• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi atoa siku tano kwa Uongozi wa Shule kuhakikisha Wanafunzi wanahamia katika Madarasa mapya

Imewekwa : September 27th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi,Mkoani Mwanza,Mhe,Juma Sweda aiagiza Kamati ya Shule ya Msingi Isela kuhakikisha Wanafunzi wanahama kutoka Shule ya Msingi Busagara kwenda katika Shule ya Msingi mpya ya Isela mara baada ya kukamilika kwa vyumba vinne vya  madarasa vya Shule hiyo.

Akizungumza wakati wa  Ziara ya kikazi katika Kata ya Usagara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe,Juma Sweda aliutaka Uongozi na Kamati ya Shule ya Msingi Isela kuhakikisha inawahamisha Wanafunzi hao na kuanza kusomea katika vyumba vinne vya madarasa vya Shule hiyo vilivyojengwa na kukamilika mwezi Julai mwaka 2018 ili kuweza kusaidia watoto wa Shule kusoma vizuri na kuleta tija na hatimaye kuongeza ufaulu kutokana na mazingira bora ya kufundisha na kujifunzia.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe, Juma Sweda akikagua Ujenzi wa Vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Msingi Isela .

Mhe, Juma Sweda alishangazwa na kusikitishwa baada ya kukagua na kukuta vyumba hivyo vya madarasa kukamilika lakini Wanafunzi hawajaanza kuvitumia badala yake wanaendelea kubanana katika madarasa ya Shule ya Msingi Mama ya Busagara,amewataka Viongozi wa Halmashauri,Kamati ya Shule kutekeleza agizo hilo kufikia siku ya Jumatatu tarehe 1 oktoba 2018 tayari Wanafunzi waanze kusomea katika Madarasa hayo.

Amewataka Viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Idetemya wakishirikiana na Kamati ya Shule kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa Shimo la Choo cha Wanafunzi ndani ya Wiki mbili kwa kutumia nguvu kazi na michango ya Wananchi kwa ajili ya matumizi ya Wanafunzi na kuondokana na milipuko ya magonjwa mbalimbali ikiwemo Kichocho,Minyooo na UTI yanayosababishwa na ukosefu wa Choo .

    Jengo la Choo chenye matundu 16 kilichojengwa katika Shule ya Msingi Isela ambapo ujenzi wa Shimo la maji machafu unaendelea kukamilishwa. 

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Isela,Bi Paskazia Changaka amesema kuwa Mradi wa ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa,ofisi ya Walmu,Choo cha Wanafunzi na Walimu umekamilika na fedha iliyotumika ni shillingi 66,600,000/= zilizotolewa na Serikali na wamejenga kwa kutumia mafundi ujenzi Wakazi kwa usimamizi wa Mhandisi wa ujenzi wa Halmashauri na Kamati ya ujenzi na ujenzi umeafanyika kwa kiwango na ubora kulingana na thamani ya fedha.

Mwalimu Mkuu huyo ameahidi kutekeleza maelekezo na maagizo ya Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Kamati ya Shule na kuhakikisha wanafunzi  wa darasa la awali, darasa la kwanza, darasa la pili, darasa la tano na Sita  wanahama na kuanza  kusomea katika vyumba hivyo vya madarasa na Wanafunzi wa darasa la tatu na darasa la Nne watabaki katika Madarasa ya Shule ya Msingi Busagara na kwamba  wataendelea kusimamia ukamilishaji wa ujenzi wa shimo la Choo cha Wanafunzi ili kiweze kukamilika mapema na kuanza kutumika lakini kwa sasa wataendelea kutumia Choo kilichopo katika Shule ya Msingi Busagara.

Mwalimu Mkuu,Bi Changaka alitoa takwimu za Wanafunzi wa Shule hiyo kwamba kuna jumla ya Wanafunzi 703 wanaosoma darasa la awali hadi darasa la saba ambao wamesajiliwa na wanaendelea na masomo kama kawaida na kwamba hali ya maendeleo ya kitaaluma ni nzuri na inaridhisha na kuwaomba ushirikiano zaidi Wananchi waweze kujitoa kuchangia shughuli za maendeleo ya Shule yao.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi,Mhe, Juma Sweda (Katikati) akifanya Ukaguzi kwenye Kiwanda cha Uzalishaji wa Mawe na Kokoto cha KASKO (Kulia ni Meneja wa Kiwanda hicho Bw,Japhet Gerasa akimwelekeza na kumwonyesha Mkuu wa Wilaya namna Uzalishaji wa Kokoto na Matofali unavyofanyika

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Bi, Dianah Kuboja amesema kwamba Menejimenti imesimamia kikamilifu ujenzi mwa madarasa hayo kupitia kwa Wataalam wa Ujenzi wa Halmashauri na mradi umetekelezwa kwa ubora na kiwango ambapo kanuni, taratibu na miongozo ya Shule inaafahamika na ipo wazi na Idara ya Elimu Msingi itaendelea kufuatilia utekelezaji wamiradi na shughuli zote zinazohusu Sekta ya Elimu pamoja na kuhakikisha wanasimamia ujenzi wa shimo la Choo na unakamilika kwa wakati ili kuwanusuru na kuwaondolea adha Wanafunzi.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ameweza pia kukagua miradi na shughuli zinazoendelea kutekelezwa katika maeneo ya Kata ya Usagara ikiwemo Ujenzi wa Sekondari ya Kijiji cha Nyang”homango, kukagua shughuli katika Kiwanda cha Uzalishaji wa Mawe na Kokoto cha KASKO,na Nyanza Roads Works, Mradi wa Maji bomba wa Usagara, Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Polisi Usagara pamoja na Mkutano wa hadhara wa Kijiji cha Usagara.

Mataofali yanayozalishwa kwa kutumia Vumbi la Kokoto na Mawe katika Kiwanda cha KASKO cha Wilayani Misungwi.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi anaendelea na ziara ya kukagua na kuona utekelezaji wa miradi na shughuli za maendeleo katika Kata zote 27 zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi akiambatana na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri..

 

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.