• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Misungwi yatoa zawadi ya Vinyago,yajipanga kufuta daraja sifuri Matokeo Kidato cha 4 mwaka huu 2020

Imewekwa : March 8th, 2020

 Halmashauri ya Wilaya ya  Misungwi,  Mkoani Mwanza, imeanza kutekeleza mpango wa utoaji wa zawadi za vinyago kwa viongozi wa Kata na shule  zilizopata ufaulu hafifu  katika matokeo ya Mitihani ya taifa ya shule za Msingi na Sekondari ya mwaka 2019, ili kuhamasisha jitihada za  ushindani  hatimaye kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Akizungumza katika kikao cha Wadau wa Elimu Wilayani Misungwi,kilichofanyika katika Ukumbi wa MGS Misungwi hivi karibuni,  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba  amesema kwamba katika Elimu suala la Motisha ni la msingi na muhimu sana na tayari utaratibu wa kutoa zawadi  umeanzishwa rasmi na ni endelevu ambapo Shule na Kata zitakazokuwa zinafanya vizuri zitapewa zawadi chanya ikiwemo vyeti, ngao, vifaa  na fedha taslimu sambamba na kutoa zawadi hasi kwa wale watakaofanya vibaya katika matokeo ikiwa ni pamoja na kupatiwa zawadi ya Vinyago.

Bw, Kisena ameeleza kuwa Halmashauri imeamua na kuweka mkakati  na malengo ya kuhakikisha Wanafunzi wa shule za msingi wanafaulu kwa asilimia 100 na wote wanajiunga na Sekondari  pamoja na kuongeza ufaulu kwa Wanafunzi wa Sekondari sambamba na kufuta daraja sifuri kwa mwaka huu 2020 na baadae kuondoa ufaulu wa daraja la 4 katika shule zote za Sekondari Wilayani hapa.

Afisa Elimu Sekondari Wilaya, Diana Kuboja  amesema kuwa shule za msingi zilizofanikiwa kupata zawadi ya ushindi ni  pamoja na shule tatu za  Serikali ambazo ni Mwakiyenze, Kwimwa na Ngeleka na shule ya Lwasa English medium inayomilikiwa na mtu binafsi, aidha, kwa upande wa Sekondari, shule zilizofanikiwa kufanya vizuri ni Ipwaga Sekondari inayomilikiwa na mtu binafsi, pamoja na shule ya Serikali ya  Sekondari ya  Mbarika, zilizofanikiwa kufuta daraja sifuri katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana.

Bi, Diana Kuboja amezitaja shule zilizopata ufaulu hafifu na kushika mkia  kiwilaya  ni, shule ya Sekondari Mawematatu ya Kata ya Mabuki na shule ya msingi Mwamazengo iliyopo Kata ya Lubili katika matokeo ya mitihani ya Taifa ya shule za Sekondari na Msingi mwaka jana, ambapo Kata ya Nhundulu imeshika nafasi ya mwisho kiwilaya

Wakati huo huo, Shule tatu za Serikali kati ya shule ishirini na nane za Sekondari za wilayani humu, zimeibuka kuwa shule bora katika matokeo ya Kidato cha nne mwaka jana Shule hizo ni pamoja na Mbarika Sekondari, Nyabumhanda Sekondari pamoja na Sekondari ya Paulo Bomani, baada ya kupata idadi kubwa ya kiwango cha ufaulu kuanzia daraja la kwanza, daraja la pili na daraja la tatu huku matokeo hayo yakiashiria kiwango cha juu cha ufaulu wilayani hapa,

Bi, Kuboja aliongeza kwamba zawadi zilizotolewa kwa shule bora za Sekondari ni pamoja na vifaa vya maabara  vyenye thamani ya shilingi milioni 10 pamoja na fedha taslimu shilingi milioni tatu, wakati shule za msingi zikipatiwa fedha taslimu shilingi milioni moja na laki nne, pamoja na ushindi huo pia shule ya Sekondari Misungwi imeibuka kidedea, baada ya kufuta daraja la nne na daraja sifuri, katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka jana.  

Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi imefanikiwa kushika nafasi ya 3 kimkoa katika ufaulu wa Mtihani wa kidato cha Nne  na nafasi ya 90 kitaifa kwa ufaulu wa asilimia 82 sambamba na kupata nafasi ya 5 kimkoa katika ufaulu wa Mtihani wa kumaliza Elimu ya msingi na nafasi ya 117 kitaifa kwa ufaulu wa asilimia 79.6 mwaka jana 2019.

Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ina jumla ya shule za msingi 149 ambapo kati  ya hizo shule tisa zinamilikiwa na watu binafsi, huku shule za Sekondari zikiwa 34 ambapo kati ya hizo shule sita zinamilikiwa na watu binafsi.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda (wa tatu kushoto) akikabidhi Zawadi ya Vifaa vya Maabara kwa Viongozi wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Mbarika iliyofuta daraja sifuri mwaka 2019, ( wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba na katikati ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya, Daud Gambadu akifuatiwa na Diwani wa Kata ya Mbarika, Joel Dogani.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba akizungumza  na wadau wa Elimu kwa msisitizo kuhusu Viongozi wa Kata na Vijiji kusimamia Elimu mashuleni na kuweka mikakati ya kuongeza ufaulu wa Wanafunzi katika Mitihani yao ya darasa la saba na kidato cha Nne na sita na hatimaye kuondoa na kufuta daraja sifuri na daraja la 4 mwaka huu 2020.



Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.