• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Madiwani Misungwi wapongeza Ukusanyaji Mapato na utekelezaji Miradi kuishia Machi 2022

Imewekwa : May 23rd, 2022

Baraza la Madiwani lapongeza juhudi ya ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa robo ya tatu kuishia mwezi machi  2022 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi  uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri. Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe, Kashinje Machibya alieleza kwamba Baraza la Madiwani limepongeza na kuridhika na juhudi na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na ukusanyaji wa mapato ya ndani ambapo kuishia mwezi machi Menejimenti wameweza kukusanya  shilingi 1,803,249,490.01 = sawa na asilimia  71.45 kwa bajeti ya mwaka 2021/2022.

Mhe, Machibya amesema kwamba wametenga fedha kiasi shilingi 400,000,000/= za mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kata ya Nhundulu Kijiji cha Mwawile na fedha hizo zinakusanywa  kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ikiwa nia asilimia 40 ya kupeleka kwenye miradi ya maendeleo  na kutoa rai kwa Wananchi watoe ushirikiano na kutoa ushuru   kwa ajili ya kuongeza mapato ya ndani na kuhakikisha Halmashauri inapata mapato ya kutosha na kukamilisha miradi iliyopangwa.

Akizungumza katika Baraza la Madiwani Mhe, Machibya ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha kwa ajili utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ikiwemo vituo vya Afya pamoja na ujenzi wa madarasa.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Misungwi Bw. Benson Mihayo amesema kwamba Menejimenti itaendelea kukusanya mapato kwa bidii ili kufikia malengo waliojiwekea katika Halmashauri ili kuendelea kutatua changamoto za Wananchi kwa kuwaletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Bw. Benson Mihayo  amesema kwamba Halmashauri katika kipndi cha kuishia mwezi Machi 2022 imeweza kukusanya kiasi cha shilingi 1,803,249,490.01 kutoka katika vyanzo vya ndani vya mapato  sawa na asilimia 71.45 na kusisitiza kwamba Menejimenti  wamejiwekea mikakati ya kuendelea kukusanya mapato na kuundwa kwa timu  mbili za ukusanyaji mapato ambazo zimeanza na Kata ya Usagara na Kata ya Misungwi na zoezi linaendelea vizuri kwa asilimia 84 na kutoa wito kwa Watendaji wa Kata pamoja na Waheshimiwa Madiwani wawe mabalozi katika ukusanyaji wa mapato na kuelimisha wananchi umuhimu wa mapato.

Alifafanua kuwa fedha zinazoletwa na Serikali ni lazima zisimamiwe vizuri pamoja na miradi iliyopo ili iweze kuwaletea maendeleo Wananchi pasipo kuwa na upotevu wa fedha,na kuwaelimisha wananchi juu ya matumizi ya  fedha ambazo Serikali inaendelea kuzitoa ni kwa ajili maslahi ya Taifa.

Wakati huo huo Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Misungwi Bw.Mohamed Ally Chorage alisisitiza Madiwani wahakikishe wanasimamia fedha zote za miradi kwenye maeneo yao ili ziweze kuleta maendeleo kwa wananchi aidha aliwataka  Waheshimiwa Madiwani kuhakiksha wanatimiza majukumu yao na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa manufaa ya Wananchi kwa ujumla,

Pia alisisitiza kuwa ni vizuri jambo lolote la kimaendeleo linapoenda kufanyika  kwenye eneo husika ni muhimu Diwani apewe taarifa ili kutoa ushirikiano na kusikiliza changamoto za wananchi katika eneo lake.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Misasi Mhe, Daniel  Busalu ameishukuru Serikali ya awamu sita kwa kuendelea kuleta fedha za miradi hususan  sekta ya Elimu pamoja na miradi ya  sekta ya maji inayoiendelea kutekelezwa na tayari fedha zipo zaidi ya bilioni 50, kwa ajili ya kutatua changamoto ya maji ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kutekeleza miradi ya Maji katika maeneo ya  Kata ya Ukiriguru, Bulemeji,  na Nyanghomango na Nyamayinza.

 Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi wakiendelea kusikiliza mjadala na hoja mbalimbali katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Halmashauri hiyo



Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.