• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi azindua msimu wa Kilimo cha Pamba mwaka 2020/2021

Imewekwa : November 23rd, 2020

Maafisa Ugani Wilayani Misungwi, Mkoani Mwanza waagizwa kuwatembelea Wakulima wa kilimo cha pamba  mashambani na kutoa ushauri na maelekezo ya kulima kitaalamu ili kupata mazao ya kutosha katika msimu huu.

Akizungumza katika uzinduzi wa msimu wa Kilimo cha Pamba katika Kijiji cha Maganzo Kata ya Mondo Wilayani humu Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda amewaagiza Maafisa Kilimo wote kuhakikisha wanawatembelea Wakulima wa pamba na kuona hali na maendeleo ya kilimo na kutatua changamoto wanazokumbuna nazo kwenye kilimo na kuwashauri kulima kitaalamu.

Amewataka maafisa Ugani kuwafuata Wakulima mashambani na ktatua changamoto zote za Kilimo na kuwashauri na kupata takwimu na taarifa zote za Wakulima wanalima mazao gani na Hekari ngapi na maendeleo yote kwa ujumla.

“ Ni aibu sana unamkuta kijana anacheza bao na karata wakati huu wa Kilimo na kuagiza Watendaji wa Kata na Vijiji kuwakamata wote wanaozurula na kucheza bao na kuhakikisha wote wanaenda kulima mashambani  na kuzalisha” Amesisitiza Juma Sweda.

Juma Sweda amewataka Wananchi wote kuendelea kulima kilimo cha Pamba kwa lengo la kujipatia fedha na kujiongezea kipato na kuimarisha uchumi wa familia na taifa kwa ujumla.

Amewasihi Wakulima pia kulima mazao ya Chakula likiwemo zao la Viazi vitamu na mahindi ili kuweza kuongeza upatikanaji wa Chakula na kujenga afya na maisha ya Wananchi, na na kueleza kwamba msimu umeanza kila mtu aanze kulima na kuacha uzembe na uvivu hivyo Waanchi wote wanapaswa kuwajibika katika Kilimo na kuzitumia vyema mvua za vuli.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Kilimo na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kwilasa Mahigu ameeleza katika taarifa ya Idara kwamba Halmashauri katika msimu huu wa 2020/2021 wamepanga kulima mashamba ya pamba zaidi ya Hekta elfu kumi mia sita themanini na saba (10,687) ambapo wastani wa Wakulima wanaolima zao la Pamba ni asilimia 56 waliopo kwenye Kaya zipatazo  elfu thelethini mia nne  na kumi na nane (30,418) na wanatarjia mavuno ya Pamba yapatayo tani 10,687.

Amesema kwamba mikakati iliyowekwa ni pamoja na kuhamasisha Wakulima wengi kujitokeza kulima zao la pamba ili kupata mavuno bora na kuleta tija katika kilimo cha pamba Wilayani Misungwi pamoja na kuwa na mashamba ya mfano ambapo Maafisa Ugani wote wameelekezwa kuwa na mashamba ya mfano na kulima kwa mfano sambamba na hilo wanatakiwa kusimamia na kushauri wakulima wasiopungua kumi na tano.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Juma Sweda (wa pili kulia) akipanda mbegu za Pamba wakati wa Uzinduzi wa msimu wa Kilimo cha Pamba katika shamba la Mkulima mmoja Kijiji cha Maganzo Wilayani Misungwi, akiwa na baadhi ya Viongozi wa Wilaya akiwemo Katibu Tawala Petro Sabatto (wa kwanza kulia) pamoja na Wakulima walioshiriki zoezi la Kilimo cha Pamba.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.