• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yaridhishwa na kasi Miradi Wilayani Misungwi

Imewekwa : October 24th, 2022

 Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mkaoani Mwanza yaridhishwa na Miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na kusimamiwa na Menejimenti kwa kutumia Mapato ya ndani pamoja na mapato kutoka  Serikali kuu.

Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango imefanya ziara ya kukagua miradi ya kipindi cha robo ya kwanza kwa Mwaka wa fedha 2022/2023 mwezi Julai –Septemba ambapo imekagua mradi wa ujenzi wa matundu ya vyoo 24 katika shule ya Msingi Buganda,Ujenzi wa Manawa Sekondari,Ujenzi wa mradi shule ya sekondari Mwanangwa,Mradi wa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi,Mradi wa kituo cha Afya Usagara,Mradi wa kituo cha Afya Fela na Mradi wa kituo cha Afya Koromije.

Akizungumza katika ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe, Kashinje Machibya amepongeza Menejimenti na Watendaji kwa kusimamia kikamilifu miradi hiyo ya maendeleo ambayo imetekelezwa na inaendelea kutekelezwa kwa fedha za Serikali, wafadhili na michango ya Wananchi.

Mhe, Machibya amesema kwamba kiujumla miradi imetekelezwa kwa kiwango na ubora na thamani ya fedha inaonekana ambapo katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi iliyopo Kata ya Misungwi ipo katika hatua ya kuridhisha ambapo   majengo manne yapo katika hatua ya ukamilishwaji ambalo ni jengo la Upasuaji,jengo la Upasuji la Wanaume na Wanawake pamoja na jengo la Mochwari.

Aidha Mhe, Machibwa amesema mradi wa ujenzi huo utakamilika mwishoni wa Mwezi wa 11,2022 Mwaka huu na kuwataka wahandisi wanaosimamia ujenzi wa Hospital hiyo kuzingatia vigezo na ushauri vilivyowekwa na kitaalamu na siyo vinginevyo na kuwataka kuwa wazalendo kwa kufanya kazi kwa weledi.

Bw,Machibya amesema Ujenzi wa majengo hayo utakapokamilika utasidia Wananchi kupata huduma ya Upasuaji kwa wakati na kwa ufanisi mkubwa pindi watakapofika Hospitalini hapo kupata huduma hiyo.

Mhe, Machibya amesema kwa ujenzia unaendelea katika Shule ya Sekondari Manawa uko katika hatua nzuri na inaridhisha na ametoa rai kwa watendaji kuongeza kasi ya ukamilishaji wa vyumba 4  vya madarasa katika  shule hiyo ili kufikia Januari 2023 wanafunzi waanze masomo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uongozi Mhe,Joel Dogani diwani wa Mbarika alimtaka  muwekezaji aliyenunua mlima kwa shilingi milioni 80  eneo la zahanati ya fela iliyopo kata ya Fela kuleta nyaraka za mkataba kwa mkurugenzi na kujiridhisha na kuona kama ilizingatia kanuni na utaratibu .  

Katika ziara hiyo Wajumbe wa Kamati kupitia Mwenyekiti wao wamempongeza mkurugenzi wa Halimashauri ya Wiaya ya Misungwi kwa namna anavyoshiriki kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za miradi ya maendeleo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri wa Wilaya ya Misungwi Bw,Benson Mihayo amepokea pongezi hizo na ameziomba Kamati hizo zinazosimamia miradi kuwa makini na matumizi ya fedha na Serikali kutekeleza shughuli mbalimbali za miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya Bw,Clement Morabu ametoa shukrani za pekee kwa Serikali ya awamu sita kwa kuleta mashine ya Upasuaji katika Hospitali hiyo,ambapo amsema pindi itakapoanza kutumika itahudumia Wananchi kwa kiwango kikubwa na itarahisisha kuwasogezea huduma kwa ukaribu Zaidi.

Ziara ya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya robo ya mwaka wa fedha hufanyika kila baada ya robo ya kwanza kukamilika Julai hadi Septemba mwaka 2022/2023 na hii ni ziara ya robo ya kwanza ikiwa lengo kukagua, kushauri na kubaini changamoto na kuzitafutia suluhisho.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango wakiendelea na ziara ya ukaguzi  katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi ili kubaini changamoto na kuzitafutia ufumbuzi .

Baadhi ya Wajumbe wakiwa kwenye ziara ya kukugua miradi mbalimbali ya Maendeleo,wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mhe,Kashinje Machibya akitoa maelekezo kwa wataalamu katika mradi wa ujenzi wa Sekondari Mwanangwa leo mapema.


Moja ya mashine ya kisasa Upasuaji katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi ambapo Mradi  huo pindi utakapokamilika mashine itasaidia kutoa huduma kwa Wananchi wa Wilaya ya Misungwi pamoja  na maeneo ya jirani.

Mwonekano wa Majengo ya vyumba vya madarasa ya Shule ya Sekondari Manawa iliyopo Kata ya Misasi  ambapo yapo katika hatua ya ukamilishwaji,Shule hiyo inataraji kupokea Wanafunzi Januari 2023.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.