• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Prof.Ndalichako aagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya kudhibiti utoro mashuleni, wakati akifungua ofisi ya Uthibiti ubora Wilayani Misungwi.

Imewekwa : November 9th, 2019

Mradi wa Jengo la ofisi ya Uthibiti Ubora wa Shule wenye gharama ya shilingi millioni 134.5 umefunguliwa  na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe, Prof. Joyce Ndalichako (MB) katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza.

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Ndalichako mapema leo amefungua Jengo la ofisi za uthibiti ubora wa Shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ambalo limejengwa  kwa muda wa miezi sita (6) kuanzia  mwezi Mei 2019 na kukamilika mwezi oktoba 2019 baada ya Serikali kutoa fedha shilingi milioni 152 za ujenzi huo mapema mwezi Aprili mwaka huu 2019.

Jengo la ofisi ya Uthibiti ubora wa shule lilofunguliwa na Waziri wa Elimu ambalo limegharimu shilingi Milioni 134.5, tayari Watumishi wa Uthibiti ubora Wilaya ya Misungwi wameanza kunufaika na Mradi huu.

Akizungumza katika hafla ya ufunguzi, Mhe, Prof. Joyce Ndalichako amewataka  Viongozi na Watendaji ngazi ya Mikoa, Wilaya  nchini  kuhakikisha wanafuatilia na kukaa na Wataalam, na Wadau wa sekta ya Elimu kwa lengo la kutatua changamoto zilizopo katika suala la watoto wa shule Wavulana kwa Wasichana wanaoacha masomo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro na mimba zisizotarajiwa, kitendo ambacho kinasababisha kushuka kwa kiwango cha elimu hapa nchini.

Prof. Joyce Ndalichako ameeleza kwamba kwa mujibu wa taarifa za Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi takwimu zinaonyesha kuwa na  jumla ya Wanafunzi 3,838 ambao wameacha shule hadi kufikia mwezi Julai mwaka 2019 kutokana na sababu mbalimbaliza utoro na wengine kupata mimba za utotoni miongoni mwao watoto 2030 ni Wavulana na 1,808 ni Wasichana.

Akieleza na kufafanua zaidi kuhusu suala la elimu  “ tatizo la kuacha shule limekuwa sugu hususani kwa watoto wa kike kutokana na tatizo la mimba lakini nashangaa sana mbona watoto wa kiume  kuacha shule ndio wamekuwa wengi, tatizo ni nini, alihoji.”  Waziri Ndalichako.

Amewaagiza Viongozi wa Mikoa na Wilaya kusimamia kikamilifu na kuweka mikakati  madhubuti ya kutatatua changamoto na tatizo la watoto kuacha shule bila sababu ya msingi wakati Serikali inaendelea kutoa fedha za elimu bila malipo ambapo  hadi sasa imeshatumia takribani kwa ajili ya kugharamia shughuli za elimu bila malipo hapa nchini pamoja na miradi ya  ukarabati wa  majengo na miundombinu uliofanywa na tayari umekamilika katika shule kongwe  68  za Sekondari ambapo Serikali inatarajia kufanya ukarabati katika  shule za Sekondari 88 nchi nzima.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.Joyce Ndalichako akizungumza na Viongozi,Watendaji pamoja na Wananchi katika hafla ya ufunguzi wa ofisi ya Uthibiti ubora wa shule Wilayani Misungwi

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya tano imeweza kujenga majengo 100 ya ofisi za Uthibiti ubora wa shule hapa nchini kwa kutumia fedha shilingi Bilioni 15.2 na ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayofanya kwa Watanzania.

Amewapongeza Viongozi  na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kazi nzuri ya kusimamia vyema ujenzi wa ofisi hiyo kwa ushirikiano na kuhakikisha  jengo linakamilika kwa wakati kwa ubora na kiwango cha ujenzi na hatimaye wameweza kuwa na ziada ya shilingi million 17 ambayo itatumika katika shughuli zingine za maendeleo.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.