• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Madiwani wa Misungwi waapishwa rasmi, DC awaagiza wakasimamie miradi vijijini kikamilifu

Imewekwa : December 8th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda awaagiza  Madiwani wa Halmashauri ya Misungwi kufuatilia na kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Kata na vijiji.

Mkuu wa Wilaya huyo ametoa agizo hilo mapema jana wakati wa Mkutano wa kwanza wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ambapo katika Mkutano huo ulimchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri na Madiwani hao wameapishwa rasmi kuwa Madiwani na wanapaswa kuanza majukumu yao mara moja.

Juma Sweda amewaagiza Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kuanza kazi ya kuhamasisha na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa , ujenzi wa vyoo, ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya pamoja na miradi mingine.

Amewataka kuanza kufanya vikao na Wananchi ili waweze kujadili mambo ya maendeleo na kuweka mipango mikakati ya kukamilisha ujenzi wa miradi hiyo ambayo imeanzishwa na inaendelea kutekelezwa kwa fedha za Serikali pamoja na michango na nguvu za Wananchi na kuhakikisha inatekelezwa kwa kiwango na ubora na inakamilika kwa wakati.

Amewapongeza pia Madiwani hao kwa kuaminiwa na Wananchi na kuchaguliwa kwa kishindo kuwa Madiwani na kuwaomba kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 hadi 2025 kwa kasi ili kuwaletea Wananchi maendeleo ya dhati na kuongeza kipato na kukuza uchumi wa taifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri, Kashinje Machibya amewashukuru Madiwani kwa kumchagua kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Misungwi kwa kipindi cha miaka mitano na na kueleza kwamba binafsi ataongoza na kufanya maamuzi ya pamoja kwa kushirikiana na kuwaomba watoe ushirikiano mkubwa katika kutekeleza majukumu ya kusimamia shughuli za Serikali na kwamba ana matumaini makubwa na Watendaji na Watumishi wa Halmashauri.

Kashinje Machibya ameahidi kusimamia Halmashauri na kuhakikikisha Halmashauri inapata Hati safi kwa kila mwaka kwa kufuata miongozo na sheria zilizopo na kupitia kwa Watendaji watahakikisha wanaweka mipango mizuri ya maendeleo.

Amewataka Madiwani hao kufanya kazi kwa umoja na mshikamano pamoja na matarajio makubwa ya kupewa ushirikiano mkubwa kutoka kwa Watendaji na Watumishi wa Halmashauri kwa kuzingatia sharia kanuni na taratibu za Serikali.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauriya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba amewasilisha taarifa ya shughuli za Serikali zilizotekelezwa  na Halmashauri kwa kipindi cha kuanizia  mwezi Mei hadi Novemba 2020, na kueleza kwamba shughuli hizo zimetekelezwa na Menejimenti ya Halmashauri ambapo utekelezaji wa miradi na shughuli umefanyika katika Idara na Vitengo vya sekta zote.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kashinje Machibya akizungumza katika Mkutano wa Braza la Madiwani mara baada ya kuchaguliwa kuongoza Halmashauri hiyo katika Ukumbi wa Halmashauri mapema jana.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Rahma Emmanuel Fidel akiomba kura kwa Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Misungwi kabla ya kuchaguliwa kwa kura zote 36 za ndiyo kuwa Makamu Mwenyekiti wa Hamashauri ya Misungwi.

 Mkurugenzi Mtendaji waHalmashauri ya  Wilaya ya Misungwi akiwasilisha taarifa ya utekelezaji kuanzia mwezi Mei hadi Novemba  2020 kwatika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmsahuri.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.