• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

RC Mwanza akagua Ujenzi Madarasa na kupokea Madawati 145 ya Benki ya CRDB Wilayani Misungwi

Imewekwa : December 7th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhadisi Robert Gabriel  afanya ukaguzi na kuridhishwa na utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya vyumba vya madarasa 146  katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Akikagua miradi hiyo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Sekondari Mawematu, Shule ya Sekondari Misungwi pamoja na shule ya Sekondari Sanjo Mhandisi Robert Gabriel ametoa maelekezo kwa Viongozi na Watendaji kuendelea kusimamia kikamilifu ujenzi huo kwa kuzingatia vipimo,mchoro na  ramani ya majengo, kuzingatia uwiano wa mahesabu  katika vipimo vya ujenzi wa majengo ya Serikali kulingana na taratibu na kanuni za kitaalam ili kuweza kukamilisha majengo ya madarasa kwa usahihi  ubora pamoja na thamani ya fedha kuweza kuonekana.

Mhandisi  Robert Gabriel amesema hayo wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya hivi karibuni kwa ajili ya kutembelea na kuona shughuli za utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa fedha shilingi Bilioni 2.9  iliyotolewa na Serikali  katika  Halmashauri hiyo kutekeleza  jumla ya madarasa 146 yanayojengwa katika shule 32 za Halmashauri hiyo.

Mhandisi Robert Gabriel amesisitiza Watendaji  kusimamia vizuri ubora na kiwango cha ujenzi wa majengo ya madarasa  na kuzingatia matumizi sahihi  ya fedha za umma  na kuhakikisha  miradi ya madarasa yote inatekekelezwa kikamilifu , akizungumza katika mradi wa ujenzi wa madarasa 6 katika Shule ya Sekondari Mawematatu ambapo ujenzi umefikia hatua ya boma na unaendelea katika hatua ya uwekaji wa jamvi na kuezeka ameshauri Halmashauri kuwatumia katika kujenga  vijana wa Chuo cha Maendeleo ya jamii ufundi cha Misungwi na kuwapatia maeneo ya kujenga ili kuweza kusaidia na kuwapa uwezo na kuaminiwa na jamii na hatimaye kuunda vikundi vya ujenzi ambavyo vitafanya shughuli za Ujenzi wa majjengo ya Serikali na kuweza kukamilisha ujenzi kwa wakati.

Mhandisi Robert  Gabriel amewataka Watendaji kuongeza ushirikiano kwa kufanya kazi kama timu na kwa kufanya hivyo kutaongeza na kuleta maendeleo makubwa zaidi na miradi  hiyo itataekelezwa kwa umakini na ubora zaidi, amewataka  kufanya kazi kwa moyo na kujituma kwa weledi hatimaye kufikia malengo na dira iliyokusudiwa.

Katika ziara hiyo Mhandisi Robert Gabriel ameushukuru Uongozi wa Benki ya CRDB Taifa kwa kuonyesha upendo na kuweza kurudisha asante kwa Wananchi kwa kutoa madawati kwa kusaidia Wanafunzi kujisomea vizuri na kuwahakikishia kwamba  Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kuleta mendeleo kwa Wananchi pamoja na juhudi za taasisi za fedha katika kuinua uchumi wa taifa.

Kwa upande wake Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa Lusingi Sitta amesema kwamba Benki imeweza kukabidhikwa Mkuu wa MKoa wa mwanza madawati 145 yenye tahmani ya Milioni 10 ambapo wameweza kuunga mkono juhudi za Serikali katika sekta ya Elimu na wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo katika sekta mbalimbali.

Katika ziara hiyo ya ukaguzi  wa miradi Mhe, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel ameambatana na Wajumbe wa  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Misungwi, pamoja na Watendaji na Wataaalam wa Halmashauri ya Misungwi.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel Katikati akizungumza na kuishukuru benki ya CRDB kwa kutoa madawati 145 kwa Hallmashauri ya Wilaya ya Misungwi pamoja na meneja wa Benki ya CRDB Lusingi Sitta ( wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya  Misungwi, Bi. Leokadia Humera pamoja na Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi, Petro Sabatto amabye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Veronika Kessy katika Hafla hiyo

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DAS Misungwi awapongeza Watendaji Halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani katika kuongeza ufanisi na ukusanyaji wa Mapato.

    April 29, 2025
  • Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yafanya ziara ya yatembelea na kupata mafunzo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya nyang'hwale Mkoani Geita

    April 25, 2025
  • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango yaridhishwa na miradi ya maendeleo ya Halmashauri Wilaya ya Misungwi

    April 23, 2025
  • Kamati ya Lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yawataka Watendaji wa Kata na Vijiji kutoa Elimu ya Shughuli za Lishe kwa Wananchi.

    February 27, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.