• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Kaya Maskini 1,976 za Vijiji 60 zatakiwa kukamilisha uhakiki wa Walengwa wa TASAF Wilayani Misungwi.

Imewekwa : November 30th, 2020

Walengwa 1,976 wa Kaya maskini  wametakiwa kujitokeza kuhakiki katika mfumo mpya wa matumizi ya Vishikwambi  kwa ajili ya kukidhi na kupata vigezo vya kupokea malipo ya ruzuku ya fedha zinazotokana na mpango wa TASAF awamu ya tatu kipengele cha pili katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Hayo yamebainika na kuelezwa mapema leo katika mafunzo ya siku moja, yaliyofanyika katika Ukumbi wa MGS Hoteli –Misungwi  kwa ajili ya kuwawezesha Wawezeshaji  33 wa ngazi ya Wilaya ambao wanatakiwa kufanya uhakiki wa walengwa wote waliopo katika Kaya hizo maskini 1,976 kwa kuzingatia masharti na vigezo na sifa zilizowekwa kwa Kaya zinazotakiwa kupata fedha za ruzuku kulingana na hali na maisha yao.

Akizungumza na Wawezeshaji wakati wa mafunzo hayo, Afisa mafunzo wa Mpango wa kunusuru Kaya maskini TASAF Makao makuu, Bi. Catherine Kisanga alisema mafunzo hayo ni kwa ajili ya maandalizi ya kwenda kuanza  zoezi la siku mbili la  la uhakiki wa Kaya maskini 1,724 ambazo hazikuhakikiwa awali  pamoja na Kaya 252 ambazo zilikuwa zimesimamishiwa malipo mwanzoni, kutokana na sababu hizo hivyo katika zoezi hili la uhakiki huu wa awamu ya pili  ni matarajio ya kuhakiki Kaya maskini 1,976  katika vijiji vya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi zilizobaki katika uhakiki wa kaya katika mpango wa TASAF awamu ya tatu kipengele cha pili..

Bi. Kisanga amewataka Wawezeshaji wa  ngazi ya Wilaya kuhakiki kwa umakini Kaya maskini za Walengwa wa mpango wa TASAF Wilaya ya Misungwi  ili kupata taarifa sahihi za walengwa, kuhakikisha wanatumia mbinu mbadala  na za kisasa za kufanya kazi na Jamii ambayo ina Wananchi tofauti na wenye uelewa, fikra na mawazo tofauti tofauti na kuhakikisha wanapata taarifa za kweli na kuwa waaminifu na waadilifu katika ujazaji wa takwimu na taarifa za walengwa wa kila Kaya maskini.

Bi. Kisanga amewataka wawezeshaji hao kutumia kikamilifu na kwa uaminifu mkubwa Vishikwambi ambavyo vimeleta tija ya kufanya kazi kwa weledi na kutoa taarifa na takwimu za walengwa wa Kaya kwa usahihi

"Ili kupata takwimu sahihi amewataka wawezeshaji hao wa mpango huo kufanya kazi kwa weledi na kufuata sheria ikiwa kila mmoja amekula kiapo cha kufanya kazi kwa kufuata sheria na nitoe rai tu kwamba kila mlengwa apatiwe huduma bora na niwatake mtumie lugha nzuri kwa walengwa na hata wale waliotolewa kwenye mpango huu muwaeleweshwe  na kuwaelekeza kwa lugha nzuri na yenye staha ". Bi. Kisanga  ameeleza na kuwasihi Wawezeshaji hao.

Naye Afisa ufuatiliaji wa TASAF III Wilaya ya Misungwi Steven Samwel alisema  kwamba katika uhakiki huu wa walengwa utafanyika katika vijiji 60 tu vilivyokuwa vinapata fedha za ruzuku ya awali  na kwamba zoezi hili litakapokamilika na kama kuna mlengwa wa Kaya maskini ambaye hataweza kujitokeza basi atakuwa amejiondoa mwenyewe  na kupoteza sifa na  fursa katika mpango wa kupata fedha za kujikimu za mpango huu.

Bw. Steven Samwel amefafanua zaidi kwamba maboresho yaliyofanyika katika uhakiki wa kaya hizi ni pamoja na mabadiliko ya maeneo ya kiutawala ikiwa ni pamoja na kijiji kilichoanzishwa upya na  kijiji kingine basi kila kimoja kitajitegemea pamoja na kuwapatia taarifa kila kaya ili kurahisisha kukamilika kwa wakati zoezi hili.

Afisa Ufuatiliaji wa Mpango wa kunusuru Kaya maskini TASAF Wilaya ya Misungwi, ameongeza kwamba katika uhakiki wa awali Kaya za Walengwa 6,843 zilihakikiwa na baadae Kaya maskini 6,764 zilipatiwa na kupokea mgawo wa fedha za malipo ya mwezi Julai hadi  Oktoba mwaka huu 2020 kiasi cha shilingi 269,612,000/= kwa awamu mbili ambazo ni sawa na shilingi 539,224,000/= 

Kwa upande wake Mratibu msaidizi wa Mpango wa kunusuru Kaya maskini TASAF III wa Wilaya ya Misungwi Bi. Abigaeli Gimbagu  alipohojiwa na Timu ya Habari, alifafanua kwamba awali kulikuwa na changamoto kwa baadhi ya walengwa kutoonekana kwenye eneo la tukio na baada ya kufuatilia tulipata sababu kuwa ni wagonjwa, wengine wapo safarini, na changamoto mbalimbali za kifamilia hivyo zoezi halikukamilika kutokana na kutowafikia walengwa zaidi ya  Kaya 8,567 zilizokuwepo awali  hivyo sasa tunaenda kwenye uhakiki wa mwisho kumalizia idadi ya walengwa ambao walikosa huduma hiyo kipindi kilichopita ambao ni kaya maskini zipatazo 1,976..

Mwezeshaji wa ngazi ya Wilaya , Bw. Lucal Nonga alibainisha na kueleza vikwazo na  changamoto.iliyosababisha kutofanikiwa kumaliza zoezi  la uhakiki kipindi kilichopita ni  pamoja na watu kutokujitokeza  kuhakiki kwa wakati na pia kuwatuma watu wasio na Vitammbulisho halisi vya uraia na mpiga kura na kusababsha kutomalizika kwa walengwa ila kwa sasa tutamaliza kutokana na elimu tuliyopatiwa imetuongezea tija ya kwenda kufabya kazi kwa weledi zaidi.

"Kupitia vishikwambi sasa mtu mmoja anaweza kuhakiki idadi ya watu 200 kwa siku na moja kwa moja ataingia kwenye mfumo rasmi wa uhakiki  kwa njia mpya ya Teknolojia na kupunguza muda wa kufanya kazi kwani vinasaidia kuboresha taarifa  sahihi na kwa wakati husika". Alieleza kwa msisitizo Mwezeshaji Nonga. 


Baadhi ya Wawezeshaji wa ngazi ya Wilaya wakiendelea kupata mafunzo ya Mpango wa TASAF kwa ajili ya uhakiki wa Kaya maskini Wilayani Misungwi

 

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.