• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Naibu Waziri wa Afya aagiza Maafisa Elimu Sekondari nchini kote kuhamasisha Wanafunzi kusoma Masomo ya Sayansi.

Imewekwa : October 18th, 2017

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto,Dkt,Faustine Ndugulile amewataka Maafisa Elimu kote nchini kuhamasisha Wanafunzi wa Sekondari wa O-level kusoma masomo ya Sayansi ili kuwa na taifa la Madaktari na Wauguzi wa kutosha katika Vituo vya kutolea huduma za Afya.

Naibu Waziri wa Afya Dkt,Ndugulile amesema hayo wakati wa Uzinduzi wa Mradi wa kusaidia na kuimarisha utoaji wa huduma za Afya ujulikanao,"The more and better Midwives for Rural Tanzanai",unaofadhiliwa na Serikali ya Canada chini ya usimamizi wa Shirika la JPAEGO unaotekelezwa katika Halmashauri za Mikoa Nane (8) za Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi kwa kuwajengea uwezo Walimu wa Vyuo vya Uuguzi na Ukunga kuhusu uendeshaji na utoaji wa huduma za Afya kwa Wananchi.

Akizungumza katika Uzinduzi wa Mradi huo ulliofanyika katika Chuo cha Uuguzi na Ukunga cha Bukumbi Wilayani Misungwi,Mkoani Mwanza,Dkt,Ndugulile alisema ni wakati umefika sasa Watoto wajipange na kuhakikisha wanasoma masomo ya Sayansi kwa lengo la kuongeza na kuboresha fani ya Sekta ya Afya nchini kwa kutoa huduma bora za Afya kwenye Vituo vyote vya Afya kupitia Wataalamu wa Afya na kuweza kupunguza changamoto ya Vifo vya Akina mama Wajawazito na Watoto.

Alieleza kuwa changamoto ya Vifo vya Akina mama Wajawazito na Watoto ipo ambayo inakadiriwa kwamba kati ya Akinamama wajawazito 100,000 ambapo kunatokea Vifo takribani 556 ambavyo husababishwa na baadhi yao kutojifungulia katika Vituo vya kutolea huduma za Afya na kutozingatia kanuni  na Miongozo ya  Afya

Naibu Waziri wa Afya Dkt,Ndugulile alibainisha matarajio na na mipango ya Serikali katika kuboresha huduma za Afya nchini ambapo inatarajia kuajiri Watumishi wa Sekta ya Afya wapatao 3,410 hivi karibuni mara baada ya taratibu za kabali cha  ajira kukamilika, ili kuwezesha kuimarika na kuboresha huduma za Afya kwenye maeneo ya Zahanati,Vituo vya Afya an Hospitali za Wialya na Mikoa.

Amesema katika jitihada ambazo Serikali inaendelea  kuchukua za kuboresha na kuimarisha Sekta ya Afya nchini kwa kushirikiana na Wadau na Wahisani mbalimbali wa Maendeleo ni pamoja na kutoa Magari ya Wagonjwa (Ambullance) zaidi ya 50 zilizotolewa na kugawiwa hivi karibuni katika Wilaya na Mikoa mbalimbali kwa ajili ya kupunguza changamoto ya Vifo vya akina mama Wajawazito na Watoto.

Ametoa wito kwa Wananchi wote kuthamini na kutambua umuhimu wa huduma za Afya zitolewazo na kuwaomba kuhudhuria katika Vituo vya kutolea huduma za Afya kwa ajili ya kupima Afya zao na kupata matibabu sahihi kwa wakati muafaka na kuwataka kutojihusisha na vitendo vya utoaji wa Rushwa kwa lengo la kupata huduma za Afya.

Awali akizungumza na Wananchi na akitao Salamu za Wilaya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Juma Sweda,aliwashukuru Wadau wote wa Maendeleo hususan wa mradi huo ana kuahidi kusimamia kikamilifu ili uweze kuleta tiaj na ufanisi kwa manufaa ya Wananchi wa Misungwi na taifa na kuwataka Wauguzi na Wakunga wote kuchapa kazi kwa kutoa huduma bora  za Afya kwa kuzingatia miongozo na kanuni na maaadili ya  fani ya Sekta ya Afya  na kuleta matokeo chanya .

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa wito kwa Wananchi wilayani humu kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya kwa kila kaya kuchangia Tsh,10,000 kwa ajili ya kuwezeshwa kupewa matibabu kw awatu 6 toka kwenye Familia ambapo takwimu zinaonyesha kwamba hadi sasa ni wananchi takribani 9,100 tu ndio wameshajiunga kwenye mfuko wa bima ya afya wilayani na kwa upande wa utoaji wa huduma zaAfya kwa Wazee tayari Halmashauri imeshawapatia Vitambulisho zaidi ya Wazee 12,000 na zoezi linaendelea kwa wilaya nzima.

. 

  

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.