• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Naibu Waziri wa Elimu aridhika na kupongeza utekelezaji Miradi Sekta ya Elimu Misungwi

Imewekwa : July 6th, 2019

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe, William Tate Ole Nasha, (MB) ametoa pongezi kwa Viongozi na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi , kwa kutekeleza vyema  na kusimamia vizuri miradi  pamoja na maendeleo ya Sekta ya Elimu Wilayani humu.

Akizungumza na Viongozi na Watendaji wa Halmashauri wakati wa Ziara ya kikazi Wilayani humu , Mhe, Naibu Waziri William  Ole Nasha amesema kwamba amefurahishwa sana na juhudi zilzofanyika katika kutekeleza na kukamilisha miradi ya Sekta ya Elimu katika Halmashauri  ya Misungwi, ikiwemo miradi ya Ujenzi wa Nyumba ya Walimu (six in one), vyumba vya Madarasa, matundu ya vyoo uliokamilika, na Ujenzi wa Jengo la  Ofisi ya Uthibiti Ubora wa Elimu unaoendelea kwa sasa katika Halmashauri 100 nchini kote.

Mhe, William Tate Ole Nasha, Naibu Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia akizungumza kwa msisitizo kuhusu maendeleo ya Elimu kwa Watoto wa Kike ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Juma Sweda (aliyekaa kulia) wakati wa Ziara ya kikazi Wilayani  humu.

Mhe, William Tate Ole Nasha, ameeleza hayo mara baada ya kupokea taarifa fupi ya maendeleo ya  Wilaya iliyowasilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe, Juma Sweda, taarifa iliyoonyesha mambo na shughuli mbalimbali zilizotekelezwa kwa mwaka 2018/2019, hususani  Sekta ya Elimu ambayo iliiwezesha Halmashauri kuongeza ufaulu wa Wanafunzi wa darasa la Saba kuwa Washindi wa tatu katika Mkoa wa Mwanza , sambamba na Wanafunzi wa Kidato cha Nne kuwa katika nafasi ya Nne kimkoa kati ya Halmashauri za Wilaya Nane za Mkoa wa Mwanza kwa matokeo ya mwaka 2018.

Mhe, Naibu Waziri Ole Nasha, ameridhishwa namna Viongozi na Watendaji wa Halmashauri ya Misungwi wanavyosimamia na kutekeleza kwa kiwango na ubora miradi akitoa mfano mradi wa Nyumba ya Walimu (Six in One) katika Sekondari ya Isakamawe uliokamilika kwa gharama ya  shilingi 141,000,000 na umefunguliwa na  Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018 ,  

Amesema Halmashauri imeweza kusimamia vyema miradi ya  ujenzi wa Vyumba viwili ambayo  yote imekamilika katika Sekondari za Mbarika, Sanjo, Mamaye na Koromije  zote kwa gharama ya shilingi 100,000,000 za ufadhili wa Serikali kuu paoja na Mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa  na matundu ya vyoo katika Shule za Msingi Isela pamoja na Shule ya Msingi Sumbuka kwa shilingi 60,000,000.

Mhe, Naibu Waziri Ole Nasha, pia amewashukuru Viongozi na Watendaji Wilayani humu kwa kushirikiana katika  kazi ya ujenzi walioufanya katika mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Uthibiti Ubora unaondelea ambapo wamefikia hatua ya ukamilishaji na kwa mujibu wa maelezo ya Mthibiti Ubora Mkuu wa  Shule Wilaya, Faustine Salala kwamba ujenzi unasimamiwa na Kamati ya ujenzi  na tayari shilingi 60,000,000 zimeshatumika kati ya fedha zote shilingi 152,000,000 zilizotolewa na Serikali kutekeleza mradi huo, na matarajio makubwa ya kukamilisha ujenzi huo mwezi Agosti mwaka huu kwa ziada ambapo fedha hiyo wameahidi kutekeleza katika kununua samani za ofisi na kuongeza miundombinu mingine muhimu.

Jengo la Ofisi ya Uthibiti Ubora Wa Elimu linaloendelea kujengwa Wilayani Misungwi,limegharimu shilingi 60,000,000 mpaka hatua ya kuweka Fremu za Milango na Madirisha, pamoja  na Vigae,  upigaji wa Lipu ndani na nje na Kamati ya Ujenzi inaendelea na ukamilishaji hadi mwezi Agosti mwanzoni mwaka 2019.

“ Nawapongezeni sana kwa namna mnavyoshirikiana kutekeleza  na kusimamia vyema miradi na kuinua ufaulu wa Elimu katika Wilaya yenu ya Misungwi, na mumeweza kuwakamata na kuwafunga Gerezani Watu 30 wakiwemo Walimu na Watendaji  wengeni waliowapa Mimba  na kuwaoa Wanafunzi wa Kike”. Alieleza Naibu Waziri Ole Nasha.

Mhe, Naibu Waziri wa Elimu ameonyeshwa kukerwa na kukemea  vikali mambo ya kizamani yanayofanywa na Wanachi ya kuwaoa  na kuwapa Mimba Watoto wa Kike wanaosoma na kuharibu ndoto na fursa ya kuendelea kimasomo na kupoteza dira na mwelekeo wao katika maisha, na amewataka Viongozi na Watendaji wote Wilayani humu kuendelea kushirikiana na kutoa Elimu kwa umma juu ya umuhimu wa Watoto kusoma ili waweze kusaidia familia zao na taifa kwa ujumla.

 

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.