• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DED Misungwi akasirishwa na baadhi ya Vitendo vya Watumishi Kutoa na Kupokea rushwa Misungwi

Imewekwa : February 24th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi awataka watumishi wa umma kuacha tabia ya kutoa na kupokea rushwa katika kutekeleza Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa na Serikali Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Wito huo umetolewa tarehe 24, Februari,2024 na Mkuregenzi wa Halmashauri Wilaya ya Misungwi Bw.Joseph Mafuru wakati wa ziara ya ukaguzi wa Miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa  katika Kata ya Mbarika Wilaya ya Misungwi.

Bw. Mafuru ameeleza na amefafanua kwamba kumekuwa na wimbi la watumishi kupokea rushwa kipindi wanapotoa huduma za afya katika Vituo vya Afya na Zahanati na kutoa onyo kali kwa mtumishi yeyote wa umma atakaye jihusisha na kitendo cha kutoa na kupokea rushwa katika kutekeleza miradi ya maendeleo na hasa katika Sekta ya Afya.

“Kuna kashfa ya rushwa sana gari la wagonjwa Serikali imetoa bure mafuta ni ya Serikali hivyo toeni huduma bure, sehemu ninayoingalia kwa tahadhari ni kwenye eneo la Afya”Alisisitiza Mkurugenzi Bw.Mafuru.

Kwa upande wake Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bi.Samina Gullums amewa kumbusha watumishi wa Halmashauri hiyo  kuwa na nidhamu katika utendaji kazi,kuzingatia mavazi yenye heshima wanapokuwa kazini na baada ya kazi na kuzingatia lugha nzuri  wakati wote wanapo hudumia wananchi.

Sambamba na hayo Bi.Gullums ametoa rai kwa watumishi wote Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kuendelea kujifunza kwa bidii mfumo wa PEPMIS ambapo zoezi la kuingiza majukumu katika mfumo  limeisha na zoezi linaloendelea sasa ni kuingiza kazi za kila siku na endapo mtumishi hataingiza kazi zake kwenye mfumo huo ambao umeunganishwa na mfumo wa mishahara atakosa stahiki zake kupata mshahara.

Naye, Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw. Christopher Legonda ametoa wito kwa Viongozi na Watendaji kuendelea kutoa elimu na hamasa kwa Wananchi na Wazazi kuendelea kuchangia chakula shuleni ili wanafunzi waweze kupata mlo kamili wawopo shuleni.

Bw.Legonda amefafanua kwamba Serikali inatoa fedha nyingi kwenye miradi ya maendeleo na kuwataka watenda wa kata,Vijiji na Walimu kusimamia kwa kikamilifu na kuwashirikisha wananchi katika miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati na kuacha vitendo vya udokozi ambavyo vinaweza kuleta migogoro kwa wananchi.

Wakati huo huo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw.Clement Morabu ameeleza na kusistiza kwamba watumishi hasa Sekta ya Afya watoe huduma nzuri kwa wananchi na kutumia lugha zenye staha wanapo wahudumia  bila kubagua mtu yeyote na kuongeza kuwa gari la wangojwa ambalo lilikuwa limeharibika ndani ya wiki mbili litakuwa limetengemaa na kuhudumia watu wa tarafa ya Mbarika.

Baadhi watumishi wa Tarafa ya Mbarika wakifuatilia na kusikiliza maelekezo ya Mkurugenzi Mtendaji katika kikao hicho ambacho kilichofanyika siku ya Jumamosi katika shule ya sekondari Mbarika.

Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bi. Samina Gullums akiongea na Watumishi wa Tarafa ya Mbarika  ambapo aliwataka kuzingatia maelekezo waliyoyapewa katika kikao hicho.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.