• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Chacha aridhishwa na Miradi ya BOOST ya Bilioni 1.5 Wilayani Misungwi

Imewekwa : October 6th, 2023


Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Paulo Chacha aridhishwa na utekelezaji wa Miradi ya Boost wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1,512,500,000/= zimetumika katika mradi  huo Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza

Hayo yamebainishwa katika ziara Ukaguzi na ufuatiliaji wa utekelezaji wa Miradi Wilayani Misungwi Mhe, Paulo Chacha ameeleza kuridhishwa na utekelezaji wa Miradi ya Boost ambapo miradi hiyo iliyokuwa na lengo la kutoa elimu bora kwa Wanafunzi kupitia ujenzi wa Madarasa yaliojengwa, vyoo pamoja na madawati uliotekelezwa kwa Shule za Msingi tisa Wilayani humo.

Mhe, Chacha amesema kupitia Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan Wilaya ya Misungwi  imefanikiwa kupata fedha na kuhakikisha kazi hizo zinafanyika kwa kasi ambayo inaridhisha ambapo changamoto kama vile huduma ya maji na umeme zimewasilishwa na zimetatuliwa na zitaendelea kushughulikiwa  kwa wakati  kabla ya mwezi Disemba mwaka 2023 ili kurahisisha shughuli za kuongeza kiwango cha elimu Wilayani nataifa kwa ujumla.  

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi Mhe, Abdi Makange akiwa katika kijiji cha Mwakiligili Wilayani Misungwi amesema Watumishi wamejitaidi kikamilifu katika kuhakikisha miradi hiyo ya Boost Wilayani Misungwi umezidi kwenda vyema kwa kujengwa kwa kiwango cha hali ya juu na hatimaye kukidhi na kujibu changamoto za watoto kutokwenda shule kwa uhaba wa majengo ya madarasa pamoja na madawati.

Mhe, Makange amewasihi na kuwataka Wananchi na Wakazi wa Kijiji cha Mwagiligili kuyatunza  na kuyalinda madarasa ,madawati pamoja na vyoo ili kuwanufaisha wao na kizazi kijacho na kuwakumbusha wazazi kuwahimiza na kuwapeleka watoto shule ili wapate elimu na maadili mazuri.

Naye Afisa Vifaa na Takwimu Msingi Wilaya ya Misungwi na Mratibu wa Mradi wa Boost na SWASH Bw Godfrey Majura amesema kiasi kilichotengwa kwa ajili ya mradi wa boost  ni shilingi bilioni 1,512,500,000/=  kwa shule takribani 9 zimefikiwa na mradi huo.

Bw Godfrey Majura amesema shule takribani 2 ambazo ni shule ya msingi Mbela na shule ya msingi Ntende (Mwabebea) zimejengwa upya na shule zilizobaki takribani 7  kufanyiwa ukarabati na nyongeza ya kujenga majengo ya Madarasa pamoja na vyoo hivyo zoezi la ujenzi limefanyika vizuri na kwa ubora.

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Shilalo Bw, Samson Selema  amesema kuwa hapo awali watoto walikua wakipata adha kubwa wakiwa darasani kwani iliwabidi kujazana hatimaye hali hio kwa sasa imetatuliwa ambapo amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Misungwi  pamoja na Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo y sekta zote ikiwemo elimu na kuwaomba waendelee na moyo huo ili kuwletea maendeleo ya dhati Wananchi.

Halmashauri ya Misungwi imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo sekta ya Afya, Barabara, Maji pamoja na sektaya Elimu ambapo kwa upande wa elimu kupitia mradi wa Boost imeweza kutekelezashile hizo mi pamoja na shule ya msingi mbele,shule ya msingi kagera,shule ya msingi ntende ,shule ya msingi iteja,shule ya msingi nyabuhele,shule ya msingi chatta,busegeja shule ya msingi,igwta shule ya msingi,shule ya msingi mwagiligili.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Paulo Chacha akikagua Mradi wa BOOST katika Shule ya Msingi Kagera Kata ya Usagara hivi karibuni ambapo aliridhishwa na Mradi huo. 

Mwonekano wa baadhi ya Majengo ya Mradi wa BOOST yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 1.5 miongoni mwa Shule tisa katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.