• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

RC Mwanza apongeza na kuridhishwa na utendaji wa Madiwani na Watendaji Misungwi

Imewekwa : June 20th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe, Mhandisi Robert Gabriel aridhishwa na kupongeza  utendaji wa  Baraza la Madiwani na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza

Mkuu wa Mkoa Robert Gabriel alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati wa Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo liloketi kwa ajili ya kupitia na kujadili taarifa ya hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020 uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri hiyo.

Mhandisi Robert Gabriel amesema kwamba ameridhishwa sana na utendaji wa Madiwani na Watendaji wa Halmashauri ya Misumgwi ambapo kutokana na taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  kwa mwaka 2019/2020 imeonyesha kuwa hoja ni chache na baadhi yake ni za kawaida na dhahiri kwamba usimamizi wa matumizi ya fedha za umma  unaridhisha na katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo inatekekelezwa kikamilifu pamoja na suala la ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mhandisi Gabriel amewataka Watendaji kuongeza ushirikiano kwa kufanya kazi kama timu na kwa kufanya hivyo kutasababisha na kufanya mambo mambo mengi makubwa na ya ajabu  na  kuongeza mafanikio makubwa zaidi katika maendeleo ya miradi  kwa Wananchi, na kuwataka Watendaji kuendelea kujibu Hoja vizuri na kuendelea kufanya matumizi ya fedha kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria za fedha ili kuepuka hoja zisizokuwa za msingi.

Awali akiwasilisha taarifa ya hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2019/2020 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba amesema kwamba  katika ukaguzi huo Halmashauri hiyo  imepata Hati ya Kuridhisha (Hati safi) ambapo hoja zilizohojiwa kwa mwaka 2019/2020 zinaendelea kutekelezwa ambazo ni pamoja na Hoja 8 zilizotekelezwa, Hoja 19 zinazoeendelea kutekelezwa na kufanya kuwa na Hoja 27 kwa mwaka huo.

Kisena Mabuba ameeleza kwamba kulikuwapo pia Hoja za nyuma ambazo ni 18 ambapo Hoja 16 zinaendelea kutekelezwa  na Hoja 2 ambazo hazijatekelezwa na kuwa na idadi ya jumla ya Hoja 45 zilizohojiwa,  na Menejimenti inaendelea kufuatilia hoja hizo na kuzitekeleza na baaadae kuhakikiwa na Wakaguzi.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Mhe, Kashinje Machibya ameeleza kuwa kwa ujumla Baraza la Madiwani limeendelea kusimamia kikamilifu shughuli za maendeleo ikiwemo miradi, Ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri, utendaji kazi wa Watendaji ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji na kuchukua hatua za kinidhamu mara inapobainika pamefanyika kinyume na sharia, kanuni na taratibu.

Mhe, Machibya amesema kwamba kutokana na usimamizi mzuri wa Baraza la Madiwani ndio umeleta mafanikio ambapo katika ukaguzi huo zimeonekana  hoja chache ambazo ni nyepesi za kiutendaji zaidi na kuahidi kuendelea kusimamia kikamilifu utendaji ili katika ukaguzi ujao kuwa na hoja chache na zilizo na majibu yanayotosheleza.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wialaya ya Misungwi, Mhe, Kashinje Machibya akizungumza na kutoa Salaam katika Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani la Halmashauri la kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu  wa Hesabu za Serikali akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ,Mhandisi Robert Gabriel (kulia) pamoja na Viongozi wengine wa Wilaya ya Misungwi.

Baadhi ya Waheshimiwa Madiwani wa Baraza la Halmashauri ya WIlaya ya Misungwi wakifuatilia mjadala wa Mkutao kwa makini wakati Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel akitoa maelekezo kwa Madini na Watendaji wa Halmashauri hiyo.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.