• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Kata ya Mondo yaibuka Kidedea yaongoza kwenye Sekta ya Kilimo na Elimu Wilayani

Imewekwa : October 9th, 2018


Kata ya Mondo katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza yaibuka Kidedea kwa kuongoza katika ushindi wa mafanikio kupitia Sekta ya Elimu na Kilimo cha Zao la Pamba kwa mwaka huu 2018.

Hayo yamebainishwa katika Ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi,Mhe,Juma Sweda wakati  akizungumza na Wananchi wa Kata ya Mondo kwenye  Mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Mwaniko, ambapo kwa mujibu wa taarifa ya mafanikio ya Kilimo cha Pamba iliyotolewa na Mkaguzi wa Pamba wa Wilaya ya Misungwi, Bw,Azalia Sanga alisema kwamba katika msimu wa mwaka 2017/2018 Wakulima waliweza kulima na kuzalisha tani 2013 za Pamba ambapo kwa msimu wa mwaka 2016/2017 wakulima walizalisha tani 1040.

Mkaguzi wa Bodi ya Pamba wa Wilaya ya Misungwi,Bw,Azalia Sanga kwa niaba ya Afisa Kilimo.Ushirika na Umwagiliaji, Bw, Majid Kabyemela aliwasilisha taarifa ya mchakato wa kumpata Mkulima Bora kwa  msimu wa mwaka 2017/2018 na kueleza kuwa mchakato huo ulianza mara moja mwezi Februari 2018 kwa kutumia Vikosi kazi vya Vijiji, na Kata na kuhitimishwa na timu ya Wataalam kutoka ngazi ya Wilaya ambayo ilichuja majina ya Wakulima 12 na kubaini Wakulima watano waliofanya vizuri zaidi na kulima kwa tija kwa kila Ekari ambapo mshindi bora Bw, Swalala Charles Nteminyanda mkazi wa Maganzo Kata ya Mondo aliibuka kidedea kwa kupata asilimia 98 kwa kuvuna Kilogramu 725 kwa Ekari.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi,Mhe,Juma Sweda amemkabidhi Zawadi ya Pikipiki na kumpongeza Mkulima huyo bora wa Pamba kutoka Kata ya Mondo kwa kulima kisasa na kwa tija na kumwomba aendelee na kuongeza bidii zaidi katika msimu huu wa 2018/2019, amewataka pia Wakulima wengine Wilayani Misungwi kuiga mfano huo wa kufufua na kuendeleza zao la Pamba ili kuweza kuinua na kukuza uchumi wa Wananchi Wilayani humu na taifa kwa ujumla.

Mkulima bora wa msimu wa 2018 Bw, Swalala Charles Nteminyanda akifurahi mara baada ya kukabidhiwa Zawadi ya Pikipiki na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi,Juma Sweda (Kulia)

Mhe,Juma Sweda awali katika Ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo aliridhishwa na utekelezaji wa miradi katika Kata ya Mondo na Mwaniko na kuwapongeza Viongozi na Wananchi wa maeneo hayo kwa kujitoa kuchangia na kusimamia kikamilifu shughuli za miradi, ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kufuatilia na kutoa fedha za mapato ya ndani  kwa ajili ya ukamilishaji wa Majengo ya madarasa katika Shule ya Msingi Nyasato ili Wanafunzi waweze kuhamia na kuanza kusoma Shuleni hapo mapema mwaka 2019 pamoja na kutenga bajeti ya fedha za mapato ya ndani kuwezesha ujenzi wa Majengo ya Kituo cha Afya cha Mondo kinachoendelea kujengwa kwa michango na nguvu za Wananchi.

Jengo la vyumba viwili vya Madarasa vilivyojengwa kwa nguvu za Wananchi hadi hatua ya boma katika Shule mpya ya Nyasato,ujenzi huu unahitaji fedha kwa ajili ya ukamilishaji

 Mhe Sweda amewapongeza pia Viongozi wa Kata ya Mondo na Mwaniko na uongozi wa Shule ya Sekondari Mwaniko kwa kuongoza kiwilaya kwa kuwa wa Kwanza kati ya Shule za  Sekondari 23  kwa kufaulu  kuanzia daraja la Pili hadi  daraja la Nne katika Mitihani ya Kidato cha Nne mwaka 2017/2018 na kupata nafasi ya 31 kimkoa, na kuwataka kuendeleza ufaulu huo na kuinua kiwango na kuimarisha Sekta ya Elimu Wilayani na nchi nzima.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.