• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ahimiza ukusanyaji Mapato Wilayani Misungwi

Imewekwa : August 7th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe, Adam Malima  ahimiza Halmashauri  kuongeza ukusanyaji wa Mapato Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe, Adam Malima katika ziara ya kujitambulisha na kupokea taarifa ya maendeleo ya miradi  Wilayani Misungwi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa  ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa Fedha 2021/2022 kwa kuvuka asilimia mia moja.

Amesema hayo  katika ukumbi wa Halmashauri wa Wilaya ya Misungwi ambapo ametoa dira ya maendeleo katika kuwahudumia Wananchi kufuatia kuteuliwa hivi karibuni na Mhe,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe,  Samia Suluhu Hassan kuongoza Mkoa wa Mwanza.

“Napenda kuwapongeza sana Mkurugenzi na timu ya  menejimenti yako kwa ukusanyaji wa mapato  ya ndani mmevuka malengo yenu lakini pamoja hilo muongezee ubunifu na jitihada za dhati katika kukusanya mapato ili kufanikisha malengo mliojiwekea ya kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 3.1 kwa mwaka wa fedha 2022/2023.” Alisema Mhe, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

 Akizungumza na Watumishi Wilayani Misungwi  ametoa rai kwa  Mamlaka ya MWAUWASA na RUWASA kuhakikisha wa wanatatua changamoto ya maji kwa wakati  ili wananchi waweze kupata maji safi na salama katika maeneo yao,wakati huohuo amewataka TANESCO kuhakikisha wanapeleka huduma ya umeme kwa wananchi na kupata umeme kwa wakati.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa,Mhe,Balandya Elikana amewataka watumishi kutumia nafasi walizo nazo kwa uaminifu mkubwa ,kujituma na kufanya kazi kwa bidii na kwa ushirikiano ili kuwapa wananchi huduma bora na stahiki ili kutimiza dhima ya Serikali ya awamu ya sita kwa maendeleo  ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Veronika Kessy  amesema kuwa Halmashauri imeweza kukusanya Mapato ya ndani  kwa kipindi cha miaka mitatu mwaka wa fedha2019/hadi 2022  yameongezeka kutoka shilingi 2.3 sawa na asilimia mia moja na moja hadi kufikia shilingi bilioni 2.7 sawa na ongezeko la asilimia mia moja kwa  mwaka fedha 2021/2022 na kipindi cha 2022/2023 wameweka Malengo ya kukusanya shilingi bilioni 3.1 sawa na ongezeko la asilimia kumi na saba ambapo kwa Mwezi Julai wameweza kukusanya kiasi cha shilingi 200,3793,000/=sawa na asilimia 7.3.

Bi Veronika Kessy ameongeza  kwamba Halmashauri   inandelea na uboreshaji wa  ukusanyaji, usimamizi na udhibiti wa mapato kwa kutumia mashine za kiletroniki yaani Pos,Sambamba na hilo ameongeza kuwa  Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi imeendelea kutoa mikopo ya mapato ya ndani ya asilimia kumi isiyokuwa na riba kwa kina mama,vijana na walemavu na imeendelea kusajili vikundi kwenye mfumo ambapo kwa sasa vikundi 300 kwa mwaka 2021/2022 vimeweza kusajiliwa na zaidi Kiasi cha shilingi 200,000,000/ zimetolewa kwa vikundi 16 vya wanawake,vikundi 6 vya vijana na watu 5 wenye ulemavu.

Naye Mbunge wa Jimbo la Misungwi Mhe,Alexender Mnyeti amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe, Adamu Malima kwa ujio wake katika Halmashauri ya Wilaya Misungwi kujitambulisha kwa wananchi na kupokea taarifa maendeleo ya miradi na kuahidi kufanya kazi kwa ushirikano mkubwa ili kuleta maendeleo kwa wananchi  na Taifa kwa ujumla.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe,Adam Malima(katikati) akiwasili katika  Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Misungwi kwa lengo la kupokea taarifa ya Miradi ya maendeleo na kujitambulisha kwa Viongozi pamoja na wananchi ,Kushoto Mkuu wa Wilaya Mhe, Veronika Kessy na Nyuma ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza aliyevaa koti jeusi ni Katibu tawala wa Mkoa wa Mwanza Mhe,Balandya Elikana na wengine ni Viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo Agost 6,2022'

Baadhi wa Viongozi wa dini,Wakuu wa Idara na Vitengo na watumishi wengine wakisikiliza kwa makini na kupokea Maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe,Adam Malima katika ziara ya kupokea taarifa za maendeleo ya Miradi na kujitambulisha katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Agosti 6,2022.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.