• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Mabalozi wa Jinsia na Lishe,Wataalamu wapatiwa Mafunzo usindikaji Maziwa misungwi

Imewekwa : March 27th, 2024

Mabalozi wa Jinsia na Lishe na Wataalam wa Sekta ya Mifugo na maendeleo ya jamii wapatiwa mafunzo ya namna ya kuongeza  ufanisi wa Usindikaji na Uzalishaji wa Maziwa Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Mafunzo hayo yametolewa leo 27, Machi, 2024 na Mratibu wa Kitengo cha Jinsia Lishe Shirika la Heifer International Bi.Nyamate Msobi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Halamshauri ya Wilaya ya Misungwi ambayo yalihusisha kuwajengea uwezo maafisa mifugo, Maafisa ushirika ,Maendeleo ya Jamii,Lishe na Mabalozi kwa lengo la kutambua namna bora ya ukuanyaji maziwa kupitia uboreshaji wa miundombinu ya kukusanyia maziwa na kuongeza tija katika uzalishaji wa maziwa.

Amesema kuwa mafunzo hayo ambayo wameyapata washiriki yatasaidia kuongeza uelewa wa juu ya dhana za kijinsia na jinsi zinazohusiana na maendeleo,na kuona umuhimu wa jinsia katika Maisha ya kila siku ya ufugaji na kutambua mwuafaka wa kijinsia katika kuboresha ushiriki wa wanawake katika maamuzi ngazi ya kaya na jamii kwa ujumla.

Bi.Nyamate ameeleza kwamba ushirikishwaji wa Wanawake katika jamii utawezesha kuongeza kufanya maamuzi katika kipato cha familia, kushiriki katika maamuzi ya kuongeza uzalishaji wa maziwa katika ngazi ya kaya pamoja kuongeza wigo wa wanawake kupata fursa za kiuchumi na kuongeza ushiriki wa wanawake na wanaume katika majukumu mbalimbali na hivyo kuchangia uwepo wa uhakika wa chakula katika kaya na jamii.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamiii Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza Bi. Janeth Shishila amesema kuwa mafunzo walioyapata yakawe chachu ya kuleta mabadiliko ya kifikra katika jamii zinazowazunguka kwa kuwaelimisha na kuwawezesha wanawake kupata fursa sawa kama wanaume katika kuzalisha uzalishaji na hivyo kupunguza njaa katika jamii.

Bi.Shishila ameongeza kuwa kwa kuzingatia umuhimu wa kujumuisha masuala jinsia na lishe  kwa  wanawake na wanaume itasaidia uhakika wa chakula na lishe na kuongeza upatikanaji wa rasilimali miongoni mwa wanawake ,hivyo kupelekea kuboresha lishe  na afya ya familia.

Naye Kaimu Afisa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw. Johnbosco Nkunguu ametoa wito kwa Wataalamu wa Mifugo na Mabalozi wa jinsia na Lishe kuendelea kutoa mafunzo kwa vikundi walivyoviunda,wasikate tamaa  katika kuwaelekeza vikundi vya wafugaji na kuwataka kundelea kuwajengea uwezo na kuwapa moyo pindi taratibu zitakapo kamilika na kukidhi vigezo watapewa mkopo wa ng’ombe wa maziwa.

Mradi Shirikishi wa Wasindikaji na Wazalishaji wa maziwa Tanzania (TI3P) umeendelea kutoa mafunzo ya Jinsia na Lishe katika ngazi ya jamii ili kuleta mabadiliko chanya katika sekta ndogo ya maziwa kupitia uhamasishaji wa uwekezaji kutoka sekta ya umma na binafsi kwa lengo kuongeza tija katika uzalishaji wa maziwa, ikiwa kauli mbiu ni” Maziwa maziwa dhahabu nyeupe,maziwa salama chakula na fedha”

Washiriki mbalimbali wakifuatilia kwa makini kikao cha mafunzo kutoka Mradi Shirikishi wa Wasindikaji,Wazalishaji wa Maziwa Tanzania kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri leo mapema ambapo wadau pamoja na wataalamu waliweza  wapatiwa mafunzo ya namna ya kuongeza  ufanisi wa Usindikaji na Uzalishaji wa Maziwa.

Mratibu wa Kitengo cha Jinsia Lishe Shirika la Heifer International Bi.Nyamate Msobi akitoa mafuzo leo ya namna ya kuongeza ufanisi wa usindikaji na uzalishaji wa maziwa katika ukumbi wa Halmasahuri ya Wilaya ya Misungwi.


Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.