• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Mkurugenzi Mtendaji awataka Watendaji wa Kata na Vijiji kutekeleza Ilani kwa Vitendo

Imewekwa : November 7th, 2017




Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi,amewataka Maafisa Watendaji wa Kata na Vijiji kutekeleza kwa Vitendo Ilani ya Uchaguzi inayoelekeza mambo yaliyoanishwa ya utekelezaji wa miradi na masuala ya maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla kwa kipindi cha miaka mitano ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri,Eliurd Mwaiteleke amewataka Watendaji hao kutekeleza kikamilifu na kwa Vitendo Miradi na shughuli  kwa kuzingatia kiwango na ubora na kuhakikisha thamani ya fedha inafikiwa kwenye miradi ya maendeleo na kuleta matokeo chanya na manufaa kwa Wananchi.

Mwaiteleke,alibainisha na kueleza hayo wakati wa Ziara ya kikazi aliyoifanya katika Kata tatu mfululizo ambazo ni Kata ya Kijima,Nhundulu,na Isesa kwa ajili ya kukagua na kuona hali halisi ya utekelezaji wa miradi na shughuli mbalimbali zinazotekelezwa,kwenye Kata 27 na Vijiji vyote 113 vya Wilaya hii ambapo  ameshatembelea Kata 21 hadi sasa.

Mkurugenzi Mwaiteleke,katika ziara hiyo amewataka Watendaji wa vijiji,Walimu Wakuu,Waganga Wafawidhi wa Zahanati na Wakuu.wa Shule kuhakikisha wanasimamia na kutekeleza vizuri Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015 ambayo imeelekeza katika kuboresha na kuimarisha maen eo ya Sekta za Elimu,Afya,Maji,Ardhi na Maliasili,Kilimo na Ushirika na Umwagiliaji,Miundombinu na Ujenzi,Maendeleo ya jamii,Biashara na Uwekezaji wa Viwanda ,Misitu,Tehama na Ukusanyaji wa Mapato yatokanayo na Ushuru na Kodi mbalimbali za Halmashauri na Serikali kuu.

Aliwataka Watendaji ambao hawakai katika Vituo vya Kazi kuhamia mara moja katika maeneo yao ya kazi Vinginevyo hatua kali za Kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao kwa kukiuka kanuni na taratibu za kazi,hivyo kuwa katika Vituo vya kazi ili kuweza kuwahudumia Wananchi kwa ubora na ufanisi zaidi pamoja na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhakikisha inatekelezwa kwa kuzingatia thamani ya fedha iliyotolewa na kukamilika kwa wakati na kwa kiwango kinachokidhi vigezo vya Serikali,vile vile waweze kuzingatia sheria,Kanuni na taratibu na maadili ya kazi na utumishi wa umma na kuweza kutimiza wajibu.

Mkurugenzi Mwaiteleke, ameweza kukagua na kuona utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa majengo ya Wodi katika Zahanati ya Mwawile,mbayo imekamilika boma pamoja hali halisi ya ukarabati ana uboreshaji wa miundombinu ya Zahanati kwa fedha za RBF ambazo zinatolewa kwa masharti ya ufanisi kwa kazi ambapo Kila Zahanati ilipewa Tsh,10,000,000/= na baadhi wamezitumia vizuri na wengine hawakufanya kwa kiwango kinachotakiwa katika uboreshaji na ukarabati wa miundombinu ya Zahanati husika,aliagiza Idara ya Afya kufuatilia kwa karibu matumizi ya fedha hizo na kutoa taarifa iliyokamilika.

Alitembelea pia katika Shule za Msingi na Sekondari na kukagua utekeleza wa miradi mabalimbali ikiwemo ujenzi wa Vyumba vya madarasa na Vyoo pamoja na Nyumba za Walimu ambapo inaonyosha hali ya upungufu wa Vyoo kwenye Shule nyingi ni tatizo na kuwaagiza Viongozi wa Vijiji kuweka mikakati ya kuanzisha ujenzi huo,na kuweza kujenga madarasa ili kukabiliana na wingi wa idadi ya wanafunzi watakaoanza shule mwaka 2018,pia kuwezesha ujenzi wa Nyumba za Walimu kwa ajili ya kukaa Walimu watakaopelekwa kufundisha katika shule husika.

Amewataka Viongozi wote wa Vijiji na Vitongoji kushirikiana na Watendaji wa Vijiji katika shughuli zote za kuibua miradi ya maendeleo na kuhamasisha wananchi kuchangia miradi hiyo kwa wakati na kushiriki katika shughuli za maendeleo kwa nguvu zao kwa lengo la kuharakisha kasi ya maendeleo wilayani na taifa kwa ujumla .

Katika ziara hiyo ameweza kuambatana na maafisa wa Halmashauri kutoka Idra na Vitengo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Idara ya Mipango na Takwimu,Afya,Maji,Elimu Msingi na Sekondari,Maendeleo ya jamii ,Ujenzi,Biashara na Fedha na Habari na Mawasiliano ambao wamewaza kuhamasisha na kutoa uzoefu kwa Viongozi na Watendaji wa Vijiji na Kata ili kujenga uelewa wa mambo na miradi mbalimbali inayotekelezwa vijijini.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.