe, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel ameambatana na Wajumbe wa Kamati ay Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mwanza,  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Misungwi, Watendaji na Wataaalam.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Nyanghomango Wilayani Misungwi wakati wa ziara ya kikazi ya shughuli za maendeleo hivi karibuni


Jengo la Vyumba viwili na ofisi moja ya Walimu lilojengwa katika Shule ya Sekondari ya Nyangh"omango ambalo limekamilika tayari na litazinduliwa na Kiongozi wa Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.