• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Miradi Uboreshaji Miundombinu Elimu msingi na Sekondari (Boost na Sequip) yenye thamani Bilioni 3.3 kuleta manufaa makubwa kwa Watoto Misungwi

Imewekwa : September 18th, 2024

Shilingi Bilioni 3.3 zaendelea kutekeleza ujenzi wa miradi ya uboreshaji mazingira ya sekta ya Elimu ya awali na msingi pamoja na Sekondari kuanzia mwaka wa fedha 2022/2023 kupitia mradi wa Boost na Sequip nchini na kupunguza kero kwa Wananchi Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika ziara ya kukagua miradi hiyo ya Boost Mwakilishi wa Shirika la Benki ya Dunia Dkt. Safari Aquiline ameridhishwa na utekelezaji wa miradi ya Boost na Sequip ambapo miradi hiyo ililetwa kwa lengo la kutoa elimu bora kwa Wanafunzi kupitia ujenzi wa Madarasa yaliyojengwa, ujenzi wa vyoo pamoja na madawati uliotekelezwa kwa Shule za Msingi 2 za Mwabebea na Shilabela pamoja na shule mpya ya Sekondari ya Mwambola na amempongeza na kumshukuru Rais Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kutoa fedha nyingi katika miradi ya elimu kwa muda mfupi na amefurahi kushuhudia miradi hiyo imetekelezwa vizuri na kwa kuzingatia viwango na ubora pamoja na suala uhifadhi na utunzaji wa mazingira na kuwataka kuendelea kubuni na kutatua changamoto zingine zilizopo ikiwemo ukosefu wa maji na nishati ya umeme.

Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya awali na msingi OR - TAMISEMI Bi. Susan Nusu akizungumza na Viongozi na Watendaji wakati wa ziara ya ukaguzi na uhakiki miradi ya Boost Sequip Wilayani Misungwi hivi karibuni.

Naye Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya awali na msingi OR- TAMISEMI Bi. Susan Nusu amepongeza juhudi za makusudi kwa Viongozi na Watendaji wa Halmashauri ya Misungwi kwa kufanya kazi kwa ushirikiano, weledi na uaminifu na kuhakikisha miradi ya Boost na Sequip inatekelezwa kikamilifu na kukamilika kwa wakati na viwango na ubora kwa kuzingatia maelekezo na miongozo ya Serikali na hatimaye kufikia lengo la kupunguza ama kuondoa adha na kero ya Watoto kutohudhuria shule kutokana na miundombinu na mazingira mabovu ya shule za msingi na Sekondari nchini.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu Archt. Chagu Ng’homa kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza amesema Watendaji wamejitaidi na kwa uaminifu mkubwa katika kuhakikisha miradi hiyo ya Boost na Sequip inakamilika na inazidi kwenda vyema kwa kujengwa kwa kiwango cha hali ya juu na ubora na hatimaye kukidhi na kujibu changamoto za watoto kutokwenda shule kutokana na uhaba wa majengo ya madarasa pamoja na madawati na mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia.

Akitoa taaarifa ya utekelezaji wa miradi ya Boost na Sequip  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw. Addo Addo Missama ameeleza kuwa Halmashauri imefanikiwa kupata fedha shilingi Bilioni 1.9 kujenga shule za awali na msingi mpya 2 na kukarabati shule zingine 7, sambamba na fedha shilingi Bilioni 1.4 zilizotumika kutekeleza miradi ya Sequip ikiwemo ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Mwambola iliyogharimu shilingi Milioni 584.2 pamoja na ujenzi wa miundombinu katika Shule za Sekondari zingine 5 ambapo Viongozi na Watendaji wamehakikisha fedha hizo zimetekeleza shughuli za ujenzi kwa wakati na kwa kasi ambayo inaridhisha ili kurahisisha shughuli pamoja na kuongeza kiwango cha ufaulu kwa Wanafunzi na kupunguza adha na kero kwa watoto kutembea umbali mrefu na msongamano darasani.  

Bw. Addo Missama amesema fedha zilizotolewa na Serikali kwa mwaka 2022/2023 kwa ajili ya kutekeleza mradi ni shilingi Bilioni 1,512,500,000/= ambazo zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya sekta ya Elimu msingi  ambapo zimeweza kunufaisha na kujenga na kukarabati miundombinu na majengo katika shule za msingi 9 ambazo ni Shilabela, Mwabebea, Mwagiligili, Chatta, Igwata, Busegeja, Iteja, Kagera, na Nyabuhele .

Amefafanua kwamba Serikali ilitoa fedha shilingi Milioni 540.3 kujenga shule mpya ya msingi ya Shilabela pamoja na shule ya msingi Ntende kwa sasa shule ya msingi mpya ya Mwabebea ambayo pia imejengwa na kukamilika kwa shilingi Milioni 540.3 na shule za msingi 7 zilizobaki  zimefanyiwa ukarabati wa miundombinu ya majengo pamoja na nyongeza ya kujenga majengo ya madarasa na vyoo hivyo zoezi la ujenzi limefanyika vizuri na kwa ubora unaoridhisha kupitia kamati za ujenzi, manunuzi na mapokezi.

Baadhi ya Wakazi na Viongozi wa Kata ya Misungwi akiwemo Bw. Jackson Farasi pamoja na Clement Matenya wamesema kuwa hapo awali watoto walikua wakipata adha kubwa wakiwa darasani kwani iliwabidi kujazana hatimaye hali hiyo kwa sasa imetatuliwa ambapo wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kwa kuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo katika sekta zote ikiwemo elimu, Afya na Maji  na kumwomba aendelee na moyo huo ili kuwaletea maendeleo ya dhati Wananchi na kuiomba Serikali kuwezesha upatikanaji wa nishati ya umeme, huduma ya maji pamoja na kujenga uzio katika  Shule mpya ya Sekondari Mwambola ili kuwalinda watoto wa kike kuondokana na adha ya kufanyiwa ukatili na kusoma kwa utulivu.





Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.