• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Madiwani Misungwi wachachamaa "waagiza miradi ya ujenzi wa Machinjio ya Nyamatala na Fella kufanyiwa marekebisho kwa kuzingatia ramani halisi ya Machinjio."

Imewekwa : February 15th, 2020

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza yaagiza Kamati ya ujenzi kufanya marekebisho mapema katika ujenzi wa machinjio ya Fella na Nyamatala zinazojengwa katika Kata ya Fella na Igokelo Wilayani humo. 

Agizo hilo limetolewa katika ziara ya Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango iliyofanyika hivi karibuni kwa lengo la kukagua na kuona utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, ambapo ujenzi wa machinjio hizo zinazogharimu zaidi ya shilingi 30,000,000/=  ni miongoni mwa miradi ilyotembelewa na Wajumbe wa kamati hiyo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Antony Bahebe amesema kwamba ujenzi wa miradi hiyo haukuzingatia vigezo na kufuata ramani ya majengo ya machinjio sambasamba na usimamizi mbovu wa Wataalam na Kamati ya ujenzi ya vijiji husika, hivyo kusababisha baadhi ya maeneo kutokujengwa vizuri na mengine kuwekwa kinyume na ramani za machinjio zinavyoelekeza.

“ Kwa kuzingatia ramani za ujenzi wa machinjio za Wizara, naona kuna baadhi ya maeneo hayakuzingatiwa katika ujenzi huu, mfano uwekaji wa Tarazo pamoja na Hooks ambapo Mifugo atanaswa wakati wa kuchinjwa, lakini pia mabomba yamewekwa pembeni na nje ya mtaro wa kutiririsha damu baada ya mifugo kuchinjwa na kutundikwa juu,” alieleza kwa msisitizo zaidi Mwenyekiti wa Hamashauri. 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Antony Bahebe Masele ( kulia) akiongoza Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango katika ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika ziara ya ukaguzi wa miradi kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2019/2020, ambapo wameweza kukagua zaidi ya miradi tisa katika vijiji vya Wilaya ya Misungwi,

Wajumbe wa Kamati ya Fedha walishangazwa na hali ya maendeleo katika ujenzi wa machinjio hayo ya Fella na Nyamatala na kuhoji namna Kamati ya ujenzi pamoja na Wataalam wa Halmashauri walivyoshiriki kusimamia ujenzi huo na kueleza kwamba ni muhimu miradi yote itekelezwe na kusimamiwa kikamilifu kwa kuzingatia ramani na maelekezo kutoka kwa Mhandisi wa ujenzi ili kuwa na majengo yenye ubora na kiwango kinachoridhisha na kuwaomba kujenga uzio katika machinjio ya Nyamatala..

Mhe, Antony Bahebe aliwataka Wataalam pamoja na Kamati ya ujenzi ya Vijiji hivyo vya Nyamatala na Fella  kuhakikisha wanasimamia na kukamilisha marekebisho yote ambayo yamebainishwa na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ili kuweza kukabidhiwa miradi hiyo na mafundi ujenzi na kuanza kutumika na ameshauri viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Fella kuwa na mpango mkakati wa kuweka na kuimarisha ulinzi katika eneo la machinjio hayo na kuitunza iweze kudumu.

Akitoa maelezo kwa Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango, Afisa Mipango Wilaya, Bi, Anna Urio  alisema kwamba ujenzi huo wa Machinjio zote  umefanyika kwa ushirikiano wa Waatalam wa Halmashauri pamoja na Kamati ya ujenzi ambapo Idara ya Mipango walikuwa wanafanya  ukaguzi na kushauri Kamati ya ujenzi kufanya marekebisho katika maeneo yaaliyoonekana na mapungufu  hususani katika machinjio ya Nyamatala wameweza kuzuia malipo ya Fundi ujenzi  yenye shilingi 1,400,000/=  na kueleza kuwa zitalipwa mara baada ya Fundi huyo kukamilisha marekebisho aliyoagizwa na Menejimenti.

Bi, Anna Urio ameongeza kwamba Menejimenti kwa ujumla imepokea changamoto zote na itahakikisha zinashughulikiwa na kutekelezwa kikamilifu na kwa wakati ikiwa ni pamoja na kufanya marekebisho katika maeneo yaliyobainishwa kwa kutumia Fedha zilizopo ambazo zililenga kujenga na kukamilisha machinjio hayo kutokana na mchoro na ramani iliyokuwepo na kuhakikisha ujenzi wa machinjio hayo ya Nyamatala na Fella yanakamilika vizuri na kuanza kutoa huduma kwa Wananchi kama ilivyokusudiwa.

Kamati ya Fedha  katika ziara hiyo imeweza kutembelea na kukagua zaidi ya miradi mingine nane ya maendeleo inayotekelezwa kwa fedha za Serikali  kuu , Mapato ya ndani ya Halmashauri na Michango ya Wahisani na nguvu za Wananchi ambayo ni pamoja na Mradi wa Ujenzi wa Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Misungwi wenye shilingi 158,000,000/=, Ukamilishai wa darasa shule ya Msingi Chata kwa shilingi 12,500,000/=,Mradi wa Ujenzi wa Wodi ya Wazazi katika Kituo cha Afya Mbarika kwa shilingi 152,000,000/=, Ujenzi wa Mradi wa Kitalu Nyumba kwa shilingi 15,850,000/=, U Mradi wa Ukarabati wa Jengo la Soko la Madini kwa shilingi 27,500,000/=, 

Miradi mingine ni pamoja na Ujenzi wa mradi wa Jengo la ofisi za Halmashauri wenye shilingi 1,000,000,000/=, Mradi wa Ujenzi wa Maabara ya Kemia na Biolojia Shule ya Sekondari Idetemya kwa shilingi 157,187,744/= na Ujenzi wa vyumba vitatu vya Madarasa katika Shule ya Sekondari J. Magufuli kwa nguvu za Wananchi na miradi yote imekamilika kwa zaidi ya asilimia 90.

Jengo la Maabara ya Kemia na Biolojia lilojengwa na Wahisani katika Shule ya Sekondari Idetemya,ujenzi huo wa Maabara hayo umegaharimu kiasi cha shilingi Milioni 157 hadi kukamilika

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.