• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Misungwi yaanza zoezi la utoaji wa Leseni za Makazi kwa Wananchi

Imewekwa : July 14th, 2021

Serikali yaanza zoezi la upimaji wa ardhi na utoaji wa Leseni za makazi kwa Wananchi wa Kata ya Misungwi katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji ,Afisa Ardhi na Maliasili wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Fredrick Nyoka  ameeleza kwamba Serikali imeamua kuanza upimaji na kutoa Lesini za Makazi katika maeneo ambayo hayajapimwa kwenye Vitongoji ambavyo vipo maeneo ya Miji kwa maana ya  kutambua na kupanga  makazi vizuri na kuweza kurasimisha kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi pamoja na maendeleo kwa ujumla.

Bw, Nyoka amesema kwamba katika Kata ya Misungwi Leseni hizo za makazi zitatolewa kwa Wananchi wa Vitongoji vya Masawe, Misungwi D, Misri, na Mitindo na kwamba Vitongoji hivi havikuwekwa kwenye mpango wa urasimishaji wala katika mpango wa upimaji wa Halmashauri ambapo zoezi litaendelea katika Kata zingine.

Kwa upande wake Afisa Ardhi na Upimaji kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi Bi, Beatrice Gowele amewaeleza Wananchi katika Mikutano yao ya Vitongoji kwamba Leseni za makazi ni nyaraka halali ya umiliki wa ardhi chini ya kifungu namba 23 ya mwaka 1999 ambayo inatolewa na kudumu kwa muda wa miaka mitano na baadaye inahuishwa, na kueleza kwamba maeneo  ya Wananchi yatakuwa na thamani zaidi mara baada ya kutolewa kwa Leseni za makazi na kupata fursa ya kukopa katika taasisi za kifedha na kuongeza mitaji kwa Wafanyabiashara.

Bi, Beatrice Gowele amesema kwamba Wananchi watapaswa kulipia shilingi elfu kumi katika akaunti ya Serikali amabyo ni gharama kwa kila kiwanja maara baada ya zoezi kukamilka na watapewa Leseni hizo za makazi na kuendelea  na matumizi yao kwa kujenga Nyumba za makazi bora na  Serikali itaweza kukusanya kodi ya ardhi vizuri kutokana na kuwatambua.

Naye Afisa Mipango Miji kutoka Ofisi ya Kamishina wa Ardhi Kanda ya Mwanza Bw, Athuman Simba amewataka Wananchi kujiandaa kikamilifu na kuwa tayari na zoezi hili kwa kutatua na kuondoa migogoro yote inayohusu maeneo na ardhi na kuwatahadharisha kwamba katika zoezi hilo Wataalam wa ardhi hawatahusika na utatuzi wa mgogoro bali watafanya upimaji katika maeneo ambayo hayana changamoto katikamatumizi na mipaka.

Ameongeza kuwa Wananchi ni muhimu kubainisha vizuri mipaka ya maeneo, kuweka na kutenga maeneo ya barabara, maeneo ya michezo, maeneo ya wazi,  taasisi za umma, maeneo ya makanisa, ambayo katika utoaji wa Leseni za makazi yataombewa kupitia bodi za Wadhamini kwa lengo la kuepusha migogoro ya baadae.

Baadhi ya Wakazi wa Kitongoji cha Misri Kata ya Misungwi wakisikiliza maaelezo kutoka kwa Afisa Mipango Miji wa Kanda ya Mwanza Mohamed Simba (hayupo pichani) wakati wa Mkutano wa kutoa taarifa kwa  Wananchi kuhusu utoaji wa Leseni za Makazi kwa Wananchi ambao hawajapimiwa Viwanja.

Afisa Mipango Miji wa Kanda ya Mwanza Athuman Simba akizungumza na Wakazi wa Kittongoji cha Misri wakati wa Mkutano wa utoaji wa Elimu kwa Wannachi kuhusu zoezi la utoaji wa Leseni za Makazi kwa Wananchi wa Kata ya Misungwi.

Baadhi ya Wanakamati ya zoezi la Utoaji wa Leseni za Makazi iliyochaguliwa katika Kitongoji cha Masawe B, Kata ya Misungwi ambayo inafanya kazi na WAataalam wa Ardhi wa Mkoa na Wilaya.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.