• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Mikopo ya asilimia mbili kuwakwamua Watu wenye Ulemavu Wilayani Misungwi

Imewekwa : May 4th, 2023

Watu wenye Ulemavu watakiwa kuchangamkia fursa za Mikopo ya asilimia kumi inayotolewa katika Halmashauri nchini kwa mapato ya ndani Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Misungwi  Mhe,Petro Sabato kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Paulo Matiko Chacha, amewataka Watu wenye Ulemavu kutumia fursa za Mikopo ya asilimia 10 asilimia ambapo asilimia 2 ni ya Watu wenye ulemavu ili kujikomboa na kujikwamua kiuchumi..

Hayo yamesemwa tarehe 02/05/2023 wakati wa kikao cha kuhuisha Kamati ya Watu wenye Ulemavu ya Wilaya kilichofanyika katika  Ukumbi wa Jengo la Bima Hospitali ya Mitindo Misungwi ambapo amewataka Watu wenye ulemavu kukopa na kurejesha mikopo hiyo isiyokuwa  na riba ili kuweza kujikwamua kwa kufanya shughuli za maendeleo na  kujipatia kipato ambapo mikopo hiyo inatolewa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw.Benson Mihayo amesema kuwa Mikopo ya asilimia mbili ipo kwa ajili ya Watu wenye Ulemavu na inakopeshwa bila riba kuanzia vikundi na hata kwa mtu mmoja moja, na kutoa wito kwa Watu wenye Ulemavu kuchangamkia fursa hiyo kwa kukopa na kurejesha kwa wakati ili kuwapa nafasi wengine ya kukopa na wazitumie fedha hizo kwa manufaa yenye kuleta tija.

Naye Mwenyekiti  wa Kamati ya Watu wenye Ulemavu  Wilaya ya Misungwi Bw.Leonidas Mtawala  amesema kuwa  changamoto kubwa ambayo imekuwa ikiwakabili ni ufinyu wa bajeti na sasa suala lipata ufumbuzi na kuwafikia Watu wenye Ulemavu kuanzia ngazi ya vijiji na kupata idadi yao na kujua changamoto gani  wanazipitia na kuzifikisha sehemu husika ili kupata ufumbuzi.

Vilevile Bw.Mtawala  ameongeza kuwa kuna umuhimu mkubwa wa Watu wenye Ulemavu kupatiwa  elimu ya kutosha juu ya madhara ya kuficha watoto wenye mahitaji maalumu majumbani kwa kufanya hivyo wanawakosesha watoto hao kupata haki yao ya msingi ya elimu bora,lakini pia amesisitiza kuwa miundo ya barabara kutoka majumbani kwenda mashuleni  kwa watoto wenye ulemavu  si rafiki na jamii kutokuwa karibu na Watu wenye ulemavu bado ni changamoto kubwa,Hivyo ameiomba jamii kuwa karibu pamoja na kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha wanawabaini watu wenye ulememavu katika kaya zao.

Mratibu wa Shirika la APDM Bw.Malimi Luhanya kwa kushirikina na Shirika la SENSE International amesema kuwa kuwepo kwa Mabaraza ya Watu wenye Ulemavu ambayo yanashughulikia kero na hoja za watu wenye ulemavu kuanzia ngazi za vijiji yamekuwa mhimili mkubwa wa kuibua changamoto zinazowakabili  katika sehemu ngazi za vitongoji na vijiji na kuiomba Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kutoa vipaumbele katika bajeti kwenye mabaraza hayo ili yaweze kutekeleza majukumu yake barabara.

Bi.Jesca Boniventura Mwenyekiti wa SHEVIWATA Wilaya ya Misungwi ameeleza kuwa kuhuishwa kwa kamati hiyo italeta tija katika utendaji kazi kwa watu wenye ulemavu kwa kutoa maoni yao na changamoto zinazowakabili na njisi gani wanavyo weza kushirikishwa katika shughuli mbalimbali za kijamii zinazowazunguka na kutambulika kutoka ngazi ya chini hadi kitaifa,wakati huo huo kuiomba Serikali kuendelea kutoa elimu hasa maeneo ya vijijini kuhusina kunyanyapaliwa kwa Watu wenye Ulemavu ili kuondokana na dhana potofu iliyojengeka miongoni mwa watu na kuona watu wote wana haki sawa.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri wa Wilaya ya Misungwi Bw.Philemoni John amesema mikopo ya asilimia 10 inatolewa katika Halmashauri zote nchini bila riba na asilimia 2 ni kwa watu wenye ulemavu ambapo amewaomba kuchangamkia fursa ya mikopo kwa lengo la kuzalisha faida endelevu ili kuweza kurejesha mikopo hiyo kwa wakati na kuwa mpango mkakati wa kujikwamua sehemu moja kwenda nyingine,na ni ruksa kwa kikundi au mtu mmoja mmoja kukopa kwa watu wenye ulemavu. Bw.John amesisitiza kuwa moja ya vigezo vya Mikopo ni pamoja na uaminifu kwa mwanakikundi katika kukopa.

Baadhi ya wajumbe wa Kamati Ulinzi ya Watu wenye Ulemavu Wilayani Misungwi wakiwa katika picha ya Pamoja walipokutana katika kuzindua kamati hiyo hivi karibuni katika ukumbi wa jengo la bima  Hospitali ya Mitindo Wilayani Misungwi.

Baadhi ya ya Viongozi wa Kamati ya Ulinzi ya Watu wenye Ulemavu Wilaya ya Misungwi,aliyesimama ni M/kiti wa kamati hiyo Bw.Leonidas Mtawala,kulia kwake ni Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi, Bw.Petro Sabato na wa kwanza kushoto ni M/ki kamati ya Huduma za Kijamii na Diwani wa Kata ya Mbarika Mhe,Joel Ndogani

Viongozi wa Kamati ya Ulinzi ya Watu wenye Ulemavu Wilaya ya Misungwi,aliyesimama ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw.Benson Mihayo akiongoza mjadala huo mapema wiki hii katika Ukumbi wa Hospitali ya Mitindo wakati wa uzinduzi wa kamati hiyo.


Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.