• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Mkurugenzi wa Halmashauri awataka Wanafunzi wa Kike kuthamini Masomo ya Sayansi ili kutumia fursa za Viwanda

Imewekwa : May 5th, 2017




Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri,Eliurd Mwaiteleke, amewataka na kuwaasa Wanafunzi wa Kike kuthamini na kufaulu vizuri katika Masomo ya Sayansi ili kujiandaa kuzitumia fursa za uwepo wa Viwanda katika maeneo mbalimbali hapa nchini kwa kutumia taaluma ya Sayansi watakayoipata kwa maanufaa yao na hatimaye kukuza Uchumi wa taifa.

Wito huo kwa Wanafunzi hususan wa Kike ulitolewa wakati Hafla maalum ya Chakula cha Jioni kilichondaliwa  na Uongozi wa Shule ya Sekondari ya Misungwi ambapo Mkurugenzi Mtendaji akiambatana na baadhi ya Wakuu wa Idara wa Halmashauri walikula  pamoja na Wanafunzi wa KIdato cha tano na Sita wakiwa na wanajumuiya, Wafanyakazi na Walimu wote wa Shule hiyo kwa lengo la kuwatakia heri na baraka katika Mitihani yao ya Kidato cha Sita mwezi Mei 2017,ambapo jumla ya Wanafunzi wa kike 44 wanamaliza masomo katika mchepuo wa CBG (26) na EGM (18),

Mwaiteleke amewasihi na kuwaombea wanafunzi hao wa kidato cha Sita kufaulu kwa kiwango kikubwa cha daraja la kwanza ili kuweza kupata fursa ya kuendelea na Chuo Kikuu na hatimaye kuhitimu masomo ya Elimu ya  juu na kulitumikia taifa hususan katika nyanja na sekta ya Viwanda ambao ndio mwelekeo na dira ya nchi yetu kufikia katika uchumi wa Viwanda na Vijana wa kike ndio nguzo safi na taifa linathamini na linahitatji  mchango wao na kuwaeleza kwamba Serikali inaandaa mazingira mazuri ya ajira na fursa nyingi zitatolewa kawa Wasomi hususani  Vijana wa Kike.

'Wanafalsafa wanasema ukimwelimisha mwanamke umeelimisha jamii nzima na Taifa kwa ujumla".Alisema kwa msisitizo Mkurugenzi Mwaiteleke,na kuwaomba wanafunzi hao kumtegemea na kumtanguliza Mungu katika kila jambo na kutenga muda na ratiba vizuri ya kusoma kwa lengo la kujpata mafanikio yao jamii na taifa kwa ujumla wake.

Mkurugenzi Mtendaji,Mwaiteleke pia ,aliwaagiza Wakuu wa Shule zote Wilayani hapa kuanzisha na kuendeleza mpango mkakati wa kufanya Midahalo mbalimbali ya kujadili masuala na mambo ya kielimu ambapo utaratibu huu utawawezesha wanafunzi kupaena na kubadilishana uzoefu na kuongeza busara,maarifa na kuwa na fikra na uwezo mpana wa kupambanua mambo ya kiuchumi na kijamii na kuandaa taifa la Vijana wenye kufanya kazi kwa kutumia taaluma na Weledi mkubwa na kuelekeza Idara ya Elimu Sekondari kufuatilia na kusimamia Vizuri utekelezaji wa Midahalo 

Akielezea mafanikio na maendeleo ya Shule na kitaaluma Mkuu wa Shule hiyo,Mathias Homboyo amesema kwamba maendeleo ya kielimu shuleni hapo nai mazuri akitoa mfano wa ufaulu wa Wanafunzi wa kidato cha Nne na Sita walifanya vizuri sana kwa mwaka 2016 ambapo matokeo ya Kidato cha Sita waliofanya mtihani walikuwa 126 na wote walifaulu katika madaraja ya Wanafunzi 120 walipata daraja la tatu hadi la kwanza na Wanafunzi 6 tu ndio walipata daraja la Nne,na kulingana na maandalizi ya Wanafunzi na walivyofundishwa na Walimu wao alisema wanamatarajio ya kufanya vizuri tena kwa mwaka 2017 na kuwasihi Vijana  82 wengine wa kike .wanaosoma kidato acha tano wafuate mfano wa wanafunzi waliowatangulia na kusoma kwa bidii na maarifa na wao kufaulu kwa kiwango kizuri.








Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.