• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

RC Mwanza aagiza kukamatwa Wadaiwa sugu fedha za Mapato ya ndani Misungwi

Imewekwa : June 27th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel aagiza kukamatwa wadaiwa sugu wa makusanyo ya Mapato ya ndani shilingi Milioni 48 na kuhakikisha wanarejesha fedha hizo ndani ya mwezi mmoja Wilayani Misungwi.

Mhe, Mkuu wa Mkoa Robert Gabriel ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo lililofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri kwa ajili ya kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022

Mhandisi Robert Gabriel amewatakaViongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kuhakikisha Watumishi hao wanaodaiwa fedha hizo wanarejesha mapema fedha za Serikali ambapo waangalie pia mikataba yao na kuona Wadhamini wao ili waweze kutoa fedha za makusanyo ya  mapato ya ndani wanayodaiwa ili ziweze kutumika kuleta maendeleo kwa Wananchi wa Misungwi.

Amesema kwamba  fedha za mapato ya ndani shilingi 48,316,205/=  zilizokusanywa kwa nyakati tofauti na Wakusanya mapato wa Halmashauri hiyo wakiwemo Watumishi na  wakusanyaji wengine wa mapato walioingia mikataba ya kukusanya mapato husika.

“ Lazima msome tabia za Makala wanaokusanya fedha za mapato na kujiridhisha na uhalali na  nyendo zao na kuhakikisha wanajiridhisha fedha za mapato kwa wakati”. Alisisitiza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza..

Ameeleza kuwa vyombo vya uchunguzi wawasake wote na warejeshe fedha zote za makusanyo ya mapato ya ndani  na kuwataka Watumishi wote wanaodaiwa fedha za mapato wakatwe kutoka katika mishahara yao pia wajiridhirishe katika kudhibiti fedha za mapato yasivuje na kuimarisha mifumo na kuweka  mikataba makini na kuagiza suala hilo lishughulikiwe kwa wakati ndani ya mwezi mmoja.

Kwa upande wake Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi limeridhiria agizo hilo la Mkuu wa Mkoa  la  kuwakamata wadaiwa sugu wa  makusanyo ya fedha za mapato pamoja Wadaiwa wa madeni ya mikopo ya Vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu ambazo ni fedha za Vikundi shilingi milioni 83.9 ambazo walikopeswa kwa muda lakini hawajweza kurejesha fedha hizo kwa wakati.

Baadhi ya Madiwani akiwemo Diwani wa Kata ya Sumbugu Jogoli Mayombo alieleza kwamba wadhamini wa kukusanya mapato wanaodaiwa wakamatwe kwa mujibu wa mkataba  pamoja madeni ya vikundi vya mikopo mbalimbali virejeshe ili  fedha hizo vipewe na Vikundi vingine.

Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi wakinyosha mikono ishara ya kuridhia maelekezo na maagizo ya Mhe, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika Mkutano wa Braza la Hoja za Mdhbiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali za mwaka 2020/2021 za Halmashauri ya Wilaya hiyo. Aliyeketi katikati ni Mhe, Joel Dogani Diwani wa Kata ya Mbarika .

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe, Robert Gabriel amesema kwamba fedha hizo hazikuwa zawadi hivyo walipe ili ziweze kukopeshwa kwa Vikundi vinavyohitaji Mkopo huo wa Serikali ambao hauna riba na kwamba Halmashauri ya Misungwi iweke mipango mikakati ya udhibiti wa matumizi ya fedha za miradi na kuhakikisha inatekeleza kikamilifu miradi na kuwapatia maendeleo Wananchi.

Awali akiwasilisha taarifa ya hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2020/2021 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Benson Mihayo  amesema kwamba  katika ukaguzi huo Halmashauri hiyo  imepata Hati ya kuridhisha (Hati safi) ambapo hoja zilizohojiwa kwa mwaka wa fedha 2020/2021 zinaendelea kutekelezwa.

Bw, Mihayo  ameeleza kwamba kulikuwa na Hoja za nyuma ambazo ni 35 ambapo Hoja 10 zimefungwa na Hoja 23 zinaendelea kutekelezwa  na Hoja 2 ambazo hazijatekelezwa  na Menejimenti inaendelea kufuatilia hoja hizo na kuzitekeleza na baaadae kuhakikiwa na Wakaguzi na watahakikisha zinafanyiwa kazi na kukamilisha kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo.

M

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Misungwi Mhe, Rahma Fidel akizungumza kwa msisitizo wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani mapema leo na kushoto ni Katibu wa Chama cha Mapinduzi Chollage A Chollage na kulia ni Mkuuw amKoa wa Mwanza Mhndisi Robert Gabriel ambaye amezungumza na Braza la Madiwani wa Halamshauri ya Misungwi.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Misungwi, Bw, Benso Mihayo (aliyesimama Kulia ) akieleza jambo wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri mapema leo 


Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.