• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Kamati ya Rufani yafanya kikao Wilayani Misungwi

Imewekwa : November 4th, 2024

Katibu Tawala na Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani Wilaya ya Misungwi Bw. Abdi Makange ametoa rai kwa  Wananchi na vyama vya siasa kuzingatia umuhimu wa kusoma kanuni za Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa ngazi ya Vijiji na Vitongoji katika Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Rufani ya Uchaguzi wa Serikali za mitaa kilichofanyika katika ofisi ya Katibu Tawala  Wilaya Bw. Abdi Makange amesema kuwa  Kamati hiyo ina jukumu la kutenda haki na kuhakikisha kwamba malalamiko yoyote yanayojitokeza yanashughulikiwa kwa mujibu wa kanuni na miongozo ya uchaguzi, hii ni muhimu sana ili kujenga imani miongoni mwa Wananchi kuhusu mchakato wa Uchaguzi na matokeo yake ambapo elimu kuhusu kanuni za Uchaguzi inapaswa kutolewa kwa Wananchi ili waweze kuelewa haki zao na wajibu wao katika uchaguzi utakaofanyika mwaka huu Novemba 27, 2024.

"ni wajibu wao kuelimisha wanachama wao kuhusu kanuni za uchaguzi na kuhimiza ushirikiano na Kamati za Uchaguzi katika ngazi zote, hii itasaidia kupunguza migogoro na malalamiko ambayo mara nyingi yanajitokeza wakati wa Uchaguzi, alihimiza kuongeza ushirikiano na Wananchi na vyama vya siasa, Kamati hiyo itahakikisha kuwa Uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu" Amesema Bw. Abdi Makange

Bw. Makange amewataka Wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi, wakijua kuwa sauti zao zina thamani na zinachangia katika maendeleo ya jamii zao alisisitiza kuwa, ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha kuwa Uchaguzi unafanyika kwa  haki na uwazi, ili kuleta maendeleo endelevu katika Wilaya ya Misungwi.

Naye Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ngazi ya Wilaya, kwa niaba ya Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Misungwi Bw. Stephen Singira, ameeleza  umuhimu wa Kamati ya Rufani katika mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za mitaa ambapo Kamati hiyo inatarajia kupokea mapingamizi yote yanayohusiana na Wagombea wa nafasi mbalimbali, na kwamba itazingatia miongozo iliyowekwa ili kutoa suluhu sahihi, ameongeza kuwa lengo la Kamati hiyo ni kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika kwa uwazi na haki, ili kuimarisha amani miongoni mwa jamii na Wananchi katika uchaguzi.

Bw. Singira alitoa wito kwa vyama vya siasa kuzingatia na kusoma kwa makini kanuni za uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa, hususan ngazi ya vijiji na vitongoji, ameeleza kuwa uelewa mzuri wa kanuni hizo utasaidia kupunguza migogoro na malalamiko wakati wa uchaguzi, na hivyo kuimarisha demokrasia katika ngazi za chini za utawala. Kamati ya Rufani inatarajia kufanya kazi kwa karibu na wadau wote ili kuhakikisha uchaguzi unakuwa wa amani na utulivu.

Naye Afisa uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Bw. Dickson Kawovela, ameeleza kuwa mgombea anaweza kupata haki zake kupitia Sheria za Serikali za mitaa, hususan kifungu cha 15 na 16 cha sheria ya Serikali za mitaa (mamlaka za wilaya) sura ya 287 na 288. Kifungu cha 15 kinataja sifa zinazotakiwa kwa mgombea, ikiwa ni pamoja na kuwa na uraia wa Tanzania, umri wa kutosha, na kuwa na elimu inayotakiwa ambapo kifungu cha 16 kinabainisha sababu ambazo zinaweza kumfanya mgombea kupoteza sifa yake, kama vile kutokuwa na sifa zilizotajwa katika kifungu cha 15 cha sheria hiyo..

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Rufani wamesema kuwa ni umuhimu wa kufuata sheria hizi ili kuhakikisha kuwa uchaguzi unakuwa wa haki na uwazi ambapo  ni jukumu la kila mgombea kujihakikishia kuwa anatimiza sifa zote zilizotajwa ili kuepuka matatizo yanayoweza kujitokeza wakati wa mchakato wa uchaguzi ambapo  wagombea wanapaswa kuzingatia sheria hizi ili kulinda haki zao na kuhakikisha kuwa wanashiriki katika uchaguzi kwa njia sahihi.

Kauli mbiu ya Uchaguzi wa Serikali za mitaa Mwaka huu 2024 inasema kuwa “Serikali za Mitaa Sauti ya Wananchi,  Jitokeze kushiriki Uchaguzi Novemba 27, 2024”.


Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.