• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Madiwani Misungwi waridhishwa na kupongeza utekelezaji wa Miradi ya ujenzi kwa kutumia (FORCE AKAUNTI)

Imewekwa : October 30th, 2018

 Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yaridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Miradi mbalimbali inayosimamiwa vizuri na Menejimenti kwa kutumia Force Akaunti iliyojengwa kwa kiwango na ubora na kuzingatia thamani ya fedha .

Akizungumza katika Ziara ya Wajumbe wa Kamati hiyo,Makamu Mwenyekiti wa Halm ashauri Mhe,Paulo Kishinda alieleza namna alivyoridhishwa na ujenzi na kuwapongeza Waatalam wa Halmashauri kwa kuweza kusimamia kikamilifu utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo imetekelezwa kupitia Kamati za Shule,Kamati za ujenzi na manunuzi kwa ushirikiano wa Wahandisi wa Ujenzi na Kitengo cha Ugavi na Manunuzi kwa kutumia Mafundi wazawa (Local Fundis) ambao wamejenga kwa ubora na kiwango kikubwa na miradi imekidhi vigezo kulingana na thamani ya fedha iliyotumika.

Makamu Mwenyekiti,Mhe,Paulo Kishinda alisema hayo mara baada ya kutembelea na kukagua Mradi wa ujenzi wa Nyumba ya Walimu( Six in One ) iliyojengwa katika Shule ya Sekondari ya Isakamawe katika Kata ya Kijima ambayo itagharimu shillingi 141,000,000 fedha ambazo ni ufadhili wa Shirika la Elimu Tanzania zilizotolewa kwa awamu mbili ya shilingi 70,500,000 kwa kila awamu,fedha hizo zimetolewa ili kuweza kuboresha na kuleta ufanisi wa utendaji kazi kwa Walimu kwa kuwa na makazi mazuri na bora.

Akitoa maelezo kwa Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango,Kaimu Mhandisi wa Ujenzi,Revocatus Bulahya alisema kwamba ujenzi huo umefanyika kwa ushirikiano wa Waatalam wa Halmashauri pamoja na Kamati ya ujenzi ya Shule ambapo walikuwa wanafanya manunuzi ya vifaa vya ujenzi moja kwa moja Madukani na kuweka stoo na kuendelea kumsimamia Fundi ujenzi na kutoa ushauri mara kwa mara kulingana na Mkataba na kwa sasa wanaendelea na hatua ya ukamilishaji wa ujenzi huo ambapo wanatarajia kumaliza ujenzi mwezi Disemba mwaka huu.

Ujenzi wa Mashimo ya Maji machafu ya Choo yanayojengwa katika Nyumba ya Walimu Six in One Sekondari ya Isakamawe.

Kaimu Mhandisi wa ujenzi,Bulahya alieleza kuwa Fundi ujenzi anaendelea kuchimba mashimo ya maji machafu matatu,kukamilisha upigaji wa lipu na kuweka dari, vigae,vioo pamoja na kupiga rangi ndani na nje ya jengo na manunuzi ya Vifaa vya ukamilishaji yameshafanyika hivyo wataendelea kusimamia kikamilifu ili kuweza kufanya ukamilishaji bora na wenye viwango, Alisisitiza Bulahya.

Kamati hiyo iliweza pia kukagua Mradi wa ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vitatu vya Madarasa ya Wanafunzi wa Kidato cha tano na Sita katika Shule ya Sekondari Misasi kwa gharama ya shilingi 30,000,000 ambapo ukamilishaji wa ujenzi umefanyika vizuri na unaendelea kukamilika kwa kuweka Vioo na Vigae na wamejenga kwa kutumia Local Fundis na kusimamiwa na Kamati ya ujenzi ya Shule kwa kushirikiana na Waatalam wa Idara ya ujenzi,Ugavi na Manunuzi na majengo yamekamilishwa vizuri.

Vioo katika Sekondari ya Misasi

Aidha,Kamati ilikagua Mradi wa ukarabati wa majengo matano ya vyumba vya madarasa yanayoendelea kukarabatiwa katika Shule ya Sekondari Misasi kwa fedha zingine 30,000,000 zilizotolewa na Serikali kuu kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia mashuleni, ili kuweza kuinua kiwango cha ufaulu wa Wanafunzi wa Sekondari na kazi ya ukarabati huo inaendelea vizuri na ipo katika hatua ya ukamilishaji.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha na Wataalam wa Halmashauri wakisikiliza maoni na ushauri kutoka kwa Mhe,Ngwanza Nyahehe (katikati) kuhusu utekelezaji wa miradi ya ujenzi kwa kutumia mafundi Wazawa.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ,Mhe, Kishinda aliishukuru Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe,Rais Dkt, John Pombe Joseph Magufuli kwa kubuni na kuleta Mpango na Sera ya kutumia Force Akaunti katika ujenzi wa Majengo ya Serikali na kueleza kwamba imesaidia sana na kuwezesha kujenga majengo zaidi kwa gharama kidogo na kupata ziada ya fedha ambazo zitafanya kazi zingine, akitolea mfano ujenzi wa Jengo la Bima ya Afya( OPD) mradi ambao unaendelea kukamilishwa ambapo hadi sasa umegharimu fedha shilingi 141,525,250 na ujenzi umefanyika kwa kiwango kikubwa, Alifafanua Makamu Mwenyekiti,Mhe Kishinda.


Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.