• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Misungwi yadhamiria kupunguza tatizo la Lishe kwa Wanafunzi Shule za Msingi na Sekondari mwaka 2024/2025.

Imewekwa : June 19th, 2024

Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi Bw. Abdi Makange  kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Johari Samizi amewataka Maafisa na Watendaji wa Kata kusimamia na kuhakikisha Watoto wa shule za Sekondari na Msingi wanapata Chakula kwa asilimia 100 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Wito huo ameutoa Leo Juni 19, 2024 wakati akifungua kikao cha Tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa shughuli za Lishe katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kipindi cha kuishia robo ya tatu ya mwezi Machi 2024 ili kuongeza ufaulu na mahudhurio ya Wanafunzi Shuleni kwani lishe bora inamchango mkubwa katika kuyafanikisha hayo.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Dkt. Clement Morabu kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Misungwi ameeleza kwamba utekelezaji wa mkataba wa shughuli za lishe unaendelea vizuri katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi hususani  katika utoaji wa Chakula shuleni ambapo zoezi hilo limefanikiwa kwa asilimia 95 ambapo kati ya Shule 178 na Shule ambazo zimekuwa na changamoto tayari wameweka mikakati kwa kushirikiana na Watendaji wa Kata ambao ndiyo wasimamizi wakuu wa shughuli hiyo ili kufikia asilimia 100 ifikapo robo ya nne.

Dkt. Morabu  ameeleza kwamba mbali na kushughulikia suala la utoaji wa chakula Shuleni Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi imefanikiwa kuwafikia watoto wenye changamoto ya utapiamlo na kuwapeleka katika vituo vya afya ambako wameendelea kupatiwa huduma stahiki za Afya na watoa huduma za afya kwa ngazi ya jamii ambao pia wamekuwa wakishirikiana nao kwa ukaribu kufanikisha zoezi la lishe bora kama ilivyoelekezwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Naye Afisa Mtendaji wa Kata ya Kanyelele Bw. Thomas Shunashu amesema kuwa katika kata hiyo wameweka kipaumbele suala la lishe kwenye ngazi zote kwa sababu lishe bora ndiyo msingi wa kuondoa udumavu na kupunguza magonjwa nyemelezi na hivyo wamefanikiwa kutoa chakula kwa wanafunzi katika Shule za Msingi 7 na Shule za Sekondari 2 baada ya kuwahamasisha wananchi kupitia vikao na hatua hiyo imesaidia wanafunzi kuendelea kupata muda mwingi wa kujifunza.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kata ya Nhundulu Bw. Msobi Daniel ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta mpango wa lishe bora nchini ili kuleta tija kwa jamii hususani wanafunzi kwa kuhimarika zaidi kitaaluma na kiafya.

Bw. Msobi Daniel amesema kwamba Shughuli ya lishe bora katika Kata ya Nhundulu imetekelezwa kwa asilimia 100 baada ya kuwashirikisha Wananchi kupitia mikutano ya hadhara ambapo Wananchi  wa kila Kijiji wamejitoa kuchangia Chakula kwa ajili ya wanafunzi na hatua hiyo imeendelea kuongeza uelewa wa lishe bora kwa Wananchi kutokana na hamasa wanayoipata kutoka kwa Viongozi wao wakiwemo Wenyeviti wa Vitongoji.

Mganga Mkuu Wilaya ya Misungwi Dkt. Clement Morabu (kushoto)akiwa pamoja na Lucia Basili wakati wa Kikao cha Lishe kilichofanyika katrika Ukumbi wa Halmashauri ya Misungwi.


Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DAS Misungwi awapongeza Watendaji Halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani katika kuongeza ufanisi na ukusanyaji wa Mapato.

    April 29, 2025
  • Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yafanya ziara ya yatembelea na kupata mafunzo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya nyang'hwale Mkoani Geita

    April 25, 2025
  • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango yaridhishwa na miradi ya maendeleo ya Halmashauri Wilaya ya Misungwi

    April 23, 2025
  • Kamati ya Lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yawataka Watendaji wa Kata na Vijiji kutoa Elimu ya Shughuli za Lishe kwa Wananchi.

    February 27, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.