• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

RC Malima awapa Kongole Wilaya ya Misungwi kwa ujenzi madarasa 44

Imewekwa : January 15th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe, Adam Malima  azindua vyumba 44 vya madarasa yenye thamani ya shilingi milioni 880 katika Halmashauri ya Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Amezindua vyumba hivyo 44 vya madarasa mwishoni mwa wiki  katika Shule ya Sekondari Idetemya ambayo imekamilisha ujenzi wa vyumba 6 vya madarasa kwa gharama ya  shilingi 120,000,000 ambapo  Halmashauri imeweza kujenga  vyumba vyote  44 vya madarasa katika shule 15 za Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Mhe, Adam Malima ametoa rai kwa  Viongozi wa Halmashauri hiyo kuweka juhudi za kuongeza eneo kwenye shule mpya ya Jitihada  iliyopo katika Kata ya Misungwi ili kusaidia shule hiyo kuwa na uwezo wa kupanuka kwa kuongeza miundombinu mingine ikiwemo ya Viwanja vya michezo pamoja na madarasa kutokana na shule hiyo kuwa katika maeneo ya mjini yenye ongezeko kubwa la idadi ya watu.

"Hamuwezi kuwa na shule mpya leo hii yenye hekari sita pekee, fanyeni jitihada kuongeza eneo ili kuiwezesha kumudu ongezeko la wanafunzi  kwa mipango ya sasa na baadae na msitegemee kuanzisha shule mpya mbali kwani zitakua na gharama ya usafiri kwa wazazi katika kuhakikisha watoto wao wanafika shuleni",Amesisitiza Mhe, Malima.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amewapongeza na kuwapa Kongole Viongozi wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi mzuri na kuhakikisha eneo la shule linapandwa Miti ya kutosha na kuomba Halmashauri zingine Mkoani humo kuiga mfano wa Halmashauri ya Misungwi na Magu ambazo zimekuwa mfano bora katika utunzaji na uhifadhi wa mazingira kitendo ambacho kitarejesha uoto wa asili na kuondoa hewa ya ukaa.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Ndugu Balandya Elikana amewataka wazazi na walezi wote Wilayani Misungwi kuhakikisha wanawapeleka watoto shule kuanza  kidato cha kwanza kutokana na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari ameshajenga madarasa na miundombinu mingine pamoja na kuweka madawati , viti na meza ili watoto waweze kusoma vizuri .

Awali katika uwasilishaji wa taarifa ya ujenzi vyumba 44 vya madarasa ilibainishwa kwamba ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa umefanyika sambamba na matengenezo ya Samani kwa wanafunzi ambapo Seti za viti na meza 1,760 zimetengenezwa ambazo zitanufaisha wanafunzi 1, 767 wa kidato cha kwanza kwa mwaka 2023.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Veronika Kessy ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za ujenzi wa madarasa  44 ambazo kwa Wilaya ya Misungwi zimesaidia kupunguza changamoto ya umbali wa baadhi ya Wanafunzi kutoka shule moja hadi nyingine, na kwamba atahakikisha wazazi na walezi wanapeleka watoto kuanza kidato cha kwanza mapema pamoja na kusimamia utunzaji wa miundombinu ya madarasa ili yaweze kuleta tija na manufaa yaliyokusudiwa na kudumu kwa muda mrefu.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, 


Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.