• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Naibu Waziri Awataka Watumishi Kutumia Taaluma zao Kutokomeza Unyanyasaji wa Kijinsia Wilayani Misungwi

Imewekwa : September 16th, 2023

Naibu Waziri  Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Mhe,Mwanaidi Ally Khamis awataka Watumishi kutumia taaluma zao kusaidia Watoto hasa wa kike na Taifa kwa ujumla Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Wito huo umetolewa jana wakati wa ziara ya Naibu Waziri  Maendeleo Jamii,Jinsia ,Wanawake na Makundi Maalum Mhe,Mwanaidi Khamisi alipotembelea na kukagua Miradi ya Maendeleo ya Ujenzi wa mabweni katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ufundi  Misungwi ambapo amewataka Watumishi kutumia taaluma zao kusaidia makundi maalumu wakiwemo,Wazee na Vikundi vya akina Mama ili kutatua changamoto zinazowakabili katika maeneo wanakoishi.

“Napenda kuwasihi Watumishi wote kutumia taaluma zao kuwasaidia na kulisaidia Taifa ili kuhakikisha wataalamu wenye fani mbalimbali za Maendeleo ya Jamii kutoa elimu kwa jamii nzima. “

Aidha Naibu Waziri Mhe,Mwanaidi Khamis amesisitiza kuwa Serikali imetoa Fedha za kutosha kwa ajili ya kukamilisha Miradi mbalimbali ya Maendeleo ambayo inatekelezwa na Serikali ya awamu ya Sita na kutoa wito kwa wakandarasi kusimamiwa kikamilifu ili kufanya kazi zao kwa wakati.

Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Paulo Chacha amesema kumekuwa na vitendo vya Watoto kike kuodheshwa wakiwa na umri mdogo jambo ambalo halikubaliki na Serikali imekuwa ikipambana na vitendo hivyo viovu ili kuvikomesha visitokee tena na kuwaonya watu wenye nidhamu mbaya kuacha kwa hiari vitendo hivyo na wasithubutu kuoa Watoto wadogo wala kuwafanyia unyanyasaji wa aina yeyote ile ikwemo kuwakatisha masomo ili waolewe.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Misungwi Bi,Ester Msoka ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Misungwi hapo awali akiwasilisha taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji amesema kuwa Ofisi ya Maendeleo Jamii imekuwa na  uhaba wa watumishi katika fani hiyo pamoja na ukosefu wa vyombo vya usafiri wa kwenda maeneo ya kazi na kuomba kupatiwa gari pamoja  pikipiki ili kurahisisha usafiri na utoaji wa elimu kwa Wananchi kwa wakati.

Naye Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ufundi {CDTTI} Bw, Charles Achuodho amesema kuwa Ujenzi wa mradi utakapokamilika utagharimu Shilingi Bilioni 2.2 ambapo awamu ya kwanza wamepewa kiasi cha fedha Shilingi Milioni 300.Pia ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ambayo inafanyika katika chuo hicho.

Diwani wa Kata ya Bulemeji Mhe,Rahma Fedelis ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita kutoa fedha zaidi ya shilingi Milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya Shule ya Sekondari Bulemeji na  Wananchi hawakuchangishwa fedha katika ujenzi huo wa madarasa lakini pia Mradi wa Maji wa Kata ya Bulemeji ambao bado unaendelea kutekelezwa kwa ajili ya manufaa ya Wananchi wa kata hiyo.

Naibu Waziri Naibu Waziri  Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Mhe,Mwanaidi Ally Khamis akisikiliza taarifa kutoka kwa Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii na Ufundi Misungwi Bw,Charles Achuodho jana mapema katika ziara yake ya kukagua Miradi mbalimbali ya Maendeleo chuoni hapo.

Naibu Waziri Bi Mwanaidi Khamis akiwa katika picha ya pamoja na Wazee wa Kituo cha Kaluande Bukumbi ambapo alitembelea na kuona makazi yao na kuwashili  Viongozi waendelee kuwatunza na kuwalea vyema.

Naibu Waziri Mhe,Mwanaidi Khamis akisalimiana na Viongozi wa Ngazi ya Wilaya ya Misungwi hapo jana wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua shughuli za miradi ya Kijamii Wilayani Misungwi.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.