• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

RAS Mwanza aaigiza Wataalam wa Afya kupunguza Vifo vya Mama na Mtoto Mkoani Mwanza

Imewekwa : February 1st, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amewataka Wataalam wa Afya kuhakikisha  wanapunguza na kutokomeza Vifo vya Mama na mtoto  kwa kuboresha na kusimamia kikamilifu utoaji wa huduma za Afya vituoni Mkoani Mwanza.

Bw, Elikana amewataka  kuhakikisha Wataalam hao wa Afya wanalinda afya ya mama na mtoto  muda wote, ikiwa ni pamoja na uimarishaji wa mfumo wa kumfuatilia mama mjamzito mpaka hatua ya  maandalizi ya kujifungua.  uwepo wa vifaa vya kujifungulia  vituoni, kujitahidi kupunguza Vifo vya Mama na Mtoto wakati wa Ujauzito, wakati wa kujifungua na watoto wachanga na ikiwezekana vifo hivyo vitokemezwe kabisa.

Wito huo  umebainishwa wakati wa  kufunga  mafunzo ya  siku mbili  yaliyoandaliwa kwa Wataalam wa Afya wa Halmashauri za Mkoa wa Mwanza  yaliyofanyika tarehe 30 hadi 31 Januari 2023 katika  ukumbi wa MGS  Wilayani Misungwi,  ambapo amesema idadi ya Vifo bado ni changamoto  mwaka 2022 vifo vimeongezeka  hadi kufikia 165,mwaka 2021 vifo vya akina mama vilikuwa 164 na vifo kwa watoto ni 1,948 kwa mwaka 2022 na 2021 vifo vya watoto vilikuwa 1,533 na kusissitiza juhudi zifanyike ili kutokomeza.

"Simamieni vifaa vya kujifungulia  na kuhakikisha vinakuwepo  vituoni muda wote, na Serikali imeendelea kutoa fedha za dawa na vifaa tiba kupitia MSD," Alibainisha Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza..

Amesisitiza kuwa asingependa kusikia mama au mtoto amekosa huduma kwa kisingizio cha kukosa dawa, na kutoa angalizo kuwa, mojawapo ya vipaumbele vya Serikali kupitia Sekta ya Afya kwa mwaka 2023 ni ubora wa huduma. za Afya na dhamiara kubwa ni kutokemeza Vifo vya akina Mama wakati ujazito ,kujifungua, na kuhakikisha Vifo vya watoto wachanga katika siku 28 za mwanzo na chini  ya umri wa miaka mitano.

Pia Bw. Elikana amewakumbusha  Wataalam hao  kuhusu  Majengo yaliyoelekezwa na Serikali kujengwa yakamilishwe na yaanze kutumika mara moja, Mganga Mkuu wa Mkoa na Mganga Mkuu wa Wilaya  kuhakikisha wanasimamia  kikamilifu ili vituo  hivyo vikamilike kwa wakati,visajiliwe na vianze kutoa  huduma  ya afya kwa wananchi ambapo Serikali imewekeza fedha nyingi.

Bw, Elikana mewataka Wataalam  wa AFya  kuendelea  na kuongeza nguvu katika kutoa elimu kwa umma kuhusu Bima ya Afya kwa wote na kusimamia utekelezaji ili elimu ya Bima ya Afya itolewe kwa wananchi kupitia vituo vya kutolea huduma za afya na katika mikusanyiko na maeneo yote ambapo amewapongeza Sekta ya  Afya  Mkoani humo kwa utaratibu wa kufanya vikao kama hivyo vya kujadili maendeleo ya Sekta ya afya pamoja na changamoto zinazozikabili jamii na sekta ya afaya kwa ujumla.

Naye  Mganga  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa alieleza  kwamba wamepokea maelekezo ya Katibu Tawala na kuanza kuyafanyia kazi  na kuhakikisha kila Halmashauri  inatekeleza yote yaliyoazimiwa na wamejipanga  vizuri na imara katika  kuhakikisha Sekta ya Afya inazidi kuwa na matokeo chanya kwa kuzingatia uwepo wa vifaa tiba na huduma bora. Katika vituo vyote vya Afya.

Mafunzo hayo yamefanyika ikiwa ni kikao cha Robo Mwaka cha Wataalam  wa Sekta ya Afya  wa Halmashauri za Mkoa wa Mwanza yaliyolenga  kujadili Vifo vya mama vitokanavyo na uzazi pamoja na vifo vya watoto wachanga kilichofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Mhe, Elikana Balandya akizungumza na Wataalam wa Afya Katika kikao cha mafunzo ya kujengeana uwezo yaliyofanyika katika Wilaya ya Misungwi.

Baadhi ya Wataaalam wa Afya wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Viongozi kuhusu changamoto za sekta ya Afya 

Matangazo

  • TANGAZO,KIKAO CHA MADIWANI KWA ROBO YA PILI 2022/2023 February 10, 2023
  • TANGAZO LA MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI -MISUNGWI DC 2022 July 26, 2022
  • TANGAZO USAILI WAKUSANYA MAPATO HALMASHAURI MISUNGWI 2022/2023 August 01, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI HALMASHAURI YA MISUNGWI June 11, 2022
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • RC Malima atoa Kongole Wananchi Misungwi kujenga Kituo cha Afya kwa Mapato ya ndani

    March 05, 2023
  • DC Misungwi aagiza Miradi ya Maendeleo kukamilika kwa wakati Misungwi

    March 01, 2023
  • Baraza la Madiwani Misungwi lapitisha Bajeti Bilioni 54.6 mwaka wa fedha 2023/2024

    February 22, 2023
  • DC Matiko Paulo Chacha akabidhiwa Ofisi na Mkuu wa Wilaya Iringa Veronika Kessy

    February 08, 2023
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0768867886

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.