• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Mwenge wa Uhuru wazindua na kufungua Miradi ya Bilioni 1.2 Wilayani Misungwi mwaka 2019

Imewekwa : May 16th, 2019

Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 umefungua na kuweka Jiwe la Msingi katika Miradi sita yenye thamani ya shilingi Bilioni 1,212,349,130/= kati ya Miradi saba yenye jumla ya shilingi Bilioni 1,638,287,062/= ulipokuwa unakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza mapema jana. 

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Mzee Mkongea Ali aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kutekeleza Miradi vizuri na kwa ubora na kwa kuzingatia viwango vya ujenzi vinavyotakiwa chini ya usimamizi wa Viongozi wote pamoja na Mhandisi wa Ujenzi na kuhakikisha inatekelezwa na kukamilika kwa wakati na kufuata vipimo na maelekezo ya Serikali ya awamu ya tano.


Jengo la Bima ya Afya lilojengwa katika Hospitali ya Misungwi

Mzee Mkongea Ali alitoa pongezi hizo wakati akizindua na kufungua Mradi wa Nyumba ya Walimu Six in One katika Sekondari ya Isakamawe wenye thamani ya shilingi Milioni 141,000,000/= pamoja na Mradi wa Jengo la Bima ya Afya Katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi uliotekelezwa kwa shilingi Milioni 198,028,930/=, miradi ambayo imejengwa kwa ubora na kiwango na kulingana na thamani ya fedha iliyotumika na amewataka Wananchi wayatumie na kuyatunza Majengo hayo vizuri ili yaweze kutoa huduma kikamilifu sambamba na kudumu kwa muda mrefu.

 Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Peter Michael akikabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Kaimu  Mkuu wa Wilaya ya Sengerema,Joseph Kapunda tarehe 15 Mei mwaka huu.

Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wakati akitoa ujumbe wa Mwenge kwa mwaka 2019, amewataka Wananchi wa Wilaya ya Misungwi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwezi Oktoba mwaka 2019 ili kuweza kutumia haki ya kikatiba ya kuchagua Kiongozi anayemtaka kwa kuzingatia sifa na vigezo, pamoja na kuongeza bidii katika kuchapa kazi ili kuleta maendeleo ya kiuchumi na kuhakikisha wanaunga mkono juhudi za Mhe,Rais wa Tanzania katika kujenga uchumi wa kati na wenye Viwanda vingi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda awali akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba ambaye awali alikabadhiwa Mwenge huo wa Uhuru na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Christopher Kadio, alisema kwamba Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Misungwi zitakimbizwa kwa umbali wa kilomita 115 na kufungua, kuweka jiwe la Msingi, kuzindua na kukagua jumla ya Miradi 7 yenye thamani ya Bilioni 1,638,287,062/= ambayo ni miradi ya Sekta ya Viwanda, Maji, Elimu, Barabara, Afya, na Mazingira ambapo Kauli Mbiu ya mwaka huu 2019 ni Maji ni Haki ya kila mtu, tutunze vyanzo vyake na Tukumbuke kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka huu, Wilayani Misungwi umepokelewa Kimkoa katika Kijiji cha Mwawile, Kata ya Nhundulu, kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini, Mkoa wa Shinyanga na Wilaya ya Misungwi ilikabidhi Mwenge huo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema tarehe 15, Mei 2019.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.