• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Kamati ya Siasa Wilaya yaridhishwa na kupongeza Viongozi na Watendaji kwa usimamizi wa Utekelezaji Miradi Misungwi

Imewekwa : February 25th, 2025

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilayani Misungwi yaridhishwa na kupongeza utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kupitia fedha za Serikali kuu, Wafadhali na mapato ya ndani kwa mwaka 2024/2025 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Akizungumza katika ziara ya siku mbili ya Kamati ya Siasa ya kutembelea, kukagua na kuona miradi ya maendeleo Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Misungwi Bw. Mwita Nyaingi Nyarukururu amesema kwamba miradi mingi ni mizuri na imetekelezwa kwa kiwango na ubora na kuwapongezi Viongozi wa ngazi ya Wilaya na Watendaji wote wa Serikali kwa utekelezaji na usimamizi mzuri ambapo miradi inaendelea vizuri na mabadiliko ni makubwa sana katika miradi ya sekta zote za Afya, Elimu, Maji, barabara, na Sekta ya maendeleo ya jamii na kuwataka Viongozi wa Serikali kuhakikisha wanatatua na kuondoa changamoto ndogo ndogo zinazojitokeza katika baadhi ya miradi michache ili kuongeza ustawi na kuwaletea Wananchi maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya kwa ujumla wamepongeza shughuli za ujenzi wa  miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Wilayani Misungwi wameeleza  kwamba Wananchi wa Wilaya ya Misungwi wanashauku na kiu kubwa ya kuona huduma za kijamii zinaboreshwa na wananufaika na miradi inayojengwa kupitia usimamizi wa Viongozi na Watendaji wa Serikali na kuwasihi kuendelea kutekeleza miradi kwa weledi ,uadilifu na kuhakikisha inakamilika kwa ubora na kwa wakati.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Johari Samizi ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya  Misungwi amempongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za kutekeleza miradi ambapo Watendaji wameendelea kutekeleza kwa kuzingatia taratibu, sharia na kanuni na kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kwa viwango na kuwataka Wananchi wote kuunga juhudi za Serikali ya awamu ya sita.

Kwa upande wake Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Misungwi Bw. Leonidas Kondela ameeleza kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuwapongeza Viongozi wote Serikali pamoja na Watendaji kwa juhudi wanazofanya katika kutekeleza miradi kupitia fedha za awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kuwaomba Wananchi waendelee kuumunga mkono Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kwaletea maendeleo ya dhati Watanzania.

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Misungwi katika ziara hiyo imeambatana na Wakuu wa taasisi za Umma, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Halmashauri  na imetembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo katika shule za msingi na Sekondari , ujenzi wa Nyumba za Watumishi, ujenzi wa miundombinu katika Zahanati na Vituo vya Afya, ujenzi wa Madaraja na matengenezo ya barabara, ujenzi wa miradi ya Maji ya bomba na Visima, ujenzi wa Mabweni ya Wasichana unaoendelea katika Shule ya Sekondari Misungwi na Mbarika, pamoja na ujenzi wa Jengo la Mahabusu ya Watoto Bukumbi.




Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.